Fahamu Ugonjwa wa mshtuko wa sumu.
Ugonjwa wa Mshtuko wa Sumu ni matatizo ya nadra, yanayotishia maisha ya aina fulani za maambukizi ya bakteria. Mara nyingi ugonjwa wa mshtuko wenye sumu hutokana na sumu zinazozalishwa na bakteria.
Dalili za ugonjwa wa mshtuko wa sumu
Dalili zinazowezekana za ugonjwa wa mshtuko wa sumu ni pamoja na:
1. Homa kali ya ghafla
2. Shinikizo la chini la damu (hypotension)
3. Kutapika au Kuharisha
4. Upele unaofanana na kuchomwa na jua, haswa kwenye viganja na nyayo zako
5. Mkanganyiko
6. Maumivu ya misuli
7. Uwekundu wa macho yako, mdomo na koo
8. Mshtuko wa moyo
9. Maumivu ya kichwa
10.mwili kukosa nguvu.
Mambo ya hatari yanayosababisha Ugonjwa wa mshtuko was sum.
Ugonjwa wa Mshtuko wa Sumu unaweza kuathiri mtu yeyote. Karibu nusu ya visa vya ugonjwa wa Mshtuko wa sumu hutokea kwa wanawake wa hedhi; wengine hutokea kwa wanawake wazee, wanaume na watoto.
Ugonjwa wa Mshtuko wa Sumu umehusishwa na:
1. Kuwa na michubuko au Kuungua kwenye ngozi yako
2. Baada ya kufanyiwa upasuaji hivi karibuni
3. Kutumia sponji za uzazi wa mpango.
4. Kuwa na maambukizi ya virusi, kama vile Mafua au Tetekuwanga
Mwisho; ikiwa una dalili au ishara za ugonjwa wa Mshtuko wa sumu Ni vyema kuwahi hospitali kwaajili ya matibabu. Hii ni muhimu hasa ikiwa una maambukizi ya ngozi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo
Post hii inahusu zaidi dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ingawa sio watu wote wenye dalili kama hizi Wana uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo Ila zikitokea mtu anapaswa
Soma Zaidi...Dalili za kipindupindu na njia za kujilinda na kipindupindu.
Post hii inazungumzia zaidi kuhusiana na ugonjwa wa kipindupindu.kipindupindu ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu ambaye kwa kitaalamu anaitwa vibrio cholera.mdudu huyu hushambulia utumbo mdogo na kusababisha madhara mengi.
Soma Zaidi...Namna ya kuishi na vidonda vya tumbo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kuishi na vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...ATHARI ZA KIAFYA ZA KUTOTIBU MALARIA AU KUCHELEWA KUTIBU MALARIA
Pindi malaria isipotibiwa inaweza kufanya dalili ziendelee na hatimaye kusababisha kifo.
Soma Zaidi...Matumizi ya dawa za kulevya na athari zake kwenye ubongo.
Dawa za kulevya hazibadili tu tabia ya mtu, bali zinasababisha mabadiliko ya kudumu kwenye muundo na utendaji kazi wa ubongo. Makala haya yanachambua jinsi dawa hizi zinavyoiba mfumo wa furaha wa ubongo (reward system), na jinsi matumizi yake yanavyoweza kusababisha madhara ya kiakili na kimwili ambayo ni vigumu kuyatengua.
Soma Zaidi...Dalili za ngozi kuwasha.
Posti hii inaonyesha kiufupi kabisa kuhusiana na dalili za ngozi kuwashwa.
Soma Zaidi...