Aina za kisukari
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu aina za kisukari
AINA ZA KISUKARI
1.Type 1 Diabetes; aina hii huotokea wakati mfumo wa kinga mwilini (immune system) unaposhambulia seli zinazozalisha insulin katika kingosho. Seli hizi zinaposhambuliwa mwili utashindwa kuzalisha insulin. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa aina hii ya kisukari husababishwa na virusi pamoja na kurithi kutoka kwa wazazi.
Aina hii ya kisukari pia huitwa insulin-dependent au juvenile diabees. Hii hutibiwa kwa kutumia dawa na mara nyingi huweza kuonekana kabla ya miaka 18. Dalili za aina hii ni za hatari sana na hutokea kwa ghafla. Miongoni mwazo ni kiu kikali, kuchoka sana na kupunguwa uzito.
2.Type 2 Diabetes; pia aina hii huitwa noninsulin-dependent diabetes na mara nyingi huwapata watu wenye umri wa kuanzia miaka 40 na wale watu ambao wana uzito wa kuzidi.
Katika aina hii ya kisukari mwili unazalisha insulin lakini seli zinashindwa kuitumia insulin inayozaliwa. Miongoni mwa dalili zake ni kukojoakojoa, kiu kikali, kutokuona kwa ufasaha, kuchelewa kupona kwa majeraha na maambukizi ya mara kwa mara.
3.Gestation Diabetes; hii huwatokea sana wajawazito mwishoni mwa mimba na hupotea baada ya mtoto kuzaliwa. Hii huweza kuongeza hatari wakati wa kijifungua na kama mama amerithi kisukari kutoka kwa wazazi hali inaweza kuwa mbaya zaid. Dalili zake ni sawa na zile za hizo aina mbili hapo juu,
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 web hosting 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Uzito kupita kiasi (Obesity): Hatari zake kiafya.
Uzito kupita kiasi, au unene uliokithiri (obesity), si suala la mwonekano wa nje pekee, bali ni changamoto kubwa ya kiafya inayoongeza hatari ya kupata magonjwa sugu ambayo yanaweza kupunguza umri wa kuishi. Hali hii hutokea wakati kiasi cha mafuta mwilini kinapozidi kiwango cha kawaida na kuanza kuathiri utendaji kazi wa viungo muhimu. Makala haya yanaelezea hatari za kiafya zinazohusiana na uzito kupita kiasi na umuhimu wa kuchukua hatua za haraka ili kulinda afya yako.
Soma Zaidi...SABABU ZINAZOPELEKEA KUJAA KWA MATE MDOMONI NA MATIBABU YAKE
Kutokwa na mate mengi mdomoni si ugojwa ni hali inayoweza kutokea kwa mtu yeyote. Mara nyingi hali hii haihitaji matibabu wa dawa, na huondoka yenyewe. Lakini hutokea baadhi ya nyakati ikawa mate yanatoka zaidi mdomoni. Je na wewe ni miongoni mwao? Makala
Soma Zaidi...Athari za kula vyakula vyenye sukari nyingi kila siku.
Katika ulimwengu wa sasa, sukari imekuwa kiungo kikuu katika vyakula vingi vilivyosindikwa, hali inayochangia kwa kiasi kikubwa magonjwa yasiyoambukiza. Makala haya yanachambua athari za muda mrefu za ulaji wa sukari nyingi, ikizingatia afya ya moyo, uzito wa mwili, na utendaji wa kimetaboliki, huku ikitoa mikakati ya kitaalamu ya kupunguza matumizi ya sukari kwa maisha marefu na yenye tija.
Soma Zaidi...Vyakula Muhimu kwa Mama Mjamzito
Ujauzito ni kipindi cha kipekee kinachohitaji uangalizi maalum wa lishe. Makala hii inaangazia vyakula muhimu ambavyo kila mama mjamzito anapaswa kuzingatia ili kuhakikisha afya yake na ukuaji bora wa mtoto aliyepo tumboni.
Soma Zaidi...