Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga

Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.

Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga


Download kitabu hiki hapa

Maana. Maana ya funga kisheria ni kujizuia na vyenye kufunguza toka kuchomoza kwa alfajiri mpaka kuzama kwa jua pamoja na kuwa na niya ya kufanya ibada kwa ajili ya Allah. Fadhila za funga Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga. Kwa hakika hiyo funga ni yangu, na mimi ndiye ninayeilipa ( thawabu) na funga ni ngome. Basi atakapfunga mmoja wenu asizungumze maneno ya upuuzi, wala asifanye mambo machafu na ya kijinga. Basi ikitikea mtu amemtukana au kumpiga yeye (asilipize) bali amwambie “nini mimefunga”. Na akasema Mtume (s.a.w) “na ninaapa kwa yule ambaye nafsi ya Muhammad ipo kwenye mkono wak: hakika harufu ya mdomo wa mwenye kufunga inapendeza zaidi mbele ya Allah siku ya kiyama kuliko harufu ya mafuta ya misk. Na ana mwenye kufunga furaha mbili: atakapofutari na atakapokutana na Mo;a wake atafurahia funga yake. (Bukhari na Muslim) Amesema Mtume kuwa Mwenye kufunga ramadhani akiwa na imani na na kutarajia malipo kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia.(Bukhari na Muslim) Amesema Mtume kuwa: hakika kuna peponi mtango unaitwa BABU RAYAAN watauingia mlango huo wenye kufunga siku ya kiyama. Na hatauingia mlango huo yeyote isipokuwa watu hao tu na itasemwa “waku wapi wenye kufunga” basi hapo watasimama na hataingia yeyote isipokuwa wao, na pindi watakapoingia utafungwa na katu hataingia yeyote. (Bukhari na Muslim) Mgawnyiko wa funga. Basi jua ewe ndugu kuwa funga zimegawanyika katika makundi makuu mawili nayo ni : 1.funga za wajibu (lazima) 2.Funga za sunnah (zisizo za lazima) 1.funga za wajibu Hugawanyika funga hizi katika makundi makuu matatu ambayo ni: 1.funga ambazo ni wajibu kwa kuingia wakati maalum. Nayo ni funga ya ramadhani 2.Funga amabzo ni wajibu kutokana na ‘ila nayo funga za kafara 3.Zilizo wajibu kwa kujiwajibishia mtu mwenyewe. Nazo ni funga za nadhir


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 694

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Ijuwe swala ya Tawbah na jinsi ya kuiswali

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya sinnah ya tawba.

Soma Zaidi...
Sanda ya mtoto

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Taasisi za Kifedha Katika Mfumo wa Uchumi wa Kiislamu

- Ni taasisi za kifedha zinazohusika na kuhifadhi akiba na mali za watu zenye thamani kubwa kama dhahabu, n.

Soma Zaidi...
Zaka ni nini? Nini maana ya zaka katika uislamu

Zaka, kilugha ni kukua; kubariki na kuzidi kheri.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya swala

Jifunze namna ya kuswali, zijuwe aina za swala na ujifunze masharti ya swala, kwa nini swala hazijibiwi? nini kifanyike?

Soma Zaidi...
Swala ya kuomba mvua swalat istiqaa na jinsi ya kuiswali.

Hapa nitakujulisha kuhusu swala ya kuomba mvia, na taratibu za kuiswali.

Soma Zaidi...