Hizi ndio nyakati za swala tano na jinsi ya kuchunga nyakati za swala.

Hizi ndio nyakati za swala tano na jinsi ya kuchunga nyakati za swala.

Posti hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkuchunga nyakatibza swala tano.

Download Post hii hapa

3. Kuchunga wakati

“... Kwa hakika swala kwa waumini ni faradhi iliyowekewa nyakati makhususi” (4:103).
Swala tano zilizofaradhishwa kwa Umma huu wa Mtume Muhammad (s.a.w) ni:- Adhuhuri, Alasiri. Magharibi, Ishai na Alfajiri. Wakati wa kuswali kila swala unabainishwa katika hadith ifuatayo:

 


“Abdullah Ibn ‘Amir amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema, Wakati w a sw ala ya adhuhuri ni kuanzia jua linapopinduka hadi kivuli cha mtu kin apokuwa sawa na kimo (urefu) chake. Na unamalizika kwa kuingia

 

Alasiri. Na muda wa swala ya Alasiri (ni kuanzia inapomalizika Adhuhuri) hadi jua linapopiga umanjano. Muda wa swala Magharibi (ni mara baada ya kuzama jua na) utabakia mpaka wingu jekundu litow eke. Muda wa swala ya Isha (ni baada ya kutoka Mgharibi) na kubakia hadi katikati ya usiku. Na wakati wa swala ya Alfajiri unaanza kwa kudhihirika kwa ukanda mweupe mpaka kabla ya kuchomoza jua. Jua linapochomoza jizuilie kusw ali kw ani huchomoza kati ya pembe za shetani. (Muslim)
Kutokana na hadithi hii, nyakati za swala tano ni:

 


Adhuhuri: Inayopasa kuswaliwa mara tu jua linapogeuka kuelekea Magharibi mpaka kuingia swala ya al’asiri.

 


Al’asiri: Huanza pale urefu wa kivuli unapokuwa sawa na kitu chenyewe mpaka kivuli kinapokuwa mara dufu ya urefu wa kitu ch en yewe.

 


Magharibi: Huanza mara tu jua linapozama na kuingia pale mawingu mekundu yanapobadilika kuwa ya kimanjano wakati inapoingia swala ya Isha.

 


Isha: Kuanzia mara tu yanapobadilika mawingu kuwa ya kimanjano mpaka usiku wa manane.

 


Alfajir: Huingia kwa kutokea alama ya mstari mweupe unaotokea Mashariki ambao ni alama ya kwisha kwa usiku na kuanza kwa mchana. Kuingia kwa Alfajiri kwa alama hii ya uzi mweupe ndio mwisho wa kula daku kwa mwenye kufunga kama isemavyo Qur-an:

 

“... Na kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa Alfajiri katika weusi wa usiku ...” (2:187)
Hizi ndizo swala tano na nyakati zake kama alivyotufundisha Mtume (s.a.w) ambazo hutegemea uchunguzi wa mwendo wa jua katika saa ishirini na nne za siku.

 

Utaalamu wa karne hii umerahisisha kuzijua nyakati za mwanzo na mwisho wa kila, swala kwa kutengeneza ratiba ya nyakati za swala kwa kutumia takwimu za mwendo wa jua katika nyakati zilizonukuliwa kwa muda mrefu na wachunguzi wa hali ya hewa.


Kuswali swala katika wakati wa mwanzo ni bora zaidi kama tunavyojifunza katika hadith ifuatayo:-
“Ummi Farawata(r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) aliulizwa, ni kitendo gani kilicho bora kuliko vyote? Akajibu: “Swala wakati wake wa mwanzo”.(Ahmad, tirm idh, Abu Daud).

 


Swala hukubaliwa kwa Kuwahi rakaa moja ndani ya wakati

 


Iwapo Muislamu kwa dharura atachelewa kuiswali swala ya faradh kiasi cha kupata rakaa moja tu ndani ya wakati,swala yake itakubaliwa kwa mujibu wa Hadith ifuatayo:


Abu Hurairah(r.a) ameeleza kuwa Mtume (s.a.w) amesema: “Mwenye kupata rakaa moja ya swala ameipata swala ”.(Maimamu sahihi sita tu).
Si vizuri kabisa kwa Muislamu, kwa makusudi kuchelewesha swala kiasi hicho.

 


Nyakati zilizoharamishwa kuswali

Kwa mujibu wa Hadith mbali mbali kuna nyakati tano zilizoharamishwa kuswali na Mtume (s.a.w):-
1. Kuswali sunnah baada ya swala ya Alfajiri mpaka jua litakapochom oza.


2. Wakati wa kuchomoza jua mpaka litakapopanda juu kabisa kiasi cha urefu wa mkuki.


3. Jua linapokuwa katikati wakati wa mchana mpaka litakaposogea kidogo upande wa Magharibi.


4. Kuswali sunnah baada ya swala ya alasiri mpaka jua litakapozama kabisa.
5. Wakati wa kuzama jua.

 

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 4916

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Mambo ya kuzingatia kabla ya kugawa mirathi
Mambo ya kuzingatia kabla ya kugawa mirathi

Haya ni mamno muhimu yanayozingatiwa kabla ya kuanza zoezi la kugawa mirathi ya marehemu.

Soma Zaidi...
Mwenendo wa mwenye kunuia hijjah na umrah
Mwenendo wa mwenye kunuia hijjah na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kwanini lengo la funga halifikiwi na wafungaji wengi
Kwanini lengo la funga halifikiwi na wafungaji wengi

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kuenea kwa dhana ya udhibiti uzazi na uzazi wa mpango
Kuenea kwa dhana ya udhibiti uzazi na uzazi wa mpango

Kustawi kwa Kampeni ya Kudhibiti UzaziMiongoni mwa sababu zilizosaidia kustawi kwa kampeni hii ni matokeo ya mapinduzi ya viwanda (Industrial revolution) ya huko Ulaya.

Soma Zaidi...
Sera ya uchumi katika uislamu
Sera ya uchumi katika uislamu

Hapa utajifunza sera za kiuchumi katika uchumi wa kiislamu. Hapa utajifunza sera kuu tatu za uchumi wa kiislamu.

Soma Zaidi...
Swala ya Istikhara na jinsi ya kuiswali
Swala ya Istikhara na jinsi ya kuiswali

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya Istikhara

Soma Zaidi...