JE?WAJUA NJIA SAFI NA KANUNI ZA KUWEKA MWILI WAKO KWENYE AFYA NZURI?
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa usafi katika maisha ya mwanadamu au mwili wa binadamu.
Tukiangalia katika maisha yetu ya iipa siku tunaona kwamba watu hawaweki mazingira yao katika hali ya usafi.usafi utusaidia kuwa salama na kuondokana na vimelea vya magonjwa.pia ukioga kunakuondolea harufu mbaya unasababishwa na jasho linalotolewa mwilini kwa njia ya ngozi.vilevile,kuoga husaidia kuzibua vitundu vya jasho,ambavyo huziba kutokana na uchafu .Aidha ,kuoga kuoga huifanya ngozi kuonekana nyororo na dhaifu.
ZIFUATAZO NI KANUNI ZA AFYA AMBAZO ZINAWEKA MWILI KATIKA NZURI YA AFYA.
- LIshe bora,kutokana na apo mwanzo tulivyoeleza kuhusu afya ya mwili ni muhimu .lishe bora au chakula ni muhimu kwa afya zetu .pia lishe bora ni chakula chenye mchanganyiko wa virutubisho vyote muhimu ambavyo vina protini,vitamin,wanga na sukari,mafuta na madini.pia maji safi na salama ni muhimu kwa afya zetu ,protini hujenga na kukuza mwili .wanga na sukari utia mwili nguvu.mafuta uleta nguvu na joto mwilini.vitamini hupinda mwili ili usipatwe na magonjwa.madini husaidia kuimarisha mifumo na mifupa ya mwili.maji husaidia kumeng'enya chakula.pia maji husaidia kuondoa uchafu wa sumu mwilini na kurekebisha joto la mwili .hio ni mojawapo ya kanuni nzuri ya kuweka afya ya mwili .pia ukiweza kutumia hivyo vyakula utapata afya nzuri sana
- safi wa mazingira,kutoka na apo awali tulivyoona jinsi ya kuweka afya zetu vizuri. Usafi wa mazingira tunayoishi ni lazima yawe katika hali ya usafi.pia ni muhimu kufanya usafi wa mazingira ya nyumbani au mazingira yote yanayotuzunguka.pia kama kuna sehemu kuna mazingira machafu huvutia sana wadudu ambao ubeba vimelea vya magonjwa.vimelea hivyo huweza kusababisha magonjwa kama vile kuharisha ,kipindupindu,malaria na ugonjwa wa ngozi.inatubidi tuwe tunafanya usafi kila siku katika mazingira yetu ili tusiweze kupata magonjwa hayo.pia tukifanya hivyo tunakuwa tunalinda afya zetu .uchafu ni adui wa maendeleo.
- kutumia maji safi na salama,ili kuwa na afya bora tunatakiwa kutumia maji safi na salama.kabla ya kunywa maji hakikisha maji yamechemshwa na kuchujwa vizuri kwa kitambaa cheupe na kisafi .maji ya kunywa yachemshwe na yahifadhiwe vizuri kwenye vyombo visafi vyenye mifuniko.ni vizuri kuwa na chombo mahalumu cha kuchotea maji ya kunywa na kumiminina kwenye chombo cha kunywea maji .havitakiwi kutumia chombo hichohicho kuchotea maji na kunywa .hio ilikuwa ni kanuni jinsi gani tunaweza kuweka mwili wetu katika hali ya usafi na afya njema.
- kupumzika na kupata usingizi,watu wengi hawajui kama kupumzika na kupata usingizi kama ni njia mojawapo ya kuweka mwili katika hali ya afya.kupumzika niuhimu kwa afya zetu.watu inabidi watenge muda ili kupumzisha akili na kupata chakula bora.ili kuweka mwili katika hali ya afya .pia ata hivyo inatubidi usiku kulala na kupata usingizi kwa muda wa kutosha .usipolala kwa muda wa kutosha mwili hudhoofika na hatimaye kukosa nguvu. Pia ,unaweza kupumzika kwa kujibirudisha kwa kuangalia runinga au kusikiliza radio na kusoma vitabu au magazeti.unapopumzika ,unapata nguvu mpya ya kuendelea na kazi yako,kusoma au kucheza kwa ufanisi au kufanya kazi yako.kupumzika ni muhimu kwa akili ya usalama wako na afya yako .pia inashauri angalau kwa siku moja ulale masaa name (8).ili kuweka wako safi.
- KUfanya mazoezi ya viungo vya mwili,watu wengi kufanya mazoezi hawafamyi sababu wanaona ni huharibifu wa mda.lakini usichokijua mazoezi ni muhimu sana ili kuweza kuweka mwili sawa.pia inabidi mazoezi yafanyike mara kwa mara.ili kuimarisha afya ya mwili.mazoezi kama.kuruka kamba,kukumbuka,gwaride,.pia mazoezi haya hutusaidia kuwa na utayari wa kufanya kitu .ndo maana uaga tunashuhudia bahadhi ya shure wanakimbia mchaka mchaka.hii uaga inawataka kuwaweka tayari wa kujifunza kwa ufanisi darasani.na kuijenga misuli.pia mchezo huleta burudani ,kwa hiyo ni muhimu kucheza mara kwa mara ili kudumisha afya ya mwili.mtu aliyezoea kucheza hashambuliwi naagonjwa mara kwa mara.ata hivyo ni muhimu kudumisha usafi na kufuata kanuni za afya ili mwili huweze kuwa na afya bora.pia kanuni za afya kuonekana nadhifu na msafi wakati wote .kuongezeka kwa umri wa kuishi,kutoshambuliwa na maradhi ya mara kwa mara ,kuwa na uwezo mkubwa wa kufikiri na kutenda mambo mbalimbali kwa ufanisi,wepesi na umakini ,na kuokoa gharama ambazo zingetumika kwenye matibabu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 web hosting 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Kutokwa na jasho kupita kiasi wakati wa kulala: Chanzo chake.
kuamka katikati ya usiku ukajikuta nguo zako au mashuka yameloa jasho hadi unalazimika kubadilisha, licha ya kwamba chumba kina ubaridi wa kutosha? Hali hii kitaalamu inajulikana kama Night Sweats. Makala haya yanachambua vyanzo mbalimbali vinavyosababisha tatizo hili, kuanzia sababu za kawaida za kimazingira hadi viashiria vya matatizo ya kiafya yanayohitaji ushauri wa daktari.
Soma Zaidi...Dalili za Mimba Baada ya Ovulation
Kipindi cha baada ya yai kupevuka (ovulation) na kabla ya siku zako za hedhi kutarajiwa (drip-wait period) ni kipindi cha kusisimua kwa mwanamke anayetafuta mtoto. Makala hii inaelezea dalili za mapema ambazo mwili unaweza kuzionyesha mara baada ya yai kurutubishwa na kupandikizwa kwenye mji wa mimba, yakikusaidia kuelewa mabadiliko ya kibaolojia yanayoendelea.
Soma Zaidi...Njia za kusambaa kwa ugonjwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine
Posti hii inahusu zaidi jinsi magonjwa yanavyosambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
Soma Zaidi...Jinsi ya kutoa huduma ya kwanz akwa liyeshambuliwa na pumu
Hii ni huduma ya kwanza kwa aliyeshambuliwa na pumu katika mazingira ambayo ni mbali na kituo cha afya, na hakuna dawa.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.
Soma Zaidi...Dalilili za kidole tumbo (appendicitis)
Posti hii inazungumzia kuhusiana na ugonjwa wa Kidole ambao kitaalamu hujulikana Kama Appendicitis. Kidole tumbo husababisha maumivu kwenye tumbo la chini la kulia. Hata hivyo, kwa watu wengi, maumivu huanza karibu na kitovu na kisha kusonga. Kadiri uvi
Soma Zaidi...