Hali za bara arab zama za jahiliya karne ya 6 kabla ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad

7.

Hali za bara arab zama za jahiliya karne ya 6 kabla ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad

Hali ya Bra arab zama za jahiliya

7.1 Hali ya Bara Arab zama za Jahiliyyah.
Jiografia ya Bara Arab.
- Bara Arabu imezungukwa na bahari katika tatu, Magharibi kuna bahari ya Shamu,
Mashariki kuna Ghuba ya Uajemi na Oman, Kusini kuna bahari ya Uarabuni na
Kaskazini ni Jangwa la Syria.



- Bara Arabu liko kati kati ya mabara matatu; Asia, Ulaya na Afrika.
- Saudi Arabia ndio nchi kubwa kuliko zote Bara Arabu ambamo kuna miji mitakatifu
ya Makkah na Madinah.



?Hali ya Maadili na ushirikina katika jamii wakati wa kuzaliwa Mtume (s.a.w).
- Wakati anazaliwa Mtume mwaka 570 A.D (karne ya 6 A.D) dunia nzima ilikuwa
katika giza totoro la ujahili.



- Maisha ya jamii yalikuwa yanaendeshwa kibabe na kibinafsi kwa kufuata matashi
ya nafsi zao.



- Ubabe, ukandamizaji, unyonyaji, uporaji na dhuluma katika maisha yalionekana
kama matendo ya kishujaa na kujivunia.



- Walizama katika ushirikina kiasi cha watu kuweza kutembea na miungu mifukoni
mwao.


- Hali hii ya giza totoro ilienea pia nchi na mabara mbali mbali ulimwenguni kote.



- Dini kubwa zilizokuwepo muda huo zilikuwa ni Uyahudi na Ukristo lakini
hazikuweza kumkomboa mwanaadamu kwa lolote hata kidogo.



- Hapakuwa na serikali, kila kabila lilikuwa na kiongozi na taratibu zake katika
kuendeshea maisha.



- Unyanyasaji wa wanawake kila nyanja, mauwaji ya watoto wa kike wakiwa hai
ilikuwa ni desturi ya kawaida katika maisha ya jamii ya Waarabu.



Mji wa Makkah na Kabila la Kiqureish.
- Mji wa Makkah ni mji mkongwe wa kihistoria ulioanzishwa na Nabii Ibrahiim miaka mingi iliyopita.



- Nabii Ibrahim (a.s) na mwanae Nabii Ismail (a.s) ndio walioinua kuta za nyumba tukufu ya Ka’abah kwa amri ya Allah (s.w).
Rejea Qur’an (2:127).



- Ka’abah ni nyumba ya mwanzo na pekee ulimwenguni iliyowekwa kwa ya kuhiji wanaadamu wote ulimwenguni.
Rejea Qur’an (22:27), (3:96) na (22:29).




- Kutokana na jangwa na ukame wa mji huu, Allah (s.w) alijaalia chem.-chem ya maji ya zamzam kutokana dua ya Nabii Ibrahim (a.s).
Rejea Qur’an (14:37).



- Mji huu ulipata utukufu kutokana na uwepo wa nyumba tukufu ya Ka’aba ambapo kabila la Qureish ndio walikuwa walinzi wa nyumba hiyo.
Rejea Qur’an (106:1-4).



- Ni mji alikozaliwa Mtume Muhammad (s.a.w) mwaka 570 A.D katika kabila la Kiqureish mwaka wa ndovu.
Rejea Qur’an (105:1-5).



- Kabila la Kiqureish liliheshimika kuliko makabila mengine kwa huduma walizokuwa wakitoa kwa watu wanaohiji, misafara ya biashara na kule kuitumikia nyumba hiyo.



- Kabila la Qureish ni miongoni mwa makabila ya waarabu yaliyojishughulisha sana na biashara mbali mbali ndani na nje ya Makkah kwa muda mrefu.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1385

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 web hosting    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Uendeshaji wa dola ya uislamu madinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Msimamo wa Nabii Nuhu(a.s) Dhidi ya Makafiri

Pamoja na upinzani mkali alioupata kutoka kwa viongozi wa makafiri, Nabii Nuhu(a.

Soma Zaidi...
Malezi ya mtume

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ayyuub(a.s)

Kutokana na kisha hiki cha Nabii Ayyuub(a.

Soma Zaidi...
Maadui wakubwa wa dola ya uislamu madinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Vitimbi vya Makafiri Dhidi ya Nabii Salih(a.s) na Waumini na kuangamizwa kwao

Makafiri wa Kithamud hawakuishia tu kwenye kuukataa ujumbe wa Nabii Salih(a.

Soma Zaidi...