image

Hali za bara arab zama za jahiliya karne ya 6 kabla ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad

7.

Hali za bara arab zama za jahiliya karne ya 6 kabla ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad

Hali ya Bra arab zama za jahiliya

7.1 Hali ya Bara Arab zama za Jahiliyyah.
Jiografia ya Bara Arab.
- Bara Arabu imezungukwa na bahari katika tatu, Magharibi kuna bahari ya Shamu,
Mashariki kuna Ghuba ya Uajemi na Oman, Kusini kuna bahari ya Uarabuni na
Kaskazini ni Jangwa la Syria.



- Bara Arabu liko kati kati ya mabara matatu; Asia, Ulaya na Afrika.
- Saudi Arabia ndio nchi kubwa kuliko zote Bara Arabu ambamo kuna miji mitakatifu
ya Makkah na Madinah.



?Hali ya Maadili na ushirikina katika jamii wakati wa kuzaliwa Mtume (s.a.w).
- Wakati anazaliwa Mtume mwaka 570 A.D (karne ya 6 A.D) dunia nzima ilikuwa
katika giza totoro la ujahili.



- Maisha ya jamii yalikuwa yanaendeshwa kibabe na kibinafsi kwa kufuata matashi
ya nafsi zao.



- Ubabe, ukandamizaji, unyonyaji, uporaji na dhuluma katika maisha yalionekana
kama matendo ya kishujaa na kujivunia.



- Walizama katika ushirikina kiasi cha watu kuweza kutembea na miungu mifukoni
mwao.


- Hali hii ya giza totoro ilienea pia nchi na mabara mbali mbali ulimwenguni kote.



- Dini kubwa zilizokuwepo muda huo zilikuwa ni Uyahudi na Ukristo lakini
hazikuweza kumkomboa mwanaadamu kwa lolote hata kidogo.



- Hapakuwa na serikali, kila kabila lilikuwa na kiongozi na taratibu zake katika
kuendeshea maisha.



- Unyanyasaji wa wanawake kila nyanja, mauwaji ya watoto wa kike wakiwa hai
ilikuwa ni desturi ya kawaida katika maisha ya jamii ya Waarabu.



Mji wa Makkah na Kabila la Kiqureish.
- Mji wa Makkah ni mji mkongwe wa kihistoria ulioanzishwa na Nabii Ibrahiim miaka mingi iliyopita.



- Nabii Ibrahim (a.s) na mwanae Nabii Ismail (a.s) ndio walioinua kuta za nyumba tukufu ya Ka’abah kwa amri ya Allah (s.w).
Rejea Qur’an (2:127).



- Ka’abah ni nyumba ya mwanzo na pekee ulimwenguni iliyowekwa kwa ya kuhiji wanaadamu wote ulimwenguni.
Rejea Qur’an (22:27), (3:96) na (22:29).




- Kutokana na jangwa na ukame wa mji huu, Allah (s.w) alijaalia chem.-chem ya maji ya zamzam kutokana dua ya Nabii Ibrahim (a.s).
Rejea Qur’an (14:37).



- Mji huu ulipata utukufu kutokana na uwepo wa nyumba tukufu ya Ka’aba ambapo kabila la Qureish ndio walikuwa walinzi wa nyumba hiyo.
Rejea Qur’an (106:1-4).



- Ni mji alikozaliwa Mtume Muhammad (s.a.w) mwaka 570 A.D katika kabila la Kiqureish mwaka wa ndovu.
Rejea Qur’an (105:1-5).



- Kabila la Kiqureish liliheshimika kuliko makabila mengine kwa huduma walizokuwa wakitoa kwa watu wanaohiji, misafara ya biashara na kule kuitumikia nyumba hiyo.



- Kabila la Qureish ni miongoni mwa makabila ya waarabu yaliyojishughulisha sana na biashara mbali mbali ndani na nje ya Makkah kwa muda mrefu.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 364


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Adam(a.s) na Mkewe Katika Pepo
Adam(a. Soma Zaidi...

Kukomeshwa kwa Riddah na Chokochoko Nyingine katika dola ya kiislamu
Soma Zaidi...

Mtume Muhammad alelewa na mama yake mzazi akiwa na umri wa miaka 4.
Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 8. Hapa utajifunza malezi ya Mtume kutokakwa Halimavkuja kwa mama yake. Soma Zaidi...

Chanzo cha vita vya Ngamia Vita Kati ya Bibi Aisha na Khalifa Ali
Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na maandalizi haya ya ki ilhamu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Chokochoko na Upinzani wakati wa khalifa uthman khalifa wa Tatu
KUPOROMOKA KWA DOLA YA KIISLAMU ALIYOICHA MTUME(S. Soma Zaidi...

Khalid Ibn al walid katika vita vya Muta
Yiomyokea khalid Ibn al walid katika vita vya Muta Soma Zaidi...

Zakaria(a.s) Akabidhiwa Ulezi wa Maryam
Baada ya kupigwa kura juu ya nani awe mlezi wa Maryam, Nabii Zakaria akachaguliwa kuwa mlezi wa Maryam. Soma Zaidi...

MTUME MUHAMMAD (S.A.W)ANAKUTANA NA BAHIRA (MTAWA WA KIYAHUDI)
KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara. Soma Zaidi...

Kuanzishwa kwa vitenge vya ulinza na Usalama, na usalama wa taifa
Soma Zaidi...

Nasaba ya Mtume Muhammad S.A.W na familia yake.
Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 1 Soma Zaidi...

Imam Nasai na kitabu cha Sunan
Soma Zaidi...