Jinsi ya kuswali swala vitani

Jinsi ya kuswali swala vitani

Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika ilibkuswalibukiwa vitani.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Kusimamisha Swala Vitani

Muislamu haruhusiwi kuswali swala ya faradhi nje ya wakati wake hata akiwa katika vita vya kupigania Dini ya Allah(s.w). Bali Allah (s.w) ametuhafifishia swala, tukiwa vitani na kutuelekeza tuswali ifuatavyo:

 

“Na unapokuwa pamoja nao (Wa is lamu katika vita) ukawaswalisha, basi kundi moja miongoni mwao wasimame pamoja nawe (waswali) na washike silaha zao. Na watakapomaliza sijda zao basi na wende nyuma yenu (kulinda); na lile kundi jingine ambalo halijaswali lisw ali pamoja naw e, nao washike hadhari yao na silaha zao (humo ndani ya swala, maana) wale waliokufuru wanataka mghafilike na silaha zenu na vitu vyenu ili wakuvamieni mvamio wa mara moja. Wala si vibaya kwenu ikiwa mnaona udhia kwa sababu ya mvua au mnaona ugonjwa, kuondoa silaha zenu,.

 

Na mshike hadhari yenu. Hakika Mwenyezi Mungu amewaandalia makafiri adhabu itakayowadhalilisha”. (4:102)
Namna ya kusimamisha swala katika uwanja wa vita kutokana na maelekezo ya aya hii ni kwamba, askari wagawanyike katika makundi mawili ambayo yataswalishwa na Imamu mmoja na swala itafupishwa kama ilivyo katika swala ya safari. Kundi moja litaanza kuswali na Imamu wakiwa na silaha zao na kundi lingine litabaki katika ulinzi. Imamu ataswali rakaa moja na hili kundi la kwanza na watakaponyanyuka kuswali rakaa ya pili Imamu atabakia pale akiendelea kusoma Qur-an na kila mtu katika wale wanaomfuata, atamaliza upesi upesi rakaa ya pili na baada ya kutoa Salaam atarudi nyuma upesi kuchukua nafasi ya ulinzi. Baada ya kundi la pili kupokelewa nafasi zao, watakwenda kujiunga na Imamu ambaye bado anaendelea na rakaa yake ya pili. Wote watakapojiunga na swala, Imamu atamalizia swala yake ya rakaa mbili. Baada ya Imamu kutoa salaam kila mmoja katika wale wanaomfuata atasimama na kumalizia rakaa yake ya pili.

 


Aya hii ya (4:102) inayotuelekeza namna ya kuswali tukiwa katika vita vya kupigania Dini ya Allah (s.w) inafuatiwa na aya inayotoa amri ya kusimamisha swala kwa nyakati zake kama tunavyosoma:

 

Mwishapo kuswali kuweni mnamkumbuka Mwenyezi Mungu - msimamapo na mkaapo na (mlalapo) ubavu. Na mtakapopata amani, basi simamisheni swala (kama kawaida). Kwa hakika swala kw a Waislamu ni faradhi iliyow ekewa nyakati maalumu. (4:1 03)

 


Hebu fikiri: Kama askari wa Allah (s.w) aliyejitoa muhanga kwa mali yake, ahli zake na nafsi yake kwa ajili ya kupigania dini ya Allah (s.w) hakuruhusiwa kuiacha swala au kuiswali nje ya wakati wake, je wewe uliyezama kwenye shughuli nyingine ndio utegemee kusamehewa kwa kupitisha wakati wa swala ukaswali wakati unapojiona kuwa huna shughuli. Aya hii inatufahamisha kwa uwazi kuwa swala tano zimefaradhishwa kwetu pamoja na nyakati zake makhsusi.

 


Tukiondoa ruhusa tulizopewa kuziswali swala kidharura tunapokuwa vitani, na tukiondoa udhuru wa kusahau na kupitiwa na usingizi hapana ruhusa yoyote iliyotolewa katika Qur-an au Hadithi inayokubalika kuswali kadha kama wengi wafanyavyo. Je, mtindo huu wa kuswali kadha tunauiga kwa nani? Je, huku sio kupuuza swala? Kama tunapuuza swala kwa nini tusitarajie kupata ghadhabu za Allah (s.w) badala ya kujidanganya na kujipa matumaini ya kupata malipo mema kutoka kwake kutokana na kadha zetu hizo. Ujira wa wapuuzaji wa swala unabainishwa katika Qur-an:

 

Basi, adhabu itawathibitikia wanao swali. Ambao wanapuuza zao. (10 7:4-5).

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1289

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Namna ya kuosha maiti hatua kwa hatua
Namna ya kuosha maiti hatua kwa hatua

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
NI ZIPI SWALA ZA SUNNAH: (qabliya (kabliya) na baadiya, tahajudi, tarawehe, qiyamu layl, shukr, istikhara)
NI ZIPI SWALA ZA SUNNAH: (qabliya (kabliya) na baadiya, tahajudi, tarawehe, qiyamu layl, shukr, istikhara)

Sunnah za SwalaSunnah za Swala Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi.

Soma Zaidi...
Yaliyo haramu kwa mtu asiyekuwa na udhu
Yaliyo haramu kwa mtu asiyekuwa na udhu

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ambauo ni haramu kwa mtu asiye na udhu.

Soma Zaidi...
Maana ya mirathi katika uislamu
Maana ya mirathi katika uislamu

Post hii itakufundishabkuhusu mirathi ya kiislamu, maana yake.

Soma Zaidi...
Kuenea kwa dhana ya udhibiti uzazi na uzazi wa mpango
Kuenea kwa dhana ya udhibiti uzazi na uzazi wa mpango

Kustawi kwa Kampeni ya Kudhibiti UzaziMiongoni mwa sababu zilizosaidia kustawi kwa kampeni hii ni matokeo ya mapinduzi ya viwanda (Industrial revolution) ya huko Ulaya.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake
Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake

Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...
Maana ya sadaqat
Maana ya sadaqat

Nguzo za imani, maana ya sadaqat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nguzo za swala ya maiti
Nguzo za swala ya maiti

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...