Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto.

Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto.

Posti hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto, ni Maambukizi ambayo yanaweza kutokea kwenye kitovu cha mtoto pale ambapo mtoto amezaliwa inawezekana ni kwa sababu ya hali ya mtoto au huduma kuanzia kwa wakunga na wale wanaotumia mtoto.

Download Post hii hapa

Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto.

1. Kwanza kabisa tunajua kuwa mtoto akiwa tumboni mwa Mama  anakuwa ameungana na mama kupitia kwenye plasenta ambapo wakati wa kuzaliwa kitovu ukatwa na plasenta utolewa kwa hiyo hicho kitovu kinapaswa kutunza vizuri ili kisiweze kupata Maambukizi ila kwa wakati mwingine kitovu hicho kinaweza kupata Maambukizi kwa sababu zifuatazo.

 

2. Pengine kunakuwepo kwa Maambukizi kutoka kwa mama wakati wa kujifungua kwa sababu kuna wadudu ambao wanakaa kwenye nje ya plasenta pale mtoto akitolewa nje na kukata kitovu ili kutenganisha na plasenta wadudu wanaweza kuingia kwenye kitovu na kusababisha maambukizi. Wadudu hao wanaweza kutokana na kuwepo kwa kaswende hasa kwa wamama ambao hawakupima walipogundua kwa na mimba na pia Maambukizi kutokana na Magonjwa mbalimbali.

 

3. Chupa ya Mama kupasuka wakati wa uchungu na Mama akakaa mda mrefu bila kujifungua.

Kuna kipindi ambapo chupa ya Mama huwa unapaswa na Mama anakaa mda mrefu bila kujifungua kwa kawaida chupa ya Mama ikifungua Mama ukaa mda kidogo na baadae anajifungua ila hadipojifungua wadudu wengine wanaweza kuingia kwenye kitovu na baada ya mtoto kutoka nje ya tumbo la Mama na kitovu kukatwa ili kutenganisha na plasenta wadudu wanaweza kuwa kwenye kitovu na kuleta Maambukizi.

 

4. Watoa huduma kutumia vifaa vichafu wakati wa kukata kitovu.

Kuna wakati mwingine watoa huduma wanakuwa wazembe katika kutoa huduma kwa sababu wanatumia vifaa ambavyo siyo visafi na wakati mwingine vinakuwa na kutu hatimaye Maambukizi yanaweza kutokea kwenye kitovu.

 

5.Hasa hasa wale wakunga Jadi wa mitaani utakuta wanatumia wembe mmoja kwa watoto mbalimbali au pengine visu na wanavisafisha kwa njia za kawaida hatimaye wanasababisha Maambukizi kwenye kitovu, kwa hiyo akina Mama wanapaswa kujifungulia hospitalini ili kuepuka hali za kuwepo kwa Maambukizi.

 

6. Walezi au wazazi kutokitunza vizuri kitovu.

Kuna wakati mwingine wazazi au walezi wa mtoto wanakuwa wazembe katika kutunza kitovu cha mtoto kwa mara nyingine wanatumia mila zao wanazozijua ili kutunza kitovu hali ambayo  Usababisha Maambukizi kwa mfano kuna makabila wanaosha kitovu kwa maji yaliyochanganywa naiti shamba hali ambayo Usababisha Maambukizi kwenye kitovu.

 

7.Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kuwatunza watoto wao vizuri na kuepuka madhara yatokanayo na Maambukizi kwenye kitovu kwa kuhakikisha kujua kubwa kitovu hakioshwi na dawa yoyote isiyotolewa hospitalini na kuacha tabia ya kuosha kitovu na miti shamba kwa sababu huwezi kujua kuna nini katika hayo matumizi ya miti shamba.

 

8 pia akina mama wanapaswa kujifungulia hospitalini hat kama ni mbali siku za kujifungua zikifika wasogee kwa ndugu aliye karibu kwa sababu kwa wakunga wa Jadi kuna shida ya ukosefu wa vifaa kwa hiyo tabia ya kutumia kifaa kimoja na kusafisha Usababisha kuenea kwa magonjwa sio tu Maambukizi kwenye kitovu tu.

 

9.Pia na wakunga mahospitali wanapaswa kuwa waangalifu katika matumizi ya vifaa ili kuweza kuepuka tatizo la kuwepo kwa Maambukizi kwenye kitovu kwa hiyo vifaa ambavyo vitatumika vinapaswa kuandaliwa vizuri kwa kuwepo  kwa watu walio na ujuzi wa kusafisha vifaa kwa utaratibu maalum ili kuweza kuepuka Maambukizi.

 

10.Vili vile wazazi na walezi wapate elimu maalumu kuhusu namna ya kutunza kitovu cha mtoto na pia wajue wazi madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na kuwepo kwa uzembe wakati wa kutunza kitovu cha mtoto. Vile na wakunga Jadi wapewe vifaa vya kutosha wanapotoa huduma ili kuweza kuepuka madhara ya kuwepo kwa magonjwa maaambukizi.

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 2071

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Huduma za msingi kwa mama mjamzito na mtoto.
Huduma za msingi kwa mama mjamzito na mtoto.

Posti hii inahusu zaidi huduma muhimu anazopaswa kupewa mama mjamzito wakati akiwa na mimba, wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua yaani ndani ya masaa ishirini na manne, tunajua wazi kuwa Mama akiwa mjamzito anaweza kupata matatizo mbalimbali kwa h

Soma Zaidi...
Sababu za kuharibika kwa ujauzito na dalili zake
Sababu za kuharibika kwa ujauzito na dalili zake

Dalili za kuharibika kwa ujauzito na dalili za kuharibika kwa ujauzo

Soma Zaidi...
Chanzo cha tezidume, dalili zake na tiba zake.
Chanzo cha tezidume, dalili zake na tiba zake.

Post hii inakwenda kukufunza mambo mengi kuhusu tezi dume kama chanzo, dalili, matibabu, njia za kujikinga na mambo hatari yanayoweza kukusababishia kupata tezi dume.

Soma Zaidi...
Je nitahakikisha vipi Kama Nina ujauzito
Je nitahakikisha vipi Kama Nina ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza njia za kuhakiki Kama u-mjamzito

Soma Zaidi...
Sifa za siku za kupata mimba
Sifa za siku za kupata mimba

Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya sifa za siku za kupata mimba

Soma Zaidi...
Vyakula vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa
Vyakula vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa

Posti hii inahusu zaidi vyakula mbalimbali vya kuongeza tendo la ndoa, kwa kawaida kuna vyakula mbalimbali ambavyo watu ukitumia ili kuweza kuongeza tendo la ndoa vyakula hivyo ni kama tutakavyoona hapo baadaye

Soma Zaidi...
Watu ambao hawapaswi kutumia njia za uzazi wa mpango
Watu ambao hawapaswi kutumia njia za uzazi wa mpango

Post hii inahusu zaidi watu ambao hawapaswi kutumia njia za uzazi wa mpango, Ni watu ambao Wana matatizo mbalimbali endapo wakitumia wanaoweza kuleta madhara mbalimbali.

Soma Zaidi...
Mimi naumwa na tumbo chini ya kitovu upande wa kulia, ninapotok kushiriki tendo la ndoa ndonapata maumivu zaid pia nawashwa sehemu za siri itakuwa shida ni nin?
Mimi naumwa na tumbo chini ya kitovu upande wa kulia, ninapotok kushiriki tendo la ndoa ndonapata maumivu zaid pia nawashwa sehemu za siri itakuwa shida ni nin?

Maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa yanaweza kuwa ni dalili ya maradhi fulani, ama shida kwenye mfumo w uzazi. PID na UTI hutuhumiwa kuwa ni katika sababu hizo. Ila zipo nyingine nyingi tu. Kama ina hali hii vyema ukafika kituo cha afya

Soma Zaidi...
Sababu za kutoka mimba yenye miezi Saba na nane
Sababu za kutoka mimba yenye miezi Saba na nane

Posti hii inahusu zaidi sababu za mtoto kuzaliwa akiwa na miezi Saba na nane kwa kawaida mtoto wa hivi anakuwa hajafikisha mda wake kwa hiyo uzaliwa akiwa na miezi saba na nane, kwa hiyo kuna sababu mbalimbali kama tutakavyoona

Soma Zaidi...
Namna ya kutunza uke
Namna ya kutunza uke

Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza uke, tunajua wazi kuna magonjwa mbalimbali yanayoweza kutokea iwapo uke hautaweza kutunzwa vizuri na pia uke ukitunzwa vizuri kuna faida ya kuepuka maradhi ya wanawake kwa njia ya kutunza uke.

Soma Zaidi...