Fahamu Ugonjwa wa mshtuko wa sumu.
Ugonjwa wa Mshtuko wa Sumu ni matatizo ya nadra, yanayotishia maisha ya aina fulani za maambukizi ya bakteria. Mara nyingi ugonjwa wa mshtuko wenye sumu hutokana na sumu zinazozalishwa na bakteria.
Dalili za ugonjwa wa mshtuko wa sumu
Dalili zinazowezekana za ugonjwa wa mshtuko wa sumu ni pamoja na:
1. Homa kali ya ghafla
2. Shinikizo la chini la damu (hypotension)
3. Kutapika au Kuharisha
4. Upele unaofanana na kuchomwa na jua, haswa kwenye viganja na nyayo zako
5. Mkanganyiko
6. Maumivu ya misuli
7. Uwekundu wa macho yako, mdomo na koo
8. Mshtuko wa moyo
9. Maumivu ya kichwa
10.mwili kukosa nguvu.
Mambo ya hatari yanayosababisha Ugonjwa wa mshtuko was sum.
Ugonjwa wa Mshtuko wa Sumu unaweza kuathiri mtu yeyote. Karibu nusu ya visa vya ugonjwa wa Mshtuko wa sumu hutokea kwa wanawake wa hedhi; wengine hutokea kwa wanawake wazee, wanaume na watoto.
Ugonjwa wa Mshtuko wa Sumu umehusishwa na:
1. Kuwa na michubuko au Kuungua kwenye ngozi yako
2. Baada ya kufanyiwa upasuaji hivi karibuni
3. Kutumia sponji za uzazi wa mpango.
4. Kuwa na maambukizi ya virusi, kama vile Mafua au Tetekuwanga
Mwisho; ikiwa una dalili au ishara za ugonjwa wa Mshtuko wa sumu Ni vyema kuwahi hospitali kwaajili ya matibabu. Hii ni muhimu hasa ikiwa una maambukizi ya ngozi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 web hosting 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
FIKRA POTOFY KUHUSU VIDONDA VYA TUMBO
FIKRA POTOFY KUHUSU VIDONDA VYA TUMBO Vidonda vya tumbo huja na maoni mengi potofu.
Soma Zaidi...Maumivu ya tumbo kitomvuni, sababu zake na dalili zake
Hapa utajifunza sababu za kuwepo na maumovu ya tumbe kitomvuni.
Soma Zaidi...Sababu kuu za maumivu ya tumbo chini ya kitomvu, Tumbo la ngiri na chango
Makala hii inakwenda kukuletea somo linalozungumzia maumivu ya tumbo chini ya kitomvu, na tumbo la ngiri kwa wanaume, na tumbo la chango kwa wanawake
Soma Zaidi...Nini husababisha ugonjwa wa kifua na maumivu ya kifua?
Posti hii inazungumzia sababu zinazopelekea kuumwa na kifua.
Soma Zaidi...dalili za mwanzo za ukimwi kwa mwanamke
Katika makala hii utakwenda kuzijuwa baadhi ya dalili za ukimwi ama HIV kwa mwanamke
Soma Zaidi...Fahamu Ugonjwa wa upungufu wa Adrenali.
Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa upungufu wa Adrenali ni ugonjwa ambao hutokea wakati mwili wako hutoa kiasi cha kutosha cha homoni fulani zinazozalishwa na tezi zako za adrenali. ugonjwa huu hutokea katika makundi yote ya umri na huathiri
Soma Zaidi...