Posti hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto, ni Maambukizi ambayo yanaweza kutokea kwenye kitovu cha mtoto pale ambapo mtoto amezaliwa inawezekana ni kwa sababu ya hali ya mtoto au huduma kuanzia kwa wakunga na wale wanaotumia mtoto.
Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto.
1. Kwanza kabisa tunajua kuwa mtoto akiwa tumboni mwa Mama anakuwa ameungana na mama kupitia kwenye plasenta ambapo wakati wa kuzaliwa kitovu ukatwa na plasenta utolewa kwa hiyo hicho kitovu kinapaswa kutunza vizuri ili kisiweze kupata Maambukizi ila kwa wakati mwingine kitovu hicho kinaweza kupata Maambukizi kwa sababu zifuatazo.
2. Pengine kunakuwepo kwa Maambukizi kutoka kwa mama wakati wa kujifungua kwa sababu kuna wadudu ambao wanakaa kwenye nje ya plasenta pale mtoto akitolewa nje na kukata kitovu ili kutenganisha na plasenta wadudu wanaweza kuingia kwenye kitovu na kusababisha maambukizi. Wadudu hao wanaweza kutokana na kuwepo kwa kaswende hasa kwa wamama ambao hawakupima walipogundua kwa na mimba na pia Maambukizi kutokana na Magonjwa mbalimbali.
3. Chupa ya Mama kupasuka wakati wa uchungu na Mama akakaa mda mrefu bila kujifungua.
Kuna kipindi ambapo chupa ya Mama huwa unapaswa na Mama anakaa mda mrefu bila kujifungua kwa kawaida chupa ya Mama ikifungua Mama ukaa mda kidogo na baadae anajifungua ila hadipojifungua wadudu wengine wanaweza kuingia kwenye kitovu na baada ya mtoto kutoka nje ya tumbo la Mama na kitovu kukatwa ili kutenganisha na plasenta wadudu wanaweza kuwa kwenye kitovu na kuleta Maambukizi.
4. Watoa huduma kutumia vifaa vichafu wakati wa kukata kitovu.
Kuna wakati mwingine watoa huduma wanakuwa wazembe katika kutoa huduma kwa sababu wanatumia vifaa ambavyo siyo visafi na wakati mwingine vinakuwa na kutu hatimaye Maambukizi yanaweza kutokea kwenye kitovu.
5.Hasa hasa wale wakunga Jadi wa mitaani utakuta wanatumia wembe mmoja kwa watoto mbalimbali au pengine visu na wanavisafisha kwa njia za kawaida hatimaye wanasababisha Maambukizi kwenye kitovu, kwa hiyo akina Mama wanapaswa kujifungulia hospitalini ili kuepuka hali za kuwepo kwa Maambukizi.
6. Walezi au wazazi kutokitunza vizuri kitovu.
Kuna wakati mwingine wazazi au walezi wa mtoto wanakuwa wazembe katika kutunza kitovu cha mtoto kwa mara nyingine wanatumia mila zao wanazozijua ili kutunza kitovu hali ambayo Usababisha Maambukizi kwa mfano kuna makabila wanaosha kitovu kwa maji yaliyochanganywa naiti shamba hali ambayo Usababisha Maambukizi kwenye kitovu.
7.Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kuwatunza watoto wao vizuri na kuepuka madhara yatokanayo na Maambukizi kwenye kitovu kwa kuhakikisha kujua kubwa kitovu hakioshwi na dawa yoyote isiyotolewa hospitalini na kuacha tabia ya kuosha kitovu na miti shamba kwa sababu huwezi kujua kuna nini katika hayo matumizi ya miti shamba.
8 pia akina mama wanapaswa kujifungulia hospitalini hat kama ni mbali siku za kujifungua zikifika wasogee kwa ndugu aliye karibu kwa sababu kwa wakunga wa Jadi kuna shida ya ukosefu wa vifaa kwa hiyo tabia ya kutumia kifaa kimoja na kusafisha Usababisha kuenea kwa magonjwa sio tu Maambukizi kwenye kitovu tu.
9.Pia na wakunga mahospitali wanapaswa kuwa waangalifu katika matumizi ya vifaa ili kuweza kuepuka tatizo la kuwepo kwa Maambukizi kwenye kitovu kwa hiyo vifaa ambavyo vitatumika vinapaswa kuandaliwa vizuri kwa kuwepo kwa watu walio na ujuzi wa kusafisha vifaa kwa utaratibu maalum ili kuweza kuepuka Maambukizi.
10.Vili vile wazazi na walezi wapate elimu maalumu kuhusu namna ya kutunza kitovu cha mtoto na pia wajue wazi madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na kuwepo kwa uzembe wakati wa kutunza kitovu cha mtoto. Vile na wakunga Jadi wapewe vifaa vya kutosha wanapotoa huduma ili kuweza kuepuka madhara ya kuwepo kwa magonjwa maaambukizi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Jifunze mengi kuhusu Afya, kuwa nasi kwenye makala hii hadi mwisho.
Soma Zaidi...Maumivu ya hedhi (dysmenorrhea) ni maumivu makali au ya kubana sehemu ya chini ya tumbo. Wanawake wengi hupatwa na Maumivu ya hedhi kabla tu na wakati wa hedhi zao. Kwa wanawake wengine, usumbufu huo ni wa kuudhi tu. Kwa wengine, 
Soma Zaidi...Zijuwe dalili 17 za mimba na mimba changa, kuanzia siku ya kwanza mpaka mwezi mmoja
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia ugumba, ni njia ambazo utumiwa na wapenzi ambao wameshindwa kupata watoto hasa kwa wale ambao wamezaliwa wakiwa na uwezo wa kupata watoto lakini kwa sababu tofauti tofauti wanashindwa kupata watoto kwa hiyo njia zifu
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba kuanzia siku ya 7 Hadi ya 14
Soma Zaidi...Ni mida gani njamzito ananza kuhisi kuwa tumboni anebeba mtoto.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na Faida za Uzazi wa mpango. Uzazi wa mpango ni huduma ambazo hutoa chaguo kwa familia kuwa na idadi ya watoto wanaotaka katika muda maalum, wanahisi na mbinu iliyoamuliwa.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi viti vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid, ni jumla ya vitu vyote vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid.
Soma Zaidi...Katika post hii utajifunza ishara na dalili ninazoonyesha kuwa mimba ipo hatarini kutoka ama inaweza kuwa imeshatoka.
Soma Zaidi...