image

Kulingania watu wake na Miujiza Aliyoonyesha Nabii Isa(a.s)

Mwenyezi Mungu pekee ndiye aliyewawezesha Mitume na Manabii kufanya miujiza.

Kulingania watu wake na Miujiza Aliyoonyesha Nabii Isa(a.s)

Kulingania watu wake na Miujiza Aliyoonyesha Nabii Isa(a.s)


Mwenyezi Mungu pekee ndiye aliyewawezesha Mitume na Manabii kufanya miujiza. Allah(s.w) aliwapa mitume miujiza ili kuwa dalili ya kuwathibitishia watu kuwa yeye ndiye aliyewatuma. Hakuna Mtume au Nabii aliyedai kufanya miujiza kwa uwezo wake mwenyewe. Na hivi ndivyo Nabii Isa alivyowaambia wana wa Israili.



.........Nimekujieni na hoja kutoka kwa Mola wenu, ya kwamba nakuumbieni, katika udongo, kama sura ya ndege, kisha nampuliza, mara anakuwa ndege kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na ninawaponesha vipofu na wenye mabalanga, na ninawafufua waliokufa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu na nitakuambieni mtakavyo vila na mtakavyo weka akiba katika nyumba zenu. Bila shaka katika haya imo hoja (ya kuonesha kuwepo Mwenyezi Mungu) kwenu ikiwa ni watu wa kuamini(3:49)

Ni dhahiri kuwa miujiza yote aliyoifanya Nabii Isa(a.s), aliifanya kwa lengo la kuwathibitishia watu kuwa yeye ametumwa na Mwenyezi Mungu. Katika Biblia, Yesu alibainisha hili wazi kabla hajafanya muujiza wa kumfufua Lazaro:



Yesu akainua macho yake juu, akasema: Baba nakushukuru kwa kuwa umenisikia. Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia siku zote; lakini ni kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kusadiki kuwa ndiwe uliyenituma. Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje. Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake umefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake (Yohana 11:41-44)

Kwa kuzingatia maandiko haya, utabaini kuwa hawasemi kweli wale wanaodai kuwa Yesu ni Mungu eti kwasababu alifanya miujiza ya kufufua wafu.



Wito wa Nabii Isa(a.s) kwa Wanafunzi Wake


Nabii Isa(a.s) alipoona ukaidi wao umeshitadi, akatoa wito maalum kwa wanafunzi wake ili wajitokeze wale watakaokuwa tayari kuwa naye bega kwa bega kupambana na madhalimu na kuufikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu kwa wengine. Hivyo, akawauliza:



Lakini Isa alipoona ukaidi wao, alisema: Nani watakuwa wasaidizi wangu katika kumtangaza Mwenyezi Mungu (mmoja)? Wanafunzi wakasema: “Sisi ni wasaidizi wa Mwenyezi Mungu. Tumemwamini Mwenyezi Mungu na ushuhudie kwamba sisi tumejisalimisha. Mola wetu! Tumeyaamini uliyoyateremsha na tumemfuata Mtume, basi tuandike pamoja na washuhudiao (3:52-53)



Baada ya hapo, wanafunzi wa Nabii Isa (a.s) wakamtaka awaombee chakula maalumu kutoka kwa Allah(s.w), wakasema:

Ewe Isa Mwana wa Maryam! Je Mola wako anaweza kututeremshia chakula kutoka mbinguni? Akasema(Nabii Isa), “Mcheni Mwenyezi Mungu kama kweli ninyi ni wenye kuamini kweli(5:112) Wakasema: “Tunataka kula katika hicho, na ili nyoyo zetu zitulie na tuwe miongoni mwa wanaoshuhudia(muujiza huo)(5:113) Akasema Isa bin Maryamu: “Ewe Mwenyezi Mungu, Mola wetu! Tuteremshie chakula kutoka mbinguni ili kiwe Sikukuu kwa ajili ya wa mwanzo wetu, na wa mwisho wetu, na kiwe Ishara itokayo kwako, basi turuzuku, kwani wewe ndiye mmbora wa wanaoruzuku(5:114)



Mwenyezi Mungu akasema: “Bila shaka Mimi nitakiteremsha juu yenu, lakini miongoni mwenu atakayekataa baada ya haya, basi Mimi nitamuadhibu adhabu ambayo sijamwadhibu yoyote katika walimwengu(5:115)



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1229


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

NI IPI FAMILIA YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) NA NI IPI NASABA YAKE, UKOO WAKE NA KABILA LAKE
FAMILIA YA MTUME (S. Soma Zaidi...

Adam na Hawah Kushushwa Ardhini
Soma Zaidi...

Watu wa Mji Waliomuua Muislamu kwa Kuwa Amewasadikisha Wajumbe wa Allah(s.w)
Katika Suratul Yassin Allah(s. Soma Zaidi...

Mtume kumuoa bi khadija
Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 15. Hapa utajifunza kuhusu chimbuko la ndoa ya Mtume s.a.w na bi Khadija. Soma Zaidi...

Malezi ya mtume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kisa cha Israa na Miraji na kufaradhishwa swala tano
Safari ya Mi'rajKatika mwaka wa 12 B. Soma Zaidi...

Uteuzi wa Uthman bin Al-'Afan khalifa wa Tatu baada ya Mtume
Soma Zaidi...

Je, Nabii Isa(a.s) ni Mtoto wa Mungu?
Mwenyezi Mungu si kiumbe. Soma Zaidi...

Mambo ya Msingi Aliyofanya Mtume(s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu Madinah.
Mambo ya Msingi Aliyofanya Mtume(s. Soma Zaidi...

Upinzani Dhidi ya Dola ya Kiislamu Wakati wa Makhalifa
Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Sulaiman(a.s)
Kutokana na histoira ya Nabii Sulaiman (a. Soma Zaidi...

Vipengele vya mkataba wa Hudaibiya na faida zake katika Ukombozi (ufunguzi) wa mji wa Makkah
Soma Zaidi...