Utekwaji wa Misri na Gavana Muawiya

Utekwaji wa Misri na Gavana Muawiya

Muawiyah Ateka Jimbo la Misri



Khalifa Ali alimteua Qais bin Sad awe gavana wa Misri. Qais alichukua ahadi ya utii kwa niaba ya watu wa Misri, lakini watu wa jimbo la Khartaban hawakutoa ahadi ya utii kwa Khalifa Ali na Qais aliwaacha kwa kuwa kulikuwa na amani.



Hali hii ya kuwaacha watu wa Khartaban iliwafanya baadhi ya watu wamuone Qais sio mtiifu kwa Khalifa. Khalifa alikusudia kumjaribu Qais kwa kumuamuru awapige vita watu wa Khartaban. Qais hakuona sababu ya kupigana na watu wa Kharaban hivyo akaondolewa kwenye ugavana na nafasi yake akateuliwa Muhammad bin Abubakar.


Muhammad alikuwa kijana hivyo aliwalazimisha watu wa Khartaban wakubali Ukhalifa wa Ali. Watu wa Khartaban hawakukubali na walisubiri hadi vita vya Siffin vilipomalizika waliamua kujilinda dhidi ya majeshi ya gavana Muhammad bin Abubakar na mapigano yakazuka. Majeshi ya gavana yakashindwa mara mbili. Khalifa aliamua kumbadilisha Muhammad na kumtuma Ushtar kuwa gavana wa Misri.


Lakini Ushtar alikufa alipofika mpakani mwa Misr hivyo Khalifa alimtaka Muhammad aendelee kushikilia ugavana wa Misri akamtumia askari 2,000 ambao aliwapata kwa taabu. Lakini kabla askari wa Khalifa hawajafika Muawiya alimtuma Amri bin al As na jeshi la kutosha, likayashinda majeshi ya gavana na yeye mwenyewe kuuliwa. Kwa ushindi huu Misri ikawa chini ya Muawiyah na Amr bin al As akawa gavana wa Muawiyah Misri. Hii ilikuwa katika mwaka wa 38 A.H.





                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 804

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Sababu ya uislamu kuwa ndiyo dini sahihi pekee

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kuhifadhiwa kwa Quran

Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga

Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.

Soma Zaidi...
vita vya ahzab, sababu ya kutokea vita hivi na mafunzo tunayoyapata

Vita vya Ahzab- Maquraish waliungana na mayahudi, wanafiki na makabila mengine ya waarabu baada ya kuona kuwa wao peke yao hawawezi kuufuta Uislamu.

Soma Zaidi...
Kulingania watu wake na Miujiza Aliyoonyesha Nabii Isa(a.s)

Mwenyezi Mungu pekee ndiye aliyewawezesha Mitume na Manabii kufanya miujiza.

Soma Zaidi...
Historia ya kujengwa kwa Alkabah (Maka)

Kama tulivyoona katika maisha ya Mtume Ibrahim(a.

Soma Zaidi...
Kulingania Uislamu kwa Jamii Nzima

Baada ya miaka mitatu ya Utume, Muhammad(s.

Soma Zaidi...