Posti hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto, ni Maambukizi ambayo yanaweza kutokea kwenye kitovu cha mtoto pale ambapo mtoto amezaliwa inawezekana ni kwa sababu ya hali ya mtoto au huduma kuanzia kwa wakunga na wale wanaotumia mtoto.
Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto.
1. Kwanza kabisa tunajua kuwa mtoto akiwa tumboni mwa Mama anakuwa ameungana na mama kupitia kwenye plasenta ambapo wakati wa kuzaliwa kitovu ukatwa na plasenta utolewa kwa hiyo hicho kitovu kinapaswa kutunza vizuri ili kisiweze kupata Maambukizi ila kwa wakati mwingine kitovu hicho kinaweza kupata Maambukizi kwa sababu zifuatazo.
2. Pengine kunakuwepo kwa Maambukizi kutoka kwa mama wakati wa kujifungua kwa sababu kuna wadudu ambao wanakaa kwenye nje ya plasenta pale mtoto akitolewa nje na kukata kitovu ili kutenganisha na plasenta wadudu wanaweza kuingia kwenye kitovu na kusababisha maambukizi. Wadudu hao wanaweza kutokana na kuwepo kwa kaswende hasa kwa wamama ambao hawakupima walipogundua kwa na mimba na pia Maambukizi kutokana na Magonjwa mbalimbali.
3. Chupa ya Mama kupasuka wakati wa uchungu na Mama akakaa mda mrefu bila kujifungua.
Kuna kipindi ambapo chupa ya Mama huwa unapaswa na Mama anakaa mda mrefu bila kujifungua kwa kawaida chupa ya Mama ikifungua Mama ukaa mda kidogo na baadae anajifungua ila hadipojifungua wadudu wengine wanaweza kuingia kwenye kitovu na baada ya mtoto kutoka nje ya tumbo la Mama na kitovu kukatwa ili kutenganisha na plasenta wadudu wanaweza kuwa kwenye kitovu na kuleta Maambukizi.
4. Watoa huduma kutumia vifaa vichafu wakati wa kukata kitovu.
Kuna wakati mwingine watoa huduma wanakuwa wazembe katika kutoa huduma kwa sababu wanatumia vifaa ambavyo siyo visafi na wakati mwingine vinakuwa na kutu hatimaye Maambukizi yanaweza kutokea kwenye kitovu.
5.Hasa hasa wale wakunga Jadi wa mitaani utakuta wanatumia wembe mmoja kwa watoto mbalimbali au pengine visu na wanavisafisha kwa njia za kawaida hatimaye wanasababisha Maambukizi kwenye kitovu, kwa hiyo akina Mama wanapaswa kujifungulia hospitalini ili kuepuka hali za kuwepo kwa Maambukizi.
6. Walezi au wazazi kutokitunza vizuri kitovu.
Kuna wakati mwingine wazazi au walezi wa mtoto wanakuwa wazembe katika kutunza kitovu cha mtoto kwa mara nyingine wanatumia mila zao wanazozijua ili kutunza kitovu hali ambayo Usababisha Maambukizi kwa mfano kuna makabila wanaosha kitovu kwa maji yaliyochanganywa naiti shamba hali ambayo Usababisha Maambukizi kwenye kitovu.
7.Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kuwatunza watoto wao vizuri na kuepuka madhara yatokanayo na Maambukizi kwenye kitovu kwa kuhakikisha kujua kubwa kitovu hakioshwi na dawa yoyote isiyotolewa hospitalini na kuacha tabia ya kuosha kitovu na miti shamba kwa sababu huwezi kujua kuna nini katika hayo matumizi ya miti shamba.
8 pia akina mama wanapaswa kujifungulia hospitalini hat kama ni mbali siku za kujifungua zikifika wasogee kwa ndugu aliye karibu kwa sababu kwa wakunga wa Jadi kuna shida ya ukosefu wa vifaa kwa hiyo tabia ya kutumia kifaa kimoja na kusafisha Usababisha kuenea kwa magonjwa sio tu Maambukizi kwenye kitovu tu.
9.Pia na wakunga mahospitali wanapaswa kuwa waangalifu katika matumizi ya vifaa ili kuweza kuepuka tatizo la kuwepo kwa Maambukizi kwenye kitovu kwa hiyo vifaa ambavyo vitatumika vinapaswa kuandaliwa vizuri kwa kuwepo kwa watu walio na ujuzi wa kusafisha vifaa kwa utaratibu maalum ili kuweza kuepuka Maambukizi.
10.Vili vile wazazi na walezi wapate elimu maalumu kuhusu namna ya kutunza kitovu cha mtoto na pia wajue wazi madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na kuwepo kwa uzembe wakati wa kutunza kitovu cha mtoto. Vile na wakunga Jadi wapewe vifaa vya kutosha wanapotoa huduma ili kuweza kuepuka madhara ya kuwepo kwa magonjwa maaambukizi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Kipimo cha Mlimba huweza kuonyesha mimba changa mapema sana. Pia ni rahisi kutumia na kinapatikana kwa bei nafuu. Je ungeoendavkujuwa ni muda gani kinatoa majibu sahihi?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia wanaotoa hedhi yenye mabonge, ni tatizo ambalo uwakumba wasichana hata wanawake wakati wa hedhi.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mimba iliyotunga nje na madhara yake kiafya
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea iwapo Kuna upungufu wa homoni ya progesterone.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba, ni Imani ambazo zimekuwepo kwenye jamii kuhusu wanawake wenye mimba.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo mwanamke hapaswi kufumbia macho.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi uhusiano uliopo kati ya Mama Mjamzito na kibofu cha mkojo.ni mwingiliano unaokuwepo ambao usababisha Mama kukojoa sana wakati wa ujauzito.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya uzito kwa mjamzito, hii ni hali ya kubadilika kwa uzito kwa Mama akiwa na Mimba
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zilijitokeza zinaweza kusababisha ugumba hasa kwa wanawake, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwa makini kwa Dalili hizi hasa kwa wadada, kama kuna uwezekano wa matibabu tibu mapema ili kuepuka tatizo la kuwa mgumba.
Soma Zaidi...