Taratibu za eda ya kufiwa katika uislamu

Taratibu za eda ya kufiwa katika uislamu

Hapa utajifunza taratibu za kukaa eda kwa mwanamke ambaye amefiwa na mume.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Eda ya Kufiwa

Eda ni kipindi cha kungojelea mwanamke baada ya kupewa talaka au baada ya kufiwa na mumewe. Katika kipindi cha eda ni haramu mwanamke kuolewa na mume mwingine. Ambapo tumejifunza kuwa eda ya kuachwa inaisha baada ya twahara tatu au miezi mitatu (kwa wale wasiopata hedhi) au baada ya kujifungua (kwa mke aliyeachwa), eda ya kuachwa inachukua miezi minne na siku kumi au siku mia moja thelathini (130).


Hukumu ya Eda ya kufiwa inabainishwa katika Qur-an:

Na wale wanaofishwa (wanaokufa) miongoni mwenu na kuacha wake; hawa (wake) wangoje (wasiolewe) miezi mine na siku kumi. Na wanapofikia muda wao (wa kumaliza eda yao hiyo), basi si dhambi juu yenu kwa yale wanayoyafanyia nafsi zao (hao wanawake) kwa yanayowafiki (kufuata) Sharia. Na Mwenyezi Mungu anazo habari za yote mnayoyatenda. Wala Si dhambi kwenu katika kupeleka habari ya posa kwa ishara tu (Si kwa maneno) kuwaoa wake (walio edani), wala (hapana dhambi pia) katika kutia katika nyoyo zenu azma (za kuwaoa) Mwenyezi Mungu anajua kwamba nyinyi mtawakumbuka.

Lakini msifunge nao ahadi kwa Sifl (ya kuwaoa maadam eda haijesha) isipokuwa mseme maneno yaliyo mazuri. Wala msiazimie kufunga ndoa mpaka muda uliyoandikwa (katika eda) ufike mwisho wake. Na jueni ya kwamba Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo katika nafsi zenu, basi mwogopeni. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, (na) Mpole sana. (2:234-235)


Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa kizuka (mwanamke aliyefiwa na mumewe) anapokuwa katika eda harusiwi kuolewa wala hata kuposwa wala hata kudhihirishiwa nia ya kuolewa baada ya eda. Bali ni ruhusa kuweka azma moyoni na kuongea naye kwa wema bila kuidhihirisha azma hiyo.

 

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1971

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

 NAMNA YA KUCHINJA KATIKA UISLAMU
NAMNA YA KUCHINJA KATIKA UISLAMU

عَنْ أَبِي يَعْلَى شَدَّادِ بْنِ أَوْسٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنْ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "إنَّ اللَّهَ كَتَبَ الْإِح...

Soma Zaidi...
Umuhimu wa funga ya ramadhan
Umuhimu wa funga ya ramadhan

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
TOFAUTI KATI YA MAKATOZO NA MAAMRISHO KATIKA SUNNAH
TOFAUTI KATI YA MAKATOZO NA MAAMRISHO KATIKA SUNNAH

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ عَبْدِ الرَّحْمَنِ بْنِ صَخْرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: سَمِعْت رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم يَقُولُ: "م...

Soma Zaidi...
Jinsi ambavyo msafiri anatakiwa aswali akiwa safarini
Jinsi ambavyo msafiri anatakiwa aswali akiwa safarini

Postvhiibinakwenda kukufundisha kuhusu swala ya msafiri na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...
MALI ZISIZORUHUSIWA KUTOLEWA ZAKA
MALI ZISIZORUHUSIWA KUTOLEWA ZAKA

*Suala la kumilikiwa binaadam (utumwa), japokuwa linaendelea kutajwa kwenye Sharia (katika vitabu), ni suala ambalo haliko.

Soma Zaidi...
 Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga
Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga

Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja
Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja

Je jamii inachukuliaje swala la kuoa mke zaidi ya mmoja.

Soma Zaidi...
Ni ipi hukumu ya kutoa talaka hali ya kuwa umelazimishwa au ukiwa umerukwa na akili
Ni ipi hukumu ya kutoa talaka hali ya kuwa umelazimishwa au ukiwa umerukwa na akili

Endapo mtu atamuacha mke pasi na ridhaa yake yaani amelazimishwa ama amemuwacha wakati amerukwa na akili. Je ni ipo hukumu yake.

Soma Zaidi...