Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga
Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.
Maana.
Maana ya funga kisheria ni kujizuia na vyenye kufunguza toka kuchomoza kwa alfajiri mpaka kuzama kwa jua pamoja na kuwa na niya ya kufanya ibada kwa ajili ya Allah. Fadhila za funga
Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga. Kwa hakika hiyo funga ni yangu, na mimi ndiye ninayeilipa ( thawabu) na funga ni ngome. Basi atakapfunga mmoja wenu asizungumze maneno ya upuuzi, wala asifanye mambo machafu na ya kijinga. Basi ikitikea mtu amemtukana au kumpiga yeye (asilipize) bali amwambie “nini mimefunga”. Na akasema Mtume (s.a.w) “na ninaapa kwa yule ambaye nafsi ya Muhammad ipo kwenye mkono wak: hakika harufu ya mdomo wa mwenye kufunga inapendeza zaidi mbele ya Allah siku ya kiyama kuliko harufu ya mafuta ya misk. Na ana mwenye kufunga furaha mbili: atakapofutari na atakapokutana na Mo;a wake atafurahia funga yake. (Bukhari na Muslim) Amesema Mtume kuwa Mwenye kufunga ramadhani akiwa na imani na na kutarajia malipo kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia.(Bukhari na Muslim) Amesema Mtume kuwa: hakika kuna peponi mtango unaitwa BABU RAYAAN watauingia mlango huo wenye kufunga siku ya kiyama. Na hatauingia mlango huo yeyote isipokuwa watu hao tu na itasemwa “waku wapi wenye kufunga” basi hapo watasimama na hataingia yeyote isipokuwa wao, na pindi watakapoingia utafungwa na katu hataingia yeyote. (Bukhari na Muslim) Mgawnyiko wa funga.
Basi jua ewe ndugu kuwa funga zimegawanyika katika makundi makuu mawili nayo ni :
1.funga za wajibu (lazima)
2.Funga za sunnah (zisizo za lazima) 1.funga za wajibu
Hugawanyika funga hizi katika makundi makuu matatu ambayo ni:
1.funga ambazo ni wajibu kwa kuingia wakati maalum. Nayo ni funga ya ramadhani
2.Funga amabzo ni wajibu kutokana na ‘ila nayo funga za kafara
3.Zilizo wajibu kwa kujiwajibishia mtu mwenyewe. Nazo ni funga za nadhir
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 web hosting 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Hukumu ya talaka iliyotolewa kabla ya tendo la ndoa
Endapo mtu atamuacha mke wake kabla hata ya kukutana kimwili, basi talaka hii itahukumiwa kwa namna hii.
Soma Zaidi...Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali
Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali kulingana na ugonjwa wake.
Soma Zaidi...Hukumu na sherei zinazohusu ajira na kazi katika uislamu
Wajibu wa KufanyakaziUislamu siyo tu unawahimiza watu kufanya kazi na kutokuwa wavivu bali kufanya kazi ni Ibada.
Soma Zaidi...