picha

Maumivu ya tumbo baada ya kula

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo baada ya kula

MAUMIVU YA TUMBO BAADA YA KULA

 

Baada ya kula ni wakatiwa wa kupumzika, lakini sivyo kwa baadhi ya watu. Wao anapomaliza tu, anangojewa na maumivu ya tumbo. Je unajuwa sababu?, je na wewe unapatwa na maumivu ya tumbo baada ya kumaliza kula? Makala hii ni kwa ajilli yako.

 

Kwa ufupi maumivu haya yanaweza kusababishwa na mchafuko wa tumbo. Tunapozungumzia mchafuko wa tumbo tunazungumzia mmeng’enypo wa chakula unakuwa na hali ambayo si ya kawaida.

 

Dalili za mchafuko wa tumbo ni kama:-A.KichefuchefuB.KuharaC.Kiungulia ama kucheuaD.Kujaa tumbo na kutoa hewa kwa mdomoni. Kwa kucheuaE.Maumivu ya tumboF.Kushiba kusikkokuwa kwa kawaidaG.Lushiba kwa harakaH.Maumivu ya sehemu ya juu ya tumboI.Kuhisi kuunguwa chini ya tumboJ.Kuhisi kuunguwa kifuani na maumivu ya kifuaK.Kutapika

 

Nini husababisha maumivu ya tumbo baada ya kula?Kwa hakika kuna sababi nyingi ambazo zinaweza kupelekea maumivu ya tumbo baada ya kula. Sio hivyo tu pia tumbo linapatwa na machafuko makubwa kwa mfano kutapika, kichefuchefu, kuharisha na mengineyo. Sasa ni zipi sababi hizo zinazoletwa maumivu ya tumbo baada ya kula?

 

1.Aleji ya chakula.2.kuna baadhi ya vyakula huwa vina aleji, hii hutokea pale mwili mwili unapokidhania chakula kuwa hakipo salama, na kuanza kukishambulia ili kukitoa. Hali hii hupelekea maumivu ya tumbo kama matokeo ya mpambano. Baadhi ya vyakula vyenye aleji ni kama:-1.Maziwa2.Maharagwe ya soya3.Baadhi ya samaki4.Vyakula jamii ya karanga na korosho5.Mayai6.Ngano

 

3.kama mfumo wa kumeng’enya chakula umeshindwa kukivumilia aina ya chakula ulichokula. Yaani mfumo wa chakula unashindwa kukimeng’enya kabisa ama kinameng’enywa lakini si kwa ufasaha. Kwa mfano baadhi ya vyakula vilivyotengenezwa na maziwa kwa baadhi ya watu inakuwa ni tatizo na hupelekea mvurugiko wa tumbo.

 

4.kama ukuta wa utumbo mdogo umeathiriwa na protini ya gluten, protini inayopatikamna kwenye nafaka kama ngano na shayiri. Hali hii hutambulika kama celiac disease.

 

5.Kama una tatizo la kupanda kwa tinikali za tumboni kuja juumkwenye koo sehemu inayojulikana kama esophagus. Tindikali hii inaweza kuathiri kuta za kiungo hiki na kusababisha machafuko ya tumbo. Hali hii kitaalamu hutambulika kama Gastroesophageal disease (GERD)

 

6.kama una matatizo kwenye utumbo mkubwa kwa kitaalamu huitwa irritable bowel syndrome. Hali hiii inaweza kuonyesha dalili kama:-A. Maumivu ya tumboB.Kujaa kwa tumboC.KuharishaD.Kukosa chooE.Kujaa gesi

 

7.Kuvimba kwa baadhi ya sehemu kwenye mfumo wa kumeng’enya chakula. Mgonjwa anaweza kuona dalili kama maumivu ya tumbo, kuhara, damu kwenye kinyesi n.k

 

8.Kama una vidonda vya tumbo. Vidond vya tumbo vinaweza kusababisha maumivu ya tumbo baada ya kumaliza kula.

 

9.Kukosa choo. Hali hii hutokea pale chakula kinapotembea kidogokidogo katika njia ya mmeng’enyo wa chakula.

 

Namna ya kujikinga na maumivu ya tumbo baada ya kula.1.Kama kuna chakula unakumbuka kilikuletea matatizo kama haya hebu kiepuke2.Kula chakula chenye kambakmba kwa wingi na matunda3.Kunywa maji mengi4.Punguza unywaji wa pombe5.Punguza matumizi ya caffein (majani ya chai kwa wingi)6.Punguza misongo ya mawazo

 

?

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021/11/11/Thursday - 12:03:01 am Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 4025

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Naombakujua kujua Kama huu uyoga unasaidia kansa Kama kwawazee

Mpaka sasa hakuna dawa ya kuponyesha saratani wala kinga ya saratani. Hata hivyo vipo vyakula ambavyo vinakadiriwa kuwa hupunguza hatari ya kuweza kupata saratani. Je unadhani uyoga ni moja ya vyakula hivyo?

Soma Zaidi...
Vitamini C ni nini, na vipo kwenye nini?

Hapa utajifunza maana ya Vitamini C, mwaka vilipogunduliwa na aliyegundua vitamini C

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula kitunguu thaumu

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kitunguu thaumu

Soma Zaidi...
Faida za kunywa maziwa

Somo hili linakwenda kukuletea faida za kunywa maziwa kiafya

Soma Zaidi...
Kazi za vitamini B mwilini Na upungufu wa vitamini B mwilini

vitamini B vipo katika makundi mengi kma aB1, B2, B3, B5, B6, B7 na B12. Makala hii itakwenda kukutajia kazi kuu za Vitamini B katika miili yetu

Soma Zaidi...
Faida za kula Palachichi

Palachichi lina virutubisho vingi na vitamini, kula palachichi uiokoe afya yako

Soma Zaidi...
Faida za kula Tangawizi

tangawizi ni katika viungio vya mboga vyenye faida, pia ni kinywaji, zijuwe leo faida za tangawizi

Soma Zaidi...
Madhara ya upungufu wa protini mwilini

Madhara ya upungufu wa protini ni mengi kiafya. Miongoni mwa madhara hayo ni..

Soma Zaidi...
Faida za kula apple (tufaha)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula apple/tufaha

Soma Zaidi...