Chanzo cha kiungulia
Post hii inahusu zaidi vyanzo vya kuwepo kwa kiungulia, kiungulia ni kitendo cha kupanda kwa gesi kutoka kwenye tumbo mpaka kwenye mdomo,hali uwasumbua wengi na kusababisha hali isiyo rafiki.
Vyanzo vya kiungulia.
1. Kudhoofika kwa utendaji kazi wa kizuizi cha juu cha tumbo kwa kitaalamu huitwa (lower esophagus sphincter) sehemu hii uhakikishe kuwa kila kitu ambacho kinaenda mwilini hakirudi ila sehemu hii ikiharibika usababisha kurudi kwa vyakula na vitu vingine kutoka kwenye tumbo kwenda kwenye mdomo.
2. Mfumo dhaifu wa mmeng'enyo wa chakula.
Kuna wakati mwingine kunakuwepo na mfumo dhaifu wa mmeng'enyo wa chakula .
Kwa sababu ya kuwepo kwa vyakula mbalimbali ambavyo uleta shida kwenye mmeng'enyo wa chakula kama vyakula vya mafuta, sukari, vyakula vya caffeine, chocolate na vyakula vya aina hiyo Usababisha mmeng'enyo wa chakula kutoenda sawa na hatimaye kusababisha kiungulia.
3. Kuwepo kwa kiwango kikubwa cha tindikali kwenye mmeng'enyo wa chakula,
Kwa kawaida tindikali ni lazima kwenye mmeng'enyo wa chakula ila ikizidi inaleta kiungulia aina hii ya tindikali ambayo ukaa tumboni kwa kitaalamu huitwa hydrocholic asidi, ikiwa nyingi upanda mpaka kwenye mdomo na kusababisha kiungulia.
4. Kuwepo kwa baadhi ya madini kwenye mwili .
Kwa sababu kwenye mwili wa binadamu kuna madini mbalimbali na kila aina ya madini ufanya kazi tofautitofauti na yakikosa usababisha matatizo mengi mwilini . Kwa mfano ukosefu wa madini ya magnesium na potassium, yakikosa usababisha kuongezeka kwa kiungulia.
5. Kuwepo kwa uzito mkubwa na kitambi.
Kwa kawaida uzito mkubwa ni chanzo cha magonjwa mengi kwa sababu kuna watu wanene na hawafanyi mazoezi usababisha na wanaopenda kula sana usababisha chakula kupanda juu na kusababisha kiungulia.
6. Wamama wajawazito na wenye umri mkubwa.
Kuna wakati mwingine wamama wajawazito wanakuwa na kiungulia kwa sababu ya hali zao na wengine wenye umri mkubwa kwa sababu ya kushuka kwa immunity upate kiungulia.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Kitau cha Fiqh π2 web hosting π3 Bongolite - Game zone - Play free game π4 Kitabu cha Afya π5 ai web app π6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Madhara ya kulala usiku sana
βPost hii inachunguza changamoto za kiafya zinazotokana na kukosa usingizi wa kutosha au kuchelewa kulala. Tutajadili athari zake kwenye mfumo wa kinga, uwezo wa kufikiri, na uzalishaji wa homoni, huku tukitoa vidokezo vya kuboresha mzunguko wako wa kulala kwa maisha bora.
Soma Zaidi...Kiasi gani cha maji kinatakiwa kunywa kwa siku?
Kunywa maji ya kutosha ni nguzo kuu ya afya bora, lakini swali la "ni kiasi gani hasa?" limekuwa likileta utata kwa muda mrefu. Makala haya yanachunguza sayansi nyuma ya mahitaji ya maji mwilini, ikivunja dhana potofu ya "glasi nane kwa siku," na kutoa mwongozo wa kitaalamu kulingana na umri, jinsia, kiwango cha mazoezi, na mazingira ya hali ya hewa.
Soma Zaidi...Tatizo la kutokwa na damu baada ya tendo la ndoa.
Kutokwa na damu baada ya tendo la ndoa (post-coital bleeding) ni hali inayoweza kuleta hofu kwa wanawake wengi. Ingawa mara nyingi sababu zake si za kutisha, ni muhimu kuelewa visababishi mbalimbali vinavyoweza kuashiria matatizo ya kiafya yanayohitaji matibabu. Makala hii inachunguza kwa kina sababu za kibiolojia, maambukizi, na magonjwa yanayoweza kusababisha hali hii, ikitoa mwongozo wa wakati wa kumwona daktari.
Soma Zaidi...Dalili za Mgonjwa wa kisukari
Post hii inahusu dalili za mtu Mwenye ugonjwa wa kisukari, dalili hizi zinaweza kujitokeza Moja kwa Moja mtu akagundua kuwa ana Ugonjwa wa kisukari.zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa kisukari.
Soma Zaidi...fangasi, aina zao, dalili zao na matibabu yao
Fangasi na Aina zao Fangasi wa kwenye kucha Fangasi wa Mapunye Fangasi aina ya candida Fangasi wa Mdomoni na kooni Fangasi wa kwenye uke Fangasi wanaoshambulia mfumo wa damu na ogran kama moyo, figo n.
Soma Zaidi...