Menu



Taratibu za eda ya kufiwa katika uislamu

Hapa utajifunza taratibu za kukaa eda kwa mwanamke ambaye amefiwa na mume.

Eda ya Kufiwa

Eda ni kipindi cha kungojelea mwanamke baada ya kupewa talaka au baada ya kufiwa na mumewe. Katika kipindi cha eda ni haramu mwanamke kuolewa na mume mwingine. Ambapo tumejifunza kuwa eda ya kuachwa inaisha baada ya twahara tatu au miezi mitatu (kwa wale wasiopata hedhi) au baada ya kujifungua (kwa mke aliyeachwa), eda ya kuachwa inachukua miezi minne na siku kumi au siku mia moja thelathini (130).


Hukumu ya Eda ya kufiwa inabainishwa katika Qur-an:

Na wale wanaofishwa (wanaokufa) miongoni mwenu na kuacha wake; hawa (wake) wangoje (wasiolewe) miezi mine na siku kumi. Na wanapofikia muda wao (wa kumaliza eda yao hiyo), basi si dhambi juu yenu kwa yale wanayoyafanyia nafsi zao (hao wanawake) kwa yanayowafiki (kufuata) Sharia. Na Mwenyezi Mungu anazo habari za yote mnayoyatenda. Wala Si dhambi kwenu katika kupeleka habari ya posa kwa ishara tu (Si kwa maneno) kuwaoa wake (walio edani), wala (hapana dhambi pia) katika kutia katika nyoyo zenu azma (za kuwaoa) Mwenyezi Mungu anajua kwamba nyinyi mtawakumbuka.

Lakini msifunge nao ahadi kwa Sifl (ya kuwaoa maadam eda haijesha) isipokuwa mseme maneno yaliyo mazuri. Wala msiazimie kufunga ndoa mpaka muda uliyoandikwa (katika eda) ufike mwisho wake. Na jueni ya kwamba Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo katika nafsi zenu, basi mwogopeni. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, (na) Mpole sana. (2:234-235)


Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa kizuka (mwanamke aliyefiwa na mumewe) anapokuwa katika eda harusiwi kuolewa wala hata kuposwa wala hata kudhihirishiwa nia ya kuolewa baada ya eda. Bali ni ruhusa kuweka azma moyoni na kuongea naye kwa wema bila kuidhihirisha azma hiyo.

 

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1723


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zifazofanana:-

Nini maana ya twahara katika uislamu
Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya twahara katika uislamu. Pia utakwenda kujifunza hukumu za twahara, aina za twahara na mambo mengineyo Soma Zaidi...

Historia ya adhana na nama ya kuadhini
Soma Zaidi...

Njia za kudhibiti riba
Ufumbuzi wa tatizo la ribaRiba imeenea na kuzoeleka duniani kwa kiasi ambacho watu wengi wanadhani kuwa bila riba hakuna shughuli yoyote ya uchumi inayowezekana. Soma Zaidi...

Jinsi ya kusherehekea siku ya idi katika uislamu
Uislamu umeweka taratibu maalumu za kuzifata katika kusherehekea siku ya idi. Soma Zaidi...

Nafasi ya serikali katika ugawaji
Soma Zaidi...

Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda
Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi Soma Zaidi...

Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake
Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

Ni kwa nini riba imeharamishwa kwenye Uislamu
Hapa utajifinza uharamu wa riba na sababu za kuharamishwa kwake. Soma Zaidi...

namna ya kuswali swala ya vitani
Soma Zaidi...

Usitamani kifo hata ukiwa mchamungu mno ama muovu mno
Katika uislamu imekatazwa kutamani kufa hata kama utakuwa ni mtu muovu sana ama mchamungu sana. Soma Zaidi...