Posti hii inahusu zaidi mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kupunguza kiwango cha kuwepo kwa magonjwa ya kuambukiza, kwa hiyo zifuatazo ni mbinu ambazo zinapaswa kutumika ili kupunguza kiwango cha magonjwa ya kuambukiza.
1.kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa kuna magonjwa mengi ya kuambukiza ingawa tunajaribu kuyatibu ila si yote yanaweza kuisha ila kuna njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kupunguza kiwango cha kuwepo kwa magonjwa ya kuambukiza.njia zenyewe ni kama ifuatavyo.
2.Kuangalia mazingira.
Kwanza kabisa mazingira ya watu yanapaswa kuangaliwa, yaani maisha ya watu kwa ujumla kwa mfano usafi pakiwepo choo, maji yaliyochenshwa na kuchujwa na mambo mengine ambayo yanaweza kuwa chanzo cha uchafu.
2. Pia kuangalia chakula kinachotumiwa na watu wa kwenye mazingira kama kinaweza kuwasaidia watu kuweza kuwa na kinga ya kupambana dhidi ya magonjwa na jinsi ya kutumia chakula kama ni sahihi.
3. Vile vile tunapaswa kuangalia kama kuna mtu yeyote kwenye jamii ana Dalili za ugonjwa tunapaswa kukusanya sampuli na kuzipeleka maabara ili kutambua tatizo lililopo na kuweza kutatua tatizo kwenye mazingira.
4. Pia kama kuna Ugonjwa ambao umekidhiri kwenye jamii husika ambao unaleta shida na matatizo makubwa kwa jamii hiyo chanjo ni lazima ili kuweza kutokomeza Tatizo lililopo.
5. Tibu magonjwa yaliyomo kwenye mazingira kwa kutumia dawa mbalimbali ambazo zimeagizwa na wahudumu wa afya baada ya kugundua ugonjwa uliopo kwenye mazingira.
6 . Pia elimu inapaswa kutolewa kwa jamii baada ya kuangalia mazingira, chakula kinachotumiwa na watu waliopo kwenye mazingira husika ili kuhakikisha kuwa wanatumia chakula kwa kuzingatia mlo kamili na kuepuka utapia mlo kwa watoto na watu wazima.
7. Kuhakikisha kubwa mazingira yanakuwa masafi kwa kukata nyasi ndefu, kufukia mashimo,kuchoma takataka mbalimbali zilizoizunguka nyumba na kuhakikisha kuwa watu wamefundishwa namna ya kutunza mazingira na pia kuhakikisha kubwa wanachemsha maji na kuchuja kabla ya kunywa.
8. Kuhakikisha mazingira hayana wadudu wanaosababisha magonjwa, wadudu kama vile chawa, mbu, viroboto, kunguni na wengine wengi ambao ukaa kwenye mazingira ya watu, kama kuna dawa wanaweza kuuawa ili kupunguza Magonjwa.
9. Pia kuhakikisha watu wanapata mahitaji ya msingi ya maisha kama vile makazi, mavazi na chakula pia wapewe na dawa kama kuna Magonjwa vile vile na wale ambao hawajiwezi kabisa wanapaswa kutafutiwa huduma za kijamii kwa kupitia viongozi wa serikali.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi maambukizi kwenye uume, maambukizi hata utokea kwenye kichwa Cha uume kwa kitaalamu huitwa Balanitis, zifuatazo ni sababu za kuwepo kwa ugonjwa huu.
Soma Zaidi...Katika post hii utajifunza maana ya homa ya ini. Pia utajifunza chanzo kinachosababisha homa ya ini. Makala hii itakuwa endelevu hivyo usikose muendelezo wake.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi mtu aliyekula chakula chenye sumu, chakula chenye sumu ni chakula ambacho kikitumiwa na mtu yeyote kinaweza kuleta madhara kwenye mwili wa binadamu hata kifo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kujikinga na magonjwa, kwa kawaida tunajua wazi kuwa magonjwa yapo na yanasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na mengine hayasambai yanaweza kumpata mtu mmoja akapona au magonjwa mengine si ya kupona
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukutajia baadhi tu ya sababu zinazopelekea kuumwa na tumbo. Hali hizi zinawweza kuwapata watu wa jinsia zote katika umri wowote ule. Ijapokuwa nyingine si kwa wote ni kwa baadhi ya watu. hapa nitakuletea sababu 5 tu.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya njia za kupambana na kuzuia gonorrhea
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za kutokea kwa maumivu ya jino
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea pale ambapo Ugonjwa wa ngiri unaposhindwa kutibiwa mapema.
Soma Zaidi...Posti hii itakwenda kuelezea mambo machache kuhusu ugonjwa wa kisukari
Soma Zaidi...Magonjwa ya kuambukiza ni maradhi yanayosababishwa na vijidudu kama vile bakteria, virusi, fangasi au vimelea. Viumbe vingi vinaishi ndani na kwenye miili yetu. Kwa kawaida hazina madhara au hata kusaidia, lakini chini ya hali fulani, baadhi ya viumbe
Soma Zaidi...