Endapo mtu atamuacha mke pasi na ridhaa yake yaani amelazimishwa ama amemuwacha wakati amerukwa na akili. Je ni ipo hukumu yake.
Talaka ya Aliyerukwa na akili na aliyetenzwa nguvu
Talaka si jambo Ia kulifanyia maskhara Muislamu anatakiwa awe hadhiri wakati wa kutoa talaka. Ahakikishe kuwa wakati anaamua kutoa talaka akili yake iko katika hali ya utulivu. Talaka ya aliyerukwa na akili haiswihi kama tunavyojifunza katika Hadith:
Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: "Kila talaka ni halali isipokuwa talaka ya punguani na mwenye kurukwa na akili". (Tirmidh).
Pia mtu akilazimishwa kutoa talaka pasina sababu za kisheria au mume na mke wakitalakishwa kwa nguvu huku bado wanapendana katika mipaka ya Allah (s.w), talaka hiyo haitaswihi kama tunavyojifunza katika Hadithi:
Aysha (r.a) ameeleza kuwa amemsikia Mtume wa Allah akisema: "Hakuna talaka wala hakuna kumwacha huru mtumwa kwa nguvu ". (Tirmidh).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Hadithi hii inakwenda kukufundisha historia fupi ya adhana pia utakwenda kujifunza jinsi ya kuadhini na kuqimu.
Soma Zaidi...Katika post hii utakwenda kuzijuwa aina za twahara katika uislamu. Utaviona vigawanyo vya twahara kulingana na maulamaa wa Fiqh
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi.
Soma Zaidi...Haya ni maandalizi ya kumuandaa maiti baada ya kufariki.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha maana ya neno talaka katika uislamu kisheria na kilugha.
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...