image

Mbinu za kupunguza Magonjwa ya kuambukiza.

Posti hii inahusu zaidi mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kupunguza kiwango cha kuwepo kwa magonjwa ya kuambukiza, kwa hiyo zifuatazo ni mbinu ambazo zinapaswa kutumika ili kupunguza kiwango cha magonjwa ya kuambukiza.

Mbinu za kupunguza Magonjwa ya kuambukiza.

1.kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa kuna magonjwa mengi ya kuambukiza ingawa tunajaribu kuyatibu ila si yote yanaweza kuisha ila kuna njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kupunguza kiwango cha kuwepo kwa magonjwa ya kuambukiza.njia zenyewe ni kama ifuatavyo.

 

2.Kuangalia mazingira.

Kwanza kabisa mazingira ya watu yanapaswa kuangaliwa, yaani maisha ya watu kwa ujumla kwa mfano usafi pakiwepo choo, maji yaliyochenshwa na kuchujwa na mambo mengine ambayo yanaweza kuwa chanzo cha uchafu.

 

2. Pia kuangalia chakula kinachotumiwa na watu wa kwenye mazingira kama kinaweza kuwasaidia watu kuweza kuwa na kinga ya kupambana dhidi ya magonjwa na jinsi ya kutumia chakula kama ni sahihi.

 

3. Vile vile tunapaswa kuangalia kama kuna mtu yeyote kwenye jamii ana Dalili za ugonjwa tunapaswa kukusanya sampuli na kuzipeleka maabara ili kutambua tatizo lililopo na kuweza kutatua tatizo kwenye mazingira.

 

4. Pia kama kuna Ugonjwa ambao umekidhiri kwenye jamii husika ambao unaleta shida na matatizo makubwa kwa jamii hiyo chanjo ni lazima ili kuweza kutokomeza Tatizo lililopo.

 

5. Tibu magonjwa yaliyomo kwenye mazingira kwa kutumia dawa mbalimbali ambazo zimeagizwa na wahudumu wa afya baada ya kugundua ugonjwa uliopo kwenye mazingira.

 

6 . Pia elimu inapaswa kutolewa kwa jamii baada ya kuangalia mazingira, chakula kinachotumiwa na watu waliopo kwenye mazingira husika ili kuhakikisha kuwa wanatumia chakula kwa kuzingatia mlo kamili na kuepuka utapia mlo kwa watoto na watu wazima.

 

7. Kuhakikisha kubwa mazingira yanakuwa masafi kwa kukata nyasi ndefu, kufukia mashimo,kuchoma takataka mbalimbali zilizoizunguka nyumba na kuhakikisha kuwa watu wamefundishwa namna ya kutunza mazingira na pia kuhakikisha kubwa wanachemsha maji na kuchuja kabla ya kunywa.

 

8. Kuhakikisha mazingira hayana wadudu wanaosababisha magonjwa, wadudu kama vile chawa, mbu, viroboto, kunguni na wengine wengi ambao ukaa kwenye mazingira ya watu, kama kuna dawa wanaweza kuuawa ili kupunguza Magonjwa.

 

9. Pia kuhakikisha watu wanapata mahitaji ya msingi ya maisha kama vile makazi, mavazi na chakula pia wapewe na dawa kama kuna Magonjwa vile vile na wale ambao hawajiwezi kabisa wanapaswa kutafutiwa huduma za kijamii kwa kupitia viongozi wa serikali.

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 932


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Sababu za maumivu ya viungo na viungo kuwaka moto nini sababu zake
Soma Zaidi...

Dalili za mawe kwenye kibofu Cha mkono
Mawe ya kibofu ni mkusanyiko mgumu wa madini kwenye kibofu chako. Mawe kwenye kibofu hukua wakati mkojo kwenye kibofu chako unapokolea, na kusababisha madini katika mkojo wako kung'aa. Soma Zaidi...

Fahamu Ugonjwa wa uti wa mgongo kwa watoto uitwao poliomyelitis
Poliomyelitis ni kuvimba kwa suala la kijivu la uti wa mgongo na wakati mwingine sehemu ya chini ya ubongo Soma Zaidi...

Nini husababisha ugonjwa wa kifua na maumivu ya kifua?
Posti hii inazungumzia sababu zinazopelekea kuumwa na kifua. Soma Zaidi...

Sababu za miguu kufa ganzi.
Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali,za miguu kufa ganzi,ni tatizo ambalo uwakumba watu wengi na walio wengi hawafahamu kabisa ni sababu zipi ambazo uleta tatizo hili. Soma Zaidi...

dalili za mimba changa ndani ya wiki moja
Je na wewe ni katika ambao wanahitaji kujuwa dalili za mimba ndani ya wiki moja? kama ndio makala hii ni kwa ajili yako. Utakwenda kuona dalili za mwanzo sana za ujauzito toka siku za mwanzoni. Soma Zaidi...

YAJUE MARADHI YA KISUKARI
Posti hii itakwenda kuelezea mambo machache kuhusu ugonjwa wa kisukari Soma Zaidi...

Dalili za tonsillitis (mafindo mafindo)
Tonsillitis kwa kiswahili hujulikana kama mafundomafundo ambayo hutokea pande mbili karibu na Koo na huwa na uvimbe na zikikaa kwa muda bila matibabu hutoa usaha.Dalili na dalili za ugonjwa wa tonsillitis ni pamoja na Soma Zaidi...

ujuwe ugonjwa wa gout na athari zake mwilini
Post hii itakwenda kuzungumzia ugonjwa wa gout unaosababishwa na ongezeko la asidi mwilini. Soma Zaidi...

Ni nini husababisha mate kujaa mdomoni, na ni yapi matibabu yake
Hapa tutaangalia baadhi ya sababu zinazopelekea mdomo kujaa mate na namna ya kutibu tatizo la kujaa kwa mate mdomoni Soma Zaidi...

Fahamu ugonjwa wa kaswende wakati wa ujauzito.
Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kaswende wakati wa ujauzito, kaswende inaweza kukaa kwa mtu zaidi ya miaka mingi bila kuleta madhara ya moja kwa moja lakini kadiri ya siku zinavyokwenda madhara utokea hasa wakati wa ujauzito, madhara hayo umwadhiri mtot Soma Zaidi...

Dalili za selulitis.
Selulitis ni maambukizi ya ngozi ya bakteria ya kawaida, ambayo yanaweza kuwa mbaya. Cellulitis inaonekana kama sehemu nyekundu ya ngozi iliyovimba na inahisi joto na laini. Inaweza kuenea kwa kasi kwa sehemu nyingine za mwili. Cellulitis haienei kuto Soma Zaidi...