Posti hii inahusu zaidi mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kupunguza kiwango cha kuwepo kwa magonjwa ya kuambukiza, kwa hiyo zifuatazo ni mbinu ambazo zinapaswa kutumika ili kupunguza kiwango cha magonjwa ya kuambukiza.
1.kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa kuna magonjwa mengi ya kuambukiza ingawa tunajaribu kuyatibu ila si yote yanaweza kuisha ila kuna njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kupunguza kiwango cha kuwepo kwa magonjwa ya kuambukiza.njia zenyewe ni kama ifuatavyo.
2.Kuangalia mazingira.
Kwanza kabisa mazingira ya watu yanapaswa kuangaliwa, yaani maisha ya watu kwa ujumla kwa mfano usafi pakiwepo choo, maji yaliyochenshwa na kuchujwa na mambo mengine ambayo yanaweza kuwa chanzo cha uchafu.
2. Pia kuangalia chakula kinachotumiwa na watu wa kwenye mazingira kama kinaweza kuwasaidia watu kuweza kuwa na kinga ya kupambana dhidi ya magonjwa na jinsi ya kutumia chakula kama ni sahihi.
3. Vile vile tunapaswa kuangalia kama kuna mtu yeyote kwenye jamii ana Dalili za ugonjwa tunapaswa kukusanya sampuli na kuzipeleka maabara ili kutambua tatizo lililopo na kuweza kutatua tatizo kwenye mazingira.
4. Pia kama kuna Ugonjwa ambao umekidhiri kwenye jamii husika ambao unaleta shida na matatizo makubwa kwa jamii hiyo chanjo ni lazima ili kuweza kutokomeza Tatizo lililopo.
5. Tibu magonjwa yaliyomo kwenye mazingira kwa kutumia dawa mbalimbali ambazo zimeagizwa na wahudumu wa afya baada ya kugundua ugonjwa uliopo kwenye mazingira.
6 . Pia elimu inapaswa kutolewa kwa jamii baada ya kuangalia mazingira, chakula kinachotumiwa na watu waliopo kwenye mazingira husika ili kuhakikisha kuwa wanatumia chakula kwa kuzingatia mlo kamili na kuepuka utapia mlo kwa watoto na watu wazima.
7. Kuhakikisha kubwa mazingira yanakuwa masafi kwa kukata nyasi ndefu, kufukia mashimo,kuchoma takataka mbalimbali zilizoizunguka nyumba na kuhakikisha kuwa watu wamefundishwa namna ya kutunza mazingira na pia kuhakikisha kubwa wanachemsha maji na kuchuja kabla ya kunywa.
8. Kuhakikisha mazingira hayana wadudu wanaosababisha magonjwa, wadudu kama vile chawa, mbu, viroboto, kunguni na wengine wengi ambao ukaa kwenye mazingira ya watu, kama kuna dawa wanaweza kuuawa ili kupunguza Magonjwa.
9. Pia kuhakikisha watu wanapata mahitaji ya msingi ya maisha kama vile makazi, mavazi na chakula pia wapewe na dawa kama kuna Magonjwa vile vile na wale ambao hawajiwezi kabisa wanapaswa kutafutiwa huduma za kijamii kwa kupitia viongozi wa serikali.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowPosti hii inahusu zaidi njia za maambukizi ya Homa ya inni, Homa ya inni usababishwa na virusi viitwavyo Hepatitis B, huwapata watu wote hasa wale wenye umri chini ya miaka mitano.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi visababishi vya ugonjwa wa Bawasili,kuna watu wengi wanapenda kujua kabisa chanzo cha kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii na kuna maswali mengi yanayoulizwa kuhusu visababishi vya Bawasili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu huduma kwa wanawake wenye mahitaji maalum, ni wanawake ambao wana shida ya akili, walionyanyaswa kijinsia, wakimbizi na wote wenye matatizo mbalimbali.
Soma Zaidi...Jipu la jino ni mfuko wa usaha unaosababishwa na maambukizi ya bakteria.
Soma Zaidi...mm nahis miguu pamoja na mikono kuishiwa nguvu ni mgongo kuuma ni dalili za ugonjwa gan ?
Soma Zaidi...Jifunze dalili za gonorrhea na namna inavyoambukiza, zipi athari za gonori kwa wanawae na wanaume
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa upele na matatibabu yake, ni ugonjwa unaosabavishwa na mdudu kwa kitaalamu huitwa mites sarcoptes scrabie mdudu huyu usababisha miwasho kwenye ngozi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu athari za maambukizi ya magonjwa ya ngono ambapo magonjwa ya ngono isipokuwa UKIMWI yanatibika .mgonjwa anashauriwa kuwahi hospitali au kituo chochote cha afya kupata matibabu mara anapoona dalili za magonjwa haya.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kujibu swali la muulizaji. Kuhusu syyle za tendo la ndoa
Soma Zaidi...Virusi vya Ebola ni virusi vinavyohusiana vinavyosababisha Homa za hemorrhagic magonjwa yanayoambatana na kutokwa na damu nyingi (kuvuja damu), viungo kushindwa kufanya kazi na, mara nyingi, kifo. Virusi vya Ebola na virusi huishi kwa wanyama, na wanad
Soma Zaidi...