Mdau anauliza ni muda gani mwanamke anaweza kujijuwa kuwa amepata ujauzito.
Habar,, mwanamke anaweza kujijua ni mjamzito baada ya muda gani?
👉 Wanawake wengi wamekuwa wakijiuliza swali hili. Wengine ni kutokana na shauku ya kutaka ujauzito na wengine ni kutokana na woga wa kupata ujauzito.
🤏 Ukweli ni kuwa sio rahisibkujuwa kabla ya kuanza kuona dalili. Kuna wengine dalili huanza kujitokeza ndani ya wiki 2 na wapo wengine ndani ya wiki tatu hadi mwezi baada ya kukosa siku zake. Hata hivyo wapo wengine ndani ya wiki moja.
👍 Miongoni mwa dalili za ujauzito za mwanzoni kabisa ni pamoja na: -
🐦 1. Maumivu ya kichwa, kizunguzungu ama kichwa kuhisi chepesi
🐦 2. Maumivu ya tumbo, haya yanaweza kuwa makali ama ya kawaida. Yanaweza kutokea kwa muda mfupi kisha kukata.
🐦 3. Kutokea na damu, hii inajulikana kama implantation bleending. Yenyewe ni kidogo ama inaweza kutoka vitone tu.
🐔 4. Maumivu ya matiti ama yanaweza kujaa kidogo. Unaweza kuhisi maumivu kidogo unapoyaminya matiti yako.
🐔 5. Kichefuchefu, mara nyingi dalili hii haitokeagi mwanzoni sana. Hata hivyo inaweza kutokea muda wowote ule.
🩸 6. Kutopata siku zako. Hii hutokea pale mwanamke anapozikosa siku zake. Hapo ataanza kuwaza ni ujauzito. Hata hivyo kukosa siku inaweza kusababishwa na mambo mengi ikiwepo maradhi, hali ya hewa, vyakula, misongo ya mawazo, matatizo ya homoni.
🚑 Ni vyema kwenda kituo cha afya upate vipimo ama uzungumze na daktari. Unaweza kupata hizo dalili na isiwe ni ujauzito.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa mpaka siku ya kujifungua Kama mume wake pamoja na yeye akiwa Hana maambukizi ya zinaa na Kama akiona dalili zozote zile za hatari ndio hataruhusiwa kushiriki tendo la ndoa.
Soma Zaidi...posti hii inaelezea kuhusiana tatizo la muingiliano wa majimaji ya seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito ambao hujulikana Kama Amniotic Fluid Embolism ni hali adimu lakini mbaya ambayo hutokea wakati Maji ya amniotiki Majimaji ambayo huzunguka mtot
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ujauzito baada ya tendo la ndoa
Soma Zaidi...Kipimo cha mimba kwa mkojo kimekuwa kikitumika sana kuangalia ujauzito. Kipimo hiki kinapotumika vibaya kinaweza kukupa majibu ya uongo. Kuwa makini na ujue muda sahihi.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, hali hii utokea kwa watoto wadogo wakati wa kuzaliwa kwa sababu maalum kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto, ni Maambukizi ambayo yanaweza kutokea kwenye kitovu cha mtoto pale ambapo mtoto amezaliwa inawezekana ni kwa sababu ya hali ya mtoto au huduma kuanzia kwa wakunga na wale wanaotumia mtoto.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama ambaye anakuwa amepasuka mfuko wa kizazi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa mama, zoezi hili ufanyika kila mwezi pale mama anapokuja kwenye mahudhurio kwa kufanya hivyo tunaweza kuja maendeleo ya mtoto kwa kila mwezi.
Soma Zaidi...Kipimo cha Mlimba huweza kuonyesha mimba changa mapema sana. Pia ni rahisi kutumia na kinapatikana kwa bei nafuu. Je ungeoendavkujuwa ni muda gani kinatoa majibu sahihi?
Soma Zaidi...