Mdau anauliza ni muda gani mwanamke anaweza kujijuwa kuwa amepata ujauzito.
Habar,, mwanamke anaweza kujijua ni mjamzito baada ya muda gani?
? Wanawake wengi wamekuwa wakijiuliza swali hili. Wengine ni kutokana na shauku ya kutaka ujauzito na wengine ni kutokana na woga wa kupata ujauzito.
? Ukweli ni kuwa sio rahisibkujuwa kabla ya kuanza kuona dalili. Kuna wengine dalili huanza kujitokeza ndani ya wiki 2 na wapo wengine ndani ya wiki tatu hadi mwezi baada ya kukosa siku zake. Hata hivyo wapo wengine ndani ya wiki moja.
? Miongoni mwa dalili za ujauzito za mwanzoni kabisa ni pamoja na: -
? 1. Maumivu ya kichwa, kizunguzungu ama kichwa kuhisi chepesi
? 2. Maumivu ya tumbo, haya yanaweza kuwa makali ama ya kawaida. Yanaweza kutokea kwa muda mfupi kisha kukata.
? 3. Kutokea na damu, hii inajulikana kama implantation bleending. Yenyewe ni kidogo ama inaweza kutoka vitone tu.
? 4. Maumivu ya matiti ama yanaweza kujaa kidogo. Unaweza kuhisi maumivu kidogo unapoyaminya matiti yako.
? 5. Kichefuchefu, mara nyingi dalili hii haitokeagi mwanzoni sana. Hata hivyo inaweza kutokea muda wowote ule.
? 6. Kutopata siku zako. Hii hutokea pale mwanamke anapozikosa siku zake. Hapo ataanza kuwaza ni ujauzito. Hata hivyo kukosa siku inaweza kusababishwa na mambo mengi ikiwepo maradhi, hali ya hewa, vyakula, misongo ya mawazo, matatizo ya homoni.
? Ni vyema kwenda kituo cha afya upate vipimo ama uzungumze na daktari. Unaweza kupata hizo dalili na isiwe ni ujauzito.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Posti hii inahusu msaada kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi, hizi ni huduma ambazo utolewa kwa wale wenye maumivu ya tumbo la hedhi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa watu waliopata maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi, ni faida wanazozipata waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi.
Soma Zaidi...Kupungua kwa idadi ya mbegu za kiume kunamaanisha kuwa Majimaji (shahawa) unayotoa wakati wa kufika kileleni huwa na mbegu chache kuliko kawaida. Hesabu yako ya manii inachukuliwa kuwa chini kuliko kawaida ikiwa una chini ya mbegu milioni 15. Kuwa na idad
Soma Zaidi...SIKU YA KUPATA UJAUZITO Mimba hutokea pindi mbegu ya kiume (sperm) inapokutana na yai la mwanamke (ova) na kuungana kwa pamoja kutengeneza selli moja iitwayo zygote.
Soma Zaidi...Hivi unadhani kuharisha ni katika dalili za mimba, vipi kuhusu kutopata choo pia inaweza kuwa ni ujauzito?
Soma Zaidi...Posti inahusu zaidi njia maalum za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha,Ni njia za uzazi ambazo wanaonyesha wanatumia kwa sababu kuna njia nyingine zikitumiwa na wanaonyonyesha zinaweza kuleta matatizo kwa watoto au kusababisha maziwa kutokuwa na vitamini v
Soma Zaidi...