Sababu ya uislamu kuwa ndiyo dini sahihi pekee


image


Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)


  1. Sababu Ya Uislamu Kuwa Ndiyo Dini Sahihi Pekee. 

Uislamu ndio dini pekee inayostahiki kuchaguliwa na kufuatwa kama muongozo sahihi wa maisha na watu wote kwa sababu zifuatazo;

 

  1. Uislamu unaeleza ukweli juu ya maumbile na nafasi ya mwanaadamu hapa Duniani;

Uislamu unaeleza lengo la kuumbwa mwanaadamu kuwa ni ibada na kumtumikia Mwenyezi Mungu na kuwa msimamizi wa sheria na hukumu zake hapa ulimwenguni ili kupata radhi zake.

Rejea Qur’an (51:56) na (2:29).

 

  1. Sheria na kanuni za Uislamu zinaendana na kanuni za kimaumbile;

Uislamu ndiyo dini pekee inaenda na kuzingatia kanuni na taratibu zote za kimaumbile za kibailojia kifizikia na kikemia ya viumbe vyote vilivyo na visivyo hai ikiwa ni pamoja na maumbile au mazingira yanayotuzunguka.

Rejea Qur’an (3:83) na (30:30).

 

  1. Uislamu ndio dini inayotosheleza matashi yote ya mwanaadamu kimwili na kiroho;

Uislamu ni dini inayotoa muongozo namna ya mtu kumiliki hisia zake na kuendea mambo katika hali tofauti tofauti kama vile wakati wa furaha, shida, huzuni, misiba, n.k.

Rejea Qur’an (2:155-157).

 

  1. Uislamu ni njia kamili ya maisha;

Ni Uislamu pekee ndio mfumo kamili wa maisha ya kila siku ya mwanaadamu katika fani na nyanja zote za kibinafsi na kijamii kama vile kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni.

 

  1. Uislamu una ibada maalum za kumjenga mwanaadamu kimaadili;

Uislamu umeweka muongozo katika kumuadilisha mwanaadamu kupitia ibada maalum kama vile swala, funga, hija, kutoa zakat na sadaqat na zinginezo za sunnah.

 

  1. Uislamu ni dini ya walimwengu wote na wa nyakati zote;

Uislamu umekuwa ni mwongozo wa maisha tangu binaadamu wa kwanza hadi wa mwisho katika Nyanja zote za maisha bila kujali taifa, ukoo, rangi na hadhi ya watu.

Rejea Qur’an (42:13).

 

  1. Uislamu ni dini ya kusimamia haki, uadilifu na usawa;

Ni dini ya Uislamu ndiyo inayotoa na kusimamia kwa usawa na uadilifu haki, hukumu na adhabu zote kwa watu wote bila ya upendeleo na ubaguzi wa rangi, taifa, hadhi na ukoo.

Rejea Qur’an (103:1-3), (9:33), (61:9) na (17:105).



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    3 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Lengo la kuumbwa Mwanadamu ni lipi?
Kwenye kipengele hichi tutajifunza lengo la kuumbwa mwaanadamuengo la kuumbwa ulimwengu na viumbe vilivyomo. Soma Zaidi...

image Tofauti kati ya hijjah na umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Sanda ya mwanamke na namna ya kumkafini
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu
Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu Ni upi? (EDK form 1: mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu) Soma Zaidi...

image Kumswalia maiti, masharti ya swala ya maiti
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mafunzo yatokanayo na maandalizi ya mtume ki-wahay
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kwanini lengo la funga halifikiwi na wafungaji wengi
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Zoezi la 3
Kipengele hichi kina maswali mbalimbali kuhusiana na dini na mitazamo mbalimbali. Soma Zaidi...

image Yaliyoharamishwa kwa mwenye kuwa katika ihram
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mfumo wa ulinzi na usalama katika fola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...