Je mwanamke anaweza kujijuwa ni mjamzito baada ya muda gani.

Mdau anauliza ni muda gani mwanamke anaweza kujijuwa kuwa amepata ujauzito.

Habar,, mwanamke anaweza kujijua ni mjamzito baada ya muda gani?

 

👉 Wanawake wengi wamekuwa wakijiuliza swali hili.  Wengine ni kutokana na shauku ya kutaka ujauzito na wengine ni kutokana na woga wa kupata ujauzito. 

 

🤏 Ukweli ni kuwa sio rahisibkujuwa kabla ya kuanza kuona dalili. Kuna wengine dalili huanza kujitokeza ndani ya wiki 2 na wapo wengine ndani ya wiki tatu hadi mwezi baada ya kukosa siku zake. Hata hivyo wapo wengine ndani ya wiki moja. 

 

👍 Miongoni mwa dalili za ujauzito za mwanzoni kabisa ni pamoja na: -

🐦 1. Maumivu ya kichwa,  kizunguzungu ama kichwa kuhisi chepesi 

 

🐦 2. Maumivu ya tumbo, haya yanaweza kuwa makali ama ya kawaida. Yanaweza kutokea kwa muda mfupi kisha kukata. 

 

🐦 3. Kutokea na damu,  hii inajulikana kama implantation bleending. Yenyewe ni kidogo ama inaweza kutoka vitone tu. 

 

 🐔 4. Maumivu ya matiti ama yanaweza kujaa kidogo. Unaweza kuhisi maumivu kidogo unapoyaminya matiti yako. 

 

🐔 5. Kichefuchefu, mara nyingi dalili hii haitokeagi mwanzoni sana. Hata hivyo inaweza kutokea muda wowote ule.

 

🩸 6. Kutopata siku zako. Hii hutokea pale mwanamke anapozikosa siku zake. Hapo ataanza kuwaza ni ujauzito. Hata hivyo kukosa siku inaweza kusababishwa na mambo mengi ikiwepo maradhi, hali ya hewa, vyakula, misongo ya mawazo, matatizo ya homoni. 

 

🚑 Ni vyema kwenda kituo cha afya upate vipimo ama uzungumze na daktari. Unaweza kupata hizo dalili na isiwe ni ujauzito. 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 4220

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 web hosting    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Huduma kwa wanaopata hedhi zaidi ya mara moja kwa mwezi

Posti hii inahusu zaidi huduma kwa wanaoingia kwenye siku zao zaidi ya mara moja kwa mwezi.

Soma Zaidi...
Kwa mjamzito kuumia wakati wa tendo la ndoa tatizo linaweza kuwa ni nini?

Je unaweza kunielezaKwa mjamzito kuumia wakati wa tendo la ndoa tatizo linaweza kuwa ni nini?

Soma Zaidi...
Dali za udhaifu wa mbegu za kiume.

Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo zinaweza kujitokeza na zikaonesha kwamba mbegu za kiume ni dhaifu au ni chache.

Soma Zaidi...
Uume ukiwa unaingia na ukiwa ndani nahic maumivu Kama uke unawaka Moto tafadhali nishauri

Je unasumbuliwa namaumivi wakati wa nlishiriki tendo la ndoa ama baada. Huwenda post hii ikakusaidia.

Soma Zaidi...
Ay ni iv kipimo cha mimb uanz kutoa majb ndan ya mda gan wik mwez au iko vipi?

Kipimo cha Mlimba huweza kuonyesha mimba changa mapema sana. Pia ni rahisi kutumia na kinapatikana kwa bei nafuu. Je ungeoendavkujuwa ni muda gani kinatoa majibu sahihi?

Soma Zaidi...
Siku za hatari, siku za kubeba mimba

Hizi ni siku hatari kwa mwanamke ambazo ni ahisi kwake kubeba mimba, siku nitakueleza ni zipi na ni zipi sifa zake

Soma Zaidi...
Kaka nasumbuliwa saan na tatizo la kuwasha kwenye kichwa Cha uume Sijui nifanyaje

Je kichwa cha uume wako kinawasha, na je kinatoa majimaji kwenye njia ya mkojo, una muda ganinavtatizo hili. Na je ulishiriki ngono zembe siku za hivi karibuni?

Soma Zaidi...
SABABU ZA KUTOKA KWA MIMBA (sababu za kuharibika kwa ujauzito)

Tafiti zinaonesha kuwa karibia asilimia 10% mpaka 25% ya wanawake wanaopata ujauzito, mimba zao hutoka.

Soma Zaidi...
Vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito

Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito, kwa sababu kuna sababu nyingi ambazo Usababisha mwanamke kushindwa kupata ujauzito kama tutakavyoona hapo mbeleni

Soma Zaidi...