Mdau anauliza ni muda gani mwanamke anaweza kujijuwa kuwa amepata ujauzito.
Habar,, mwanamke anaweza kujijua ni mjamzito baada ya muda gani?
? Wanawake wengi wamekuwa wakijiuliza swali hili. Wengine ni kutokana na shauku ya kutaka ujauzito na wengine ni kutokana na woga wa kupata ujauzito.
? Ukweli ni kuwa sio rahisibkujuwa kabla ya kuanza kuona dalili. Kuna wengine dalili huanza kujitokeza ndani ya wiki 2 na wapo wengine ndani ya wiki tatu hadi mwezi baada ya kukosa siku zake. Hata hivyo wapo wengine ndani ya wiki moja.
? Miongoni mwa dalili za ujauzito za mwanzoni kabisa ni pamoja na: -
? 1. Maumivu ya kichwa, kizunguzungu ama kichwa kuhisi chepesi
? 2. Maumivu ya tumbo, haya yanaweza kuwa makali ama ya kawaida. Yanaweza kutokea kwa muda mfupi kisha kukata.
? 3. Kutokea na damu, hii inajulikana kama implantation bleending. Yenyewe ni kidogo ama inaweza kutoka vitone tu.
? 4. Maumivu ya matiti ama yanaweza kujaa kidogo. Unaweza kuhisi maumivu kidogo unapoyaminya matiti yako.
? 5. Kichefuchefu, mara nyingi dalili hii haitokeagi mwanzoni sana. Hata hivyo inaweza kutokea muda wowote ule.
? 6. Kutopata siku zako. Hii hutokea pale mwanamke anapozikosa siku zake. Hapo ataanza kuwaza ni ujauzito. Hata hivyo kukosa siku inaweza kusababishwa na mambo mengi ikiwepo maradhi, hali ya hewa, vyakula, misongo ya mawazo, matatizo ya homoni.
? Ni vyema kwenda kituo cha afya upate vipimo ama uzungumze na daktari. Unaweza kupata hizo dalili na isiwe ni ujauzito.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Posti hii inahusu zaidi hatari za kutokwa na damu wakati wa ujauzito, hali hii utokea wakati wa ujauzito ambapo Kuna baadhi ya wajawazito utokwa na damu jambo ambalo hatupaswi kutarajia kwa sababu tunafahamu kabisa mama akishapata ujauzito na damu zinakom
Soma Zaidi...Posti hii inakwenda kukueleza jinsi ya kuwjuwa kama mtoto ni wa kike ama wa kiume.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi sababu za ugumba kwa wanawake, ni sababu ambazo upelekea wanawake wengi kuwa wagumba ukizingatia kuwa wanazaliwa wakiwa na uwezo kabisa wa kupata watoto lakini kwa sababu mbalimbali za kimazingira wanakoswa watoto, zifuatazo ni saba
Soma Zaidi...Nini humaanisha kama chuchu zinauma na hupati period mwanaidi mrefu.
Soma Zaidi...Korodani ni kiungo muhimu kwa mwanaume, katika afya ya uzazi. Unaweza kusema ni kiwanda cha kutengeneza mbegu za kiume. Kiungo hiki ni sawa na ovari kwa mwanamke.
Soma Zaidi...Kufanya tendo la ndoa wakati wa ujauzito kina faida nyingi kwa mama na mtoto. Miongni mwa faida hizo ni kuimarisha mfumo wa kinga wa mama, kumuondolea stress na ukuajinmzuri wa mimba
Soma Zaidi...