image

Ujue ugonjwa wa tauni

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa tauni ambao kwa kitaalamu huitwa plague ni Ugonjwa unaosababishwa na wadudu ambao huitwa kitaalamu huitwa yersinia pestis ambao ukaa ndani ya panya.

 Ujue ugonjwa wa tauni.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kuwa ugonjwa wa tauni ni Ugonjwa unaosababishwa na wadudu wanaoitwa kwa kitaalamu yersinia pestis wadudu hawa uishi ndani ya panya na viroboto ambao ufyonza damu kwenye panya ufyonza pamoja na wadudu hawa, na pia viroboto uweza kung'ata binadamu na kuingiza wadudu wanaoitwa yersinia pestis ambao usababisha ugonjwa wa tauni ambao uwatesa watu wengi na kusababisha madhara mbalimbali kwenye jamii.

 

2. Ugonjwa huu umeenea katika sehemu mbalimbali za Afrika, Asia, na Amerika inavyokadiriwa ni kuwa kuanzia mwaka elfu moja mia tisa tisini na nne mpaka elfu mbili na tatu watu elf mbili mia nane na hamsini wameripotiwa na shirika la WHO, asilimia tisini waliokuwa wameugua ugonjwa huu ni waafrika ukilinganisha na mataifa mengine ,kwa hiyo na Tanzania mpaka sasa kuna sehemu ambapo ugonjwa bado upo na unaowasumbua watu sehemu ambazo zinapatwa na Ugonjwa huu ni sehemu zenye unyevunyevu kwa wingi ukilinganisha na sehemu nyingine.

 

3. Ugonjwa huu kwa ujumla unaweza kutibiwa na kupotea kabisa kwenye jamii kwa sababu watu wanapaswa kuzingatia usafi ili kuepuka kuwepo kwa panya ambao wanatunza hawa wadudu na pia kwenye kipindi cha mavuno watu wanapaswa kuwa makini ili kuweza kuepuka kuongezeka kwa panya ambao ndio chanzo cha Ugonjwa huu,kwa wakati mwingine dalili za Ugonjwa huu uchanganya watu na kuwa kama Dalili za kawaida kama vile homa na mwili kuishiwa nguvu ila zinabadilika kadri ugonjwa inavyoongezeka.

 

4.Dalili nyingine ambazo zinaweza kujitokeza ni kama vile miwasho kwenye mwili, maumivu ya kichwa ambayo yanaweza kuanza taratibu na ukitumia dawa yanaisha na baadae yanaanza tena  maumivu kwenye mwili, kichefuchefu na kutapika, kuwepo kwa vipele kwenye kwapa, na Dalli hizi utofautiana na kuongezeka kadri siku na mda unavyoenda.

 

5.Kwa hiyo jamii nzima inapaswa kuelimishwa kuhusu Ugonjwa huu na kujua Dalili zake kwa sababu wakati mwingine Dalili hizi ufanana na magonjwa mengine ya kawaida kwa hiyo ni lazima kuzijua kwa uhakika ili kuweza kupata huduma sahihi na kuepukana na madhara mengine makubwa.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2156


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Vidonda vya tumbo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa vidonda vya tumbo Soma Zaidi...

Dalili za Kufunga kwa ulimi (tongue tie)
Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili za Kufunga kwa ulimi (Tongue-tie) kuanzia Mtoto anavyo zalia mpaka navyokua ni hali inayotokea wakati wa kuzaliwa ambayo kitaalamu hujulikana kama ankyloglossia. Soma Zaidi...

Dalili kuu za Malaria mwilini
Malaria husababishwa na vijidudu vidogo parasite wanaojulikana kama plasmodium. Vijidudu hivi hubebwa na mbu aina ya anophelesi. Kuna ina nyingi za plasmodium lakini aina 5 tu ndizo husababisha malaria Soma Zaidi...

Minyoo na athari zao kiafya
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu minyoo na athari zao kiafya Soma Zaidi...

Je unaweza sex na mwanamke mwenye HIV na ukaenda kupima wiki moja na ukagundurika kwa vipimo vya maabara
Utakapofanya ngono na aliyeathirika haimaanishi na wewe kuwa lazima utakuwa umeathirika. Kuathirika kuna mambo mengi lazima yafanyike. Soma Zaidi...

Kiungulia na tiba zake kwa wajawazito.
Posti hii inahusu kiungulia kwa wanawake wajawazito na tiba yake, ni ugonjwa au hali inayowapata wajawazito walio wengi kwa sababu ya kuwepo kwa mabadiliko ya homoni wakati wa ujauzito. Soma Zaidi...

Homa ya Dengue, dalili za homa ya dengue na Njia ya kujikinga nayo
HOMA YA DENGUEHoma ya dengue ni miongoni mwa maradhi hatari ambayo husambazwa na mbu. Soma Zaidi...

Namna ya kuepuka Ugonjwa wa ngiri.
Posti hii inahusu zaidi namna au njia za kuepuka na Ugonjwa huu wa ngiri ambao uleta madhara kwa watoto, vijana na watu wazima, kwa hiyo ili tuweze janga hili ni lazima tufanye yafuatayo. Soma Zaidi...

VIDONDA VYA TUMBO NA ATHARI ZAKE
Soma Zaidi...

Dalili za mkojo mchafu na rangi za mkojo na mkojo mchafu
Hapautajifunza rangi kuu za mkojo na dalili zako kiafya, mkojo mchafu na dalili zake Soma Zaidi...

Hatua za Maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi.
Posti hii inahusu zaidi hatua mbalimbali za Ugonjwa wa Ukimwi, kawaida Ugonjwa huu huwa na hatua kuu nne ila kila hatua huwa na sifa zake kwa hiyo tunapaswa kujua hatua za Ugonjwa huu na kujaribu kuzuia maambukizi yasisambae kabisa. Soma Zaidi...

Chanzo cha VVU na UKIMWI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyanzo m ali mbali vinavyohisiwa kuwa chanzo cha UKIMWI Soma Zaidi...