Je mwanamke anaweza kujijuwa ni mjamzito baada ya muda gani.
Mdau anauliza ni muda gani mwanamke anaweza kujijuwa kuwa amepata ujauzito.
Habar,, mwanamke anaweza kujijua ni mjamzito baada ya muda gani?
? Wanawake wengi wamekuwa wakijiuliza swali hili. Wengine ni kutokana na shauku ya kutaka ujauzito na wengine ni kutokana na woga wa kupata ujauzito.
? Ukweli ni kuwa sio rahisibkujuwa kabla ya kuanza kuona dalili. Kuna wengine dalili huanza kujitokeza ndani ya wiki 2 na wapo wengine ndani ya wiki tatu hadi mwezi baada ya kukosa siku zake. Hata hivyo wapo wengine ndani ya wiki moja.
? Miongoni mwa dalili za ujauzito za mwanzoni kabisa ni pamoja na: -
? 1. Maumivu ya kichwa, kizunguzungu ama kichwa kuhisi chepesi
? 2. Maumivu ya tumbo, haya yanaweza kuwa makali ama ya kawaida. Yanaweza kutokea kwa muda mfupi kisha kukata.
? 3. Kutokea na damu, hii inajulikana kama implantation bleending. Yenyewe ni kidogo ama inaweza kutoka vitone tu.
? 4. Maumivu ya matiti ama yanaweza kujaa kidogo. Unaweza kuhisi maumivu kidogo unapoyaminya matiti yako.
? 5. Kichefuchefu, mara nyingi dalili hii haitokeagi mwanzoni sana. Hata hivyo inaweza kutokea muda wowote ule.
? 6. Kutopata siku zako. Hii hutokea pale mwanamke anapozikosa siku zake. Hapo ataanza kuwaza ni ujauzito. Hata hivyo kukosa siku inaweza kusababishwa na mambo mengi ikiwepo maradhi, hali ya hewa, vyakula, misongo ya mawazo, matatizo ya homoni.
? Ni vyema kwenda kituo cha afya upate vipimo ama uzungumze na daktari. Unaweza kupata hizo dalili na isiwe ni ujauzito.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Madhara ya mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kama mtoto alizaliwa na uzito mkubwa.
Soma Zaidi...Dalili za mimba ya mtoto wa kiume ama mtoto wa kike
Posti hii inakwenda kukueleza jinsi ya kuwjuwa kama mtoto ni wa kike ama wa kiume.
Soma Zaidi...MAUMIVU WAKATI WA TENDO LA NDOA
Maumivu wakati wa tendo la ndoa kitaalamu huitwa dyspareunia.
Soma Zaidi...Mabadiliko kwenye tumbo la uzazi wa Mama anapobeba Mimba.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye tumbo la uzazi la Mama pindi anapobeba mimba, ni mabadiliko yanayotokea kwa mwanamke anapobeba mimba kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...CHANGAMOTO ZA UJAUZITO, NA DALILI ZAKE NA NAMNA YA KUKABILIANA NAZO
Utawezaje kukabiliana na changamoto za ujauzito, je ni zipi changamoto hizo. Hapa nitakujuza.
Soma Zaidi...