Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga
Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.
Maana.
Maana ya funga kisheria ni kujizuia na vyenye kufunguza toka kuchomoza kwa alfajiri mpaka kuzama kwa jua pamoja na kuwa na niya ya kufanya ibada kwa ajili ya Allah. Fadhila za funga
Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga. Kwa hakika hiyo funga ni yangu, na mimi ndiye ninayeilipa ( thawabu) na funga ni ngome. Basi atakapfunga mmoja wenu asizungumze maneno ya upuuzi, wala asifanye mambo machafu na ya kijinga. Basi ikitikea mtu amemtukana au kumpiga yeye (asilipize) bali amwambie “nini mimefunga”. Na akasema Mtume (s.a.w) “na ninaapa kwa yule ambaye nafsi ya Muhammad ipo kwenye mkono wak: hakika harufu ya mdomo wa mwenye kufunga inapendeza zaidi mbele ya Allah siku ya kiyama kuliko harufu ya mafuta ya misk. Na ana mwenye kufunga furaha mbili: atakapofutari na atakapokutana na Mo;a wake atafurahia funga yake. (Bukhari na Muslim) Amesema Mtume kuwa Mwenye kufunga ramadhani akiwa na imani na na kutarajia malipo kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia.(Bukhari na Muslim) Amesema Mtume kuwa: hakika kuna peponi mtango unaitwa BABU RAYAAN watauingia mlango huo wenye kufunga siku ya kiyama. Na hatauingia mlango huo yeyote isipokuwa watu hao tu na itasemwa “waku wapi wenye kufunga” basi hapo watasimama na hataingia yeyote isipokuwa wao, na pindi watakapoingia utafungwa na katu hataingia yeyote. (Bukhari na Muslim) Mgawnyiko wa funga.
Basi jua ewe ndugu kuwa funga zimegawanyika katika makundi makuu mawili nayo ni :
1.funga za wajibu (lazima)
2.Funga za sunnah (zisizo za lazima) 1.funga za wajibu
Hugawanyika funga hizi katika makundi makuu matatu ambayo ni:
1.funga ambazo ni wajibu kwa kuingia wakati maalum. Nayo ni funga ya ramadhani
2.Funga amabzo ni wajibu kutokana na ‘ila nayo funga za kafara
3.Zilizo wajibu kwa kujiwajibishia mtu mwenyewe. Nazo ni funga za nadhir
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Madhara ya riba kwenye jamii
Haya ni madhara ya riba katika jamii. Ni kwa namna gani jamii inadhurika kutokana na riba?
Soma Zaidi...Mambo Yanayobatilisha Swala Katika Uislamu
Swala ni nguzo ya pili ya Uislamu na ni ibada muhimu sana kwa Muislamu. Ili swala ikubalike mbele ya Mwenyezi Mungu, lazima itekelezwe kwa kufuata masharti na nguzo zake. Kuna mambo mbalimbali ambayo yakitokea wakati wa swala yanaweza kuibatilisha na kuifanya isikubalike. Katika makala hii tutajifunza mambo yanayobatilisha swala, sababu zake, na jinsi ya kujiepusha nayo.
Soma Zaidi...Je inafaha kuingizwa eda na kutolewa?
Kuingizwa au Kutolewa EdaKatika sheria ya Kiislamu hapana suala Ia kuingizwa au kutolewa eda na Sheikh.
Soma Zaidi...Taratibu za eda ya kufiwa katika uislamu
Hapa utajifunza taratibu za kukaa eda kwa mwanamke ambaye amefiwa na mume.
Soma Zaidi...