Huduma kwa mama mwenye kifafa cha mimba.
Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wajawazito wanaweza kuzipata wakiwa na Dalli au tayari wana kifafa cha mimba.
Huduma kwa wanawake wenye kifafa cha mimba.
1. Kwanza kabisa Mama anapaswa kuhakikisha anahudhuria mahudhurio ya mara kwa mara ili kupima kiwango cha presha na pia kuangalia kiwango cha protini kwenye mkojo na pia kuzingatia mda wa kujifungua na ajitahidi kujifungulia hospitalini ili kuweza kuwa na uhakika wa huduma wakati wa kujifungua, akijifungua mitaani anaweza kupatwa na matatizo ambayo wahudumu wa pale wanaweza kushindwa kuyafanyia kazi na kulingana na tatizo.
2. Pia Mama anapaswa kupata mda wa kutosha kupumzika, pia huduma zota anapaswa kuzipata akiwa kitandani kwa hiyo akikaribia kujifungua aepukane na kutembea huku na huko bila sababu ya msingi na pia anapaswa kufundishwa jinsi ya kulala kwenye kitandani ili kuhakikisha kubwa damu inatembelea kwenye mfuko wa uzazi kwa kiwango cha kutosha pia kuhakikisha kubwa na miguu kama imevimba inatoka na kuwa kwenye hali ya kawaida.
3. Vile vile mkojo wa Mama unapaswa kuangaliwa kila mara ili kuweza kutambua kama kiwango cha protini kwenye mkojo kimepungua au kinaendelea kuongezeka na kuweza kutoa huduma za msingi ili kupunguza kiwango cha protini kwenye mkojo.
4. Kwa mama mjamzito kiwango cha vimiminika vinavyoingia na kutoka vinapaswa kupimwa, ikionekana kwamba kiwango cha kimiminika kinachotoka ni kikubwa tunajua wazi figo linafanya kazi vizuri ila kama ni kidogo tunajua wazi kubwa kuna tatizo kwenye figo.
5. Kupima mara kwa mara kiasi cha presha kwa sababu ili kuweza kutambua kuwa kiwango kinaongezeka au kina pungua kupima mara nne kwa saa.
6. Kuendelea kuangalia tumbo mara kwa mara walau mara mbili kwa siku moja ili kuweza kuangalia kama kuna maumivu kwenye tumbo au kitu chochote kisicho cha kawaida.
7. Kuangalia mara kwa mara mapigo ya mtoto kama yapo sawa kwa sababu tatizo hili kama halijaangaliwa vizuri usababisha matatizo makubwa kwa mtoto
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 ai web app 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Huduma kwa wanaotoa damu yenye mabonge
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia wanaotoa hedhi yenye mabonge, ni tatizo ambalo uwakumba wasichana hata wanawake wakati wa hedhi.
Soma Zaidi...Dalili za kuvimba kwa ovari.
 Posti hii inazungumzia kuhusiana na kuvimba kwa ovari kunakosababishwa na maambukizo ya bakteria na kawaida huweza kusababishwa na magonjwa sugu katika Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke.
Soma Zaidi...Tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID
Posti hii inahusu zaidi tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID, tunaita tiba ya awali kwa sababu baada ya kupima na kugunduliwa kwamba una tatizo au changamoto ya PID ni vizuri kutumia tiba hiii baadae ndipo utumie dawa.
Soma Zaidi...Mabadiliko ya mzunguko wa damu kwa wajawazito.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya mzunguko wa damu kwa wajawazito, tunajua wazi kuwa wajawazito pindi ujauzito ukiingia tu, kila kitu kwenye mwili ubadilika vile vile na mzunguko wa damu ubadilika.
Soma Zaidi...Mimi ni mama ninaye nyonyesha toka nimejefunguwa sijawai kuziona siku zangu lakini nilipo choma sindano za yutiai nikaaza kutokwa na tamu kama siku tano na mwanangu ana mwaka moja je ninahatali ya kubeba mimba
Kunyonyesha ni moja katika njia za asili za kuzuia upatikanaji wa miba nyingine. Hata hivyo hii haimaanishi kuwa huwezi kupata mimba ukiwa unavyonyesha.
Soma Zaidi...Jinsi ya kuongeza nguvu za kiume
Post hii itakwenda kukuletea orodha ya vyakla vinavyoaminika kuongeza nguvu za kiume.
Soma Zaidi...