Utaratibu wa kuzika, hatua kwa hatua, na namna ya kusindikiza jeneza

4.

Utaratibu wa kuzika, hatua kwa hatua, na namna ya kusindikiza jeneza

Utaratibu wa kuzika, hatua kwa hatua, na namna ya kusindikiza jeneza

4. Kuzika.

Kusindikiza jeneza.
- Waislamu (watu) wataongozana nayo mpaka kaburini kimya kimya.
- Jeneza lisitanguliwe na watu (msafara).
- Haitakiwi watu kukaa kabla ya jeneza kukalishwa chini.



Kaburi.
- Kaburi liwe pana na kina cha kutosha, mtu kuweza kusimama na kunyoosha mkono kama kuna uwezekano.
- Kisha lichimbwe shimo dogo (mwana ndani) upande wa Qibla ndani ya kaburi.
- Urefu na ukubwa wa kaburi unategemea na ukubwa wa maiti.



Namna ya Kuzika hatua kwa hatua.
a)Waingie watu kaburini kwa idadi ya witiri; 3, 5, 7, n.k.
b)Jeneza liwekwe upande wa kaburi itakapokuwa miguu ya maiti.
c)Maiti itolewe na kutanguliza kichwa kuelekea kaburini.


d)Wapokeaji kaburini watamuweka magotini mwao ili kufungua kamba kichwani, tumboni na miguuni. Pia watafunua shavu la kulia ili liguse ardhini (mchanga) atakapolazwa ndani ya mwana-ndani.

e)Maiti italazwa katika mwana-ndani kwa ubavu wa kulia na kuelekezwa Qibla. Wakati wa kuilaza ni sunnah kusema,
Kama ilivyosimuliwa na Ibn Umar (r.a) kuwa, Mtume (s.a.w) alipokuwa akizika alikuwa akisema:
“Bismillaah wabilahi wa’alaa millati Rasuulullaahi”
Tafsiri:
“Kwa jina la Allah na kwa uwezo wa Allah na kwa mujibu wa mwenendo wa Mtume wa Allah.” (Ahmad, Tirmidh, Ibn Majah).



f)Maiti ipindishwe miguuni na kichwani ili uso na miguu iweze kugusa kuta za mwana-ndani. Kifua, tumbo na sehemu za katikati zibinuliwe nyuma kidogo.

g)Maiti iwekewe mawe au udongo nyuma ya kichwa na miguu isibinuke. Pia ni sunnah kusoma aya za Qur’an (2:1-5) au (2:285-286).

h)Baada ya maiti kulazwa na kusomewa aya hizi, ifunikwe kwa ubao na kama kuna matundu ya kupitisha udongo pazibwe kwa majani.

i)Kabla kaburi halijafunikwa, vitupiwe viganja vitatu vya udongo, na kila tupo unasoma aya ya Qur’an (20:55).
1. Tupo la 1: “Min-haa khalaq-naakum” – Kutokana na hii (ardhi) tumekuumbeni.
2. Tupo la 2: “Wa fiyhaa nughiydukum” – Na humo (katika ardhi) tutakurudisheni.
3. Tupo la 3: “Wa min-haa nukhrjukum taaratan-ukhraa” – Na humo
(katika ardhi) tutakutoweni mara nyingine.



j)Kaburi lijazwe udongo mpaka lijae na kuinuliwa kiasi cha shiburi moja na kuwekewa alama miguuni na kichwani au kupanda miti mibichi.
- Ni vizuri kumiminia maji juu yake ili kuepusha vumbi kupeperushwa na upepo.
- Ni haramu kujengea kaburi kwa namna yeyote ile, kukaa juu yake, kuwasha taa
juu yake na kuielekea wakati wa kuswali.
‘Jabir (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amekataza kuyajengea makaburi au kuyajengea nyumba juu yake au kukaa juu yake’. (Muslim)



Abu Marsad Al-ghafariyyi ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema:
“Msikae juu ya makaburi na wala msiswali kwa kuyaelekea.”
(Muslim)



- Baada ya kuzika Mtume (s.a.w) alikuwa akisimama na kusema:
“Muombeeni msamaha ndugu yenu na muombeeni awe
na kauli thabiti kwani sasa anaulizwa”



- Ni sunnah baada ya mazishi kuwapa mikono wafiwa na kuwausia subira
Rejea Qur’an (2:155-156).
- Pia haifai kusema (kusengenya) mabaya ya marehemu.



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1165

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda

Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi

Soma Zaidi...
Hijjah

Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kujitwaharisha Najisi hafifu na najisi ndogo

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi hafifu na najisi ndogo.

Soma Zaidi...
Hija ya Kuaga na Kutawafu kwa Mtume (s.a.w)

Hija ya Kuaga na Kutawafu kwa Mtume (s.

Soma Zaidi...
Mambo yanayoharibu Udhu (yanayobatilisha udhu)

Post hii inakwenda kukufundisha mambo ambayo hubatilisha udhu yaani mam,boa mbayo yanaharibu udhu.

Soma Zaidi...
HUKUMU YA KUUWA MTU (KUMWAGA DAMU) KWENYE UISLAMU

عَنْ ابْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم "لَا يَحِلُّ دَمُ امْرِئٍ مُسْلِمٍ [ يشهد أن ل?...

Soma Zaidi...