picha

Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto.

Posti hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto, ni Maambukizi ambayo yanaweza kutokea kwenye kitovu cha mtoto pale ambapo mtoto amezaliwa inawezekana ni kwa sababu ya hali ya mtoto au huduma kuanzia kwa wakunga na wale wanaotumia mtoto.

Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto.

1. Kwanza kabisa tunajua kuwa mtoto akiwa tumboni mwa Mama  anakuwa ameungana na mama kupitia kwenye plasenta ambapo wakati wa kuzaliwa kitovu ukatwa na plasenta utolewa kwa hiyo hicho kitovu kinapaswa kutunza vizuri ili kisiweze kupata Maambukizi ila kwa wakati mwingine kitovu hicho kinaweza kupata Maambukizi kwa sababu zifuatazo.

 

2. Pengine kunakuwepo kwa Maambukizi kutoka kwa mama wakati wa kujifungua kwa sababu kuna wadudu ambao wanakaa kwenye nje ya plasenta pale mtoto akitolewa nje na kukata kitovu ili kutenganisha na plasenta wadudu wanaweza kuingia kwenye kitovu na kusababisha maambukizi. Wadudu hao wanaweza kutokana na kuwepo kwa kaswende hasa kwa wamama ambao hawakupima walipogundua kwa na mimba na pia Maambukizi kutokana na Magonjwa mbalimbali.

 

3. Chupa ya Mama kupasuka wakati wa uchungu na Mama akakaa mda mrefu bila kujifungua.

Kuna kipindi ambapo chupa ya Mama huwa unapaswa na Mama anakaa mda mrefu bila kujifungua kwa kawaida chupa ya Mama ikifungua Mama ukaa mda kidogo na baadae anajifungua ila hadipojifungua wadudu wengine wanaweza kuingia kwenye kitovu na baada ya mtoto kutoka nje ya tumbo la Mama na kitovu kukatwa ili kutenganisha na plasenta wadudu wanaweza kuwa kwenye kitovu na kuleta Maambukizi.

 

4. Watoa huduma kutumia vifaa vichafu wakati wa kukata kitovu.

Kuna wakati mwingine watoa huduma wanakuwa wazembe katika kutoa huduma kwa sababu wanatumia vifaa ambavyo siyo visafi na wakati mwingine vinakuwa na kutu hatimaye Maambukizi yanaweza kutokea kwenye kitovu.

 

5.Hasa hasa wale wakunga Jadi wa mitaani utakuta wanatumia wembe mmoja kwa watoto mbalimbali au pengine visu na wanavisafisha kwa njia za kawaida hatimaye wanasababisha Maambukizi kwenye kitovu, kwa hiyo akina Mama wanapaswa kujifungulia hospitalini ili kuepuka hali za kuwepo kwa Maambukizi.

 

6. Walezi au wazazi kutokitunza vizuri kitovu.

Kuna wakati mwingine wazazi au walezi wa mtoto wanakuwa wazembe katika kutunza kitovu cha mtoto kwa mara nyingine wanatumia mila zao wanazozijua ili kutunza kitovu hali ambayo  Usababisha Maambukizi kwa mfano kuna makabila wanaosha kitovu kwa maji yaliyochanganywa naiti shamba hali ambayo Usababisha Maambukizi kwenye kitovu.

 

7.Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kuwatunza watoto wao vizuri na kuepuka madhara yatokanayo na Maambukizi kwenye kitovu kwa kuhakikisha kujua kubwa kitovu hakioshwi na dawa yoyote isiyotolewa hospitalini na kuacha tabia ya kuosha kitovu na miti shamba kwa sababu huwezi kujua kuna nini katika hayo matumizi ya miti shamba.

 

8 pia akina mama wanapaswa kujifungulia hospitalini hat kama ni mbali siku za kujifungua zikifika wasogee kwa ndugu aliye karibu kwa sababu kwa wakunga wa Jadi kuna shida ya ukosefu wa vifaa kwa hiyo tabia ya kutumia kifaa kimoja na kusafisha Usababisha kuenea kwa magonjwa sio tu Maambukizi kwenye kitovu tu.

 

9.Pia na wakunga mahospitali wanapaswa kuwa waangalifu katika matumizi ya vifaa ili kuweza kuepuka tatizo la kuwepo kwa Maambukizi kwenye kitovu kwa hiyo vifaa ambavyo vitatumika vinapaswa kuandaliwa vizuri kwa kuwepo  kwa watu walio na ujuzi wa kusafisha vifaa kwa utaratibu maalum ili kuweza kuepuka Maambukizi.

 

10.Vili vile wazazi na walezi wapate elimu maalumu kuhusu namna ya kutunza kitovu cha mtoto na pia wajue wazi madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na kuwepo kwa uzembe wakati wa kutunza kitovu cha mtoto. Vile na wakunga Jadi wapewe vifaa vya kutosha wanapotoa huduma ili kuweza kuepuka madhara ya kuwepo kwa magonjwa maaambukizi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2905

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Fahamu kuhusu fangasi za ukeni

Posti hii inahusu zaidi fangasi za ukeni, hili ni tatizo kubwa ambalo linawakumba watoto, akina dada na wanawake kwa hiyo na vizuri kujua Dalili zake na kuweza kuchukua hatua mapema.

Soma Zaidi...
Kazi ya metronidazole

Posti hii zaidi kazi ya Dawa ya metronidazole katika kutibu Minyoo, ni aina ya Dawa ambayo imetumiwa na watu wengi wakaweza kupona na kuepukana na minyoo. Zifuatazo ni baadhi ya kazi za metronidazole.

Soma Zaidi...
Sababu za wajawazito kupata Bawasili.

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali ambazo zinafanya wajawazito kupata ugonjwa wa Bawasili, kwa sababu tatizo hili linawapa wakina mama wajawazito, kwa hiyo tutaona kwa nini wajawazito wanapatwa na tatizo hili sana.

Soma Zaidi...
Ujue Ute kwenye uke

Post hii inahusu zaidi Ute ambao umo kwenye uke, Ute huu utofautiana kulingana na hali ya mama aliyonayo, kama mama ana mimba uke utakuwa tofauti na yule ambaye hana mimba au kama Ute una una magonjwa na hivyo utakuwa tofauti.

Soma Zaidi...
Sababu za mwanamke kukosa hamu ya kushiriki tendo la ndoa

Posti hii inazungumzia kuhusiana na sababu zinazosababisha kukosa hamu ya kushiriki tendo la ndoa.

Soma Zaidi...
Namna ya kutunza joto la mtoto mara tu baada ya kuzaliwa.

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kutunza joto la mtoto mara tu anapozaliwa,tunajuwa wazi kuwa Mama anaweza kujifungulia sehemu yoyote ile kabla hajafika hospitalini kwa hiyo mtoto anapaswa kuwa na joto la mwili la kutosha i

Soma Zaidi...