ZIJUE SABABU ZA MOYO KUTANUKA.


image


Posti hii inahusu zaidi sababu za moyo kutanuka, Kuna kipindi ambapo moyo utoka kwenye hali yake ya kawaida na kutanuka hali ambayo usababisha madhara kwa mwenye tatizo hilo, ila Kuna sababu ambazo usababisha moyo kutanuka kama tutakavyoona.


Zijue sababu za moyo kutanuka.

1. Kupanda kwa shinikizo la damu.

Kuna wakati ambapo shinikizo la damu upanda na hali hii usababisha moyo kusukuma damu kwa nguvu na kusababisha moyo kupanuka Ili kuruhusu damu iweze kufika kwenye sehemu mbalimbali za mwili.

 

2. Ugonjwa wa misuli ya moyo.

Kuna wakati mwingine kunakuwepo na ugonjwa wa misuli ya moyo au maambukizi kwenye misuli ya moyo hali hii ikitokea usababisha moyo kusukuma damu kwa nguvu na hivyo kusababisha kupanuka kwa moyo.

 

3. Uwepo wa maji maji ambayo yameuuzunguka moyo.

Kwa kawaida moyo unapaswa kuwa kwenye hali yake ya kawaida lakini Kuna wakati kunakuwepo na maji maji yanayouzunguka moyo ambayo usababisha kuleta maambukizi kwenye sehemu mbalimbali za moyo na hivyo kusababisha moyo kutanuka.

 

4. Upungufu wa damu mwilini.

Kumbuka kwamba damu ndiyo imebeba hewa ya oksijeni  kwa hiyo damu ikipungua usababisha na hewa ya oksijeni kupungua kwa hiyo moyo utumiwa nguvu nyingi Ili kuweza kusukuma damu kwenye sehemu mbalimbali za mwili Ili kukidhi kiwango cha hewa ya oksijeni iliyokosa kwenye mwili.

 

5. Matatizo ya tezi.

Kuna wakati mwingine tezi zinashindwa kutoa vichocheo vya kutosha Ili kuweza kukidhi mahitaji ya mwili hali ambayo usababisha mwili  kukosa virutubisho hivyo tukumbuke kwamba vichocheo hivyo upitia kwenye damu . Kwa hiyo hivyo vichocheo vikipungua mwilini usababisha moyo kusukuma damu kwa nguvu Ili kusafirisha vichocheo hivyo kwenye mwili hali inayosababisha moyo kupanuka.

 

6 kuwepo kwa madini mengi ya chumu.

Madini ya chuma yakikusanyika kwenye moyo usababisha moyo kukosa nafasi ya kutosha ya kuweza kusukuma damu ipasavyo kwa hiyo moyo utafuta nafasi ya kusukuma damu kwa nguvu kupitia kwenye mlundikano wa madini ya chuma na kwa sababu ya pressure kubwa ya moyo kusukuma damu hatimaye moyo kutanuka.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    2 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    3 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    5 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    6 Hadiythi za alif lela u lela    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Koo langu limekauka yaweza kuwa ni muadhirika?
kuwashwa na koo ni katika dalili za kuwa na maambukizi mwilini. Kuwa na maambukizi haimaanishi ni HIV ama UKIMWI laa hili ni neno pana. Hapa nitakujuza kwa ufupi kuhusu swali hilo la muulizaji kuwa anawashwa na koo. Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Bawasili
Posti hii inahusu zaidi juu ya ugonjwa wa Bawasili, ni ugonjwa unaotokea kwenye njia ya haja kubwa hali ambayo upelekea kuwepo kwa uvimbe au nyama ambazo uonekana hadi nje, kwa lugha ya kitaalamu ujulikana kama haemorrhoid au pokea. Soma Zaidi...

image Sababu za mwanamke kuumwa tumbo y chini ya kitovu.
Posti hii inahusu sababu za mwanamke kuumwa tumbo chini ya kitovu, ni tatizo ambalo limewapata wanawake wengi na pengine sababu ni vigumu kupata au pengine zinapatikana lakini kwa kuchelewa hali ambayo usababisha madhara mbalimbali kwenye mwili. Soma Zaidi...

image Huduma kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi
Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wagonjwa wanaoishi na maambukizi ya virus vya ukimwi wanaweza kupata, huduma hii utolewa hasa kwa wale ambao wamejitokeza kupima afya zao na kujua wazi hali zao na kwa wale wanaofatilia huduma hii wanaweza kuishi vizuri na kuwa na afya nzuri. Soma Zaidi...

image Njia za kuondokana na fangasi
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuweza kupambana na fangasi za ukeni ili kuweza kujiepusha na madhara mbalimbali kwenye maisha ambayo ni pamoja na ugumba na Maambukizi kwenye via vya uzazi. Soma Zaidi...

image Mbinu za kuzuia na kuepukana na maradhi ya uti wa mgongo
Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepukana na tatizo la ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo. Soma Zaidi...

image Dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa ,kwa kawaida Ugonjwa huu utokea kuanzia kwenye wiki ya pili mpaka mwaka mmoja na hapo Ugonjwa unakuwa bado haujaonesha Dalili na Dalili zikishaonekana ni vigumu kutibika. Soma Zaidi...

image je kukohoa kunaweza kuwa ni dalili ya minyoo?
Dalili za minyoo zipo nyingi kama kuumwa na tumbo, tumbo kujaa gesi, uchovu, kukosa hamu ya kula, kupata choo chenye uteute na kupunguwa uzito. je kukohoa kunaweza kuwa ni dalili ya minyoo? Soma Zaidi...

image Madhara ya kutotibu maambukizi chini ya kitovu
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu maambukizi chini ya kitovu ni madhara ambayo yanaweza kutokea kwa mgonjwa pale ambapo matibabu yanapokuwa hayatolewi kwa mgonjwa wa maumivu chini ya kitovu. Soma Zaidi...

image Namna ya kuzuia Ugonjwa wa kaswende
Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia Ugonjwa wa kaswende, tunajua wazi kuwa Ugonjwa huu unasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kufanya ngono zembe na njia nyingine kwa hiyo tunaweza kuzuia kusambaa na kuenea kwa ugonjwa huu kwa njia mbalimbali kama tutakavyoona hapo baadaye. Soma Zaidi...