Tamko la suluhu baada ya vita vya Siffin

Tamko la suluhu baada ya vita vya Siffin

Tamko la Wapatanishi



Baada ya mazungumzo marefu wapatanishi walikubaliana kuwa wote wawili Ali na Muawiyah hawafai kugombea nafasi ya ukhalifa. Amr bin al- As alimtegea Abu Mussa aanze yeye kusema msikitini juu ya maazimio yao. Abu Muusa akasema; โ€œEnyi watu tumelizingatia vyema suala linalotukabili. Hatukuona njia nyingine ya kuleta amani miongoni mwa watu ila kuwaondoa wote katika nafasi ya kugombea Ukhalifa. Baada ya hivi mchague Khalifa anayefaa. Hii ndio hukumu yangu.


Alipopanda jukwaani Amr bin al As alibadili maneno na kusema maneno wasiyokubaliana na mwenziwe kwa kusema; โ€œMmesikia hukumu ya Abu Mussa. Amemuondoa mtu wake nami pia ninamuondoa. Lakini kwa chifu wangu Muawiyah, yeye ninamthibitisha, ni mrithi wa Uthman, mlipiza wa damu yake, ni bora kuliko wote kwa kuchukua nafasi yake.


Wajumbe wote walichanganyikiwa kwa kauli hii na kukawa hakuna maelewano. Nusra Amr bin al-As auliwe na askari wa Ali. Uamuzi huu haukufuata Qurโ€™an hivyo haukukubalika. Khawarij walijikusanya na kuanza uasi. Walihama Harorah na kwenda Nahruwan. Katika eneo hili waliuwa watu na kufanya ukatili. Khalifa Ali alizungumza na Khawarij hawa ili waache vitendo vyao na imani yao potofu.


Lakini hawakukubali, kwa hali hii mapigano yakawa lazima, hata hivyo walishindwa vibaya. Baada ya hapa Khalifa Ali aliamuru jeshi lake liende Syria kupambana na Amir Muawiya kwa sababu suluhu haikuwa katika Qurโ€™an. Lakini kabla ya kwenda Syria Khalifa Ali alipiga kambi mahali paitwapo Nakhila karibu na mji wa Kufa. Askari wake waliomba kwenda makwao na akawaruhusu, wengi hawakurudi na safari ikavunjika. Alijaribu mara mbili kukusanya askari kwenda Syria bila mafanikio na kutokana na hali hii suala zima la kupigana tena na Muawiya akaliacha.





                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 824

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰2 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰3 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰5 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ayyuub(a.s)

Kutokana na kisha hiki cha Nabii Ayyuub(a.

Soma Zaidi...
Mtume Muhammad s.a. w akutana na Bahira

Sura na historia ya Mtume Muhammad s.a. w sehemu ya 11

Soma Zaidi...
Kusingiziwa Nabii Sulaiman Uchawi

Pamoja na Ucha-Mungu aliokuwa nao Nabii Sulaiman watu hawakuacha kumsingizia mambo machafu.

Soma Zaidi...
Kuandaliwa kwa Muhammad kabla ya kupewa utume

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Uendeshaji wa dola ya uislamu madinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...