Vyakula na ugonjwa wa kisukari
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya vyakula vimpasavyo mgonjwa wa kisukari
VYAKULA NA UGONJWA WA KISUKARI
Chakula; mgonjwa wa isukari anatakiwa ale chakula kisicho na mafuta mengi, ckisicho na chumvi wala sukari nyingi. Kuala matunda na mboga za majani. Hakikisha unakula katika muda maalumu siku zote pia angalau upate chakula mara tatu kwa siku kula chakula kisicho kobolewa. Pia hakikisha unakunywa maji mengi zaidi kwa siku Mazoezi; hakikisha unafanya mazoezi si chini ya mara tatu kwa wiki.Hii huenda ikasaidia kupunguza usito na kuthibiti kiasi cha sukari ndani ya mwili wako. Pia kufanya mazoezi ni muhimu kwa afya yako kwa ujumla. Mazoezi yanaweza kupunguza mlundikano wa mafuta kwenye ngozi na mishipa yta damu. Hali hii itakusaidia kupunguza uwezekano wa kuapata strock na shambulio la moyo.Dhibiti uzito wako; hakikisha kuwa hauna uzito usio wa kawaida. Yaani hakikisha kuwa unapunguza uzito kama uzito wako ni mkubwa. Pata ushauri wa daktari kuhusu uzito wako kama unakufaa au umezidi kulingana na afya yako. Zipo njia nyingi za kupunguza uzito kupitia vyakula, mazoezi na nyinginezo. Muone daktari au pata ushauri kwa walio na ujuzi wa njia salama ya kupunguza uzito.Tumia dawa; kama kisukari kimeshindikana kuthibitiwa kwa nyia hizo hapo juu anza kutumia dawa. Zipo dawa maalumu kwa wagonjwa wa kisukari. Pia inashauriwa kuwa mtu aanze kutumia dawa za kumeza kabla ya zile za sindano. Muone daktari atakupatia dawa hizo kulingana na afya yako. Watu wengi wanakuwa wavivu wa kunywa dawa lakini kwa baadhi ya magonjwa uvivu huu ni hatari zaidi kwa afya zao.
?
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia, sababu zake na dalili zzake
Hapa utajifunza sababu za kupatwa na maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia
Soma Zaidi...Lishe sahihi kwa wazee: Nini cha kuzingatia?
Kadiri tunavyozidi kuzeeka, mwili wetu hubadilika. Hitaji la nishati hupungua, lakini hitaji la virutubisho hubaki juu—au hata kuongezeka. Lishe sahihi katika uzee sio tu kwa ajili ya "kushiba," bali ni kinga dhidi ya magonjwa, njia ya kudumisha nguvu za misuli, na ufunguo wa kuishi kwa heshima na afya njema. Makala haya yanakupa mwongozo wa mambo muhimu ya kuzingatia katika kula kwa afya katika umri wa utu uzima.
Soma Zaidi...Vyakula salama kwa mwenye kisukari
Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya vyakula salama kwa mwenye kisukari
Soma Zaidi...Faida za kula fyulisi/peach
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula fyulisi/ peach
Soma Zaidi...Vyakula vya vitamini na faida zake
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula vya vitamini na faida zake
Soma Zaidi...