Swala ya tarawehe jinsi ya kuiswali


image


Post hii itakwenda kukufundisha kuhusi swala ya tarawehe, faida zake na jinsi ya kuiswali.


5. Swala ya Tarawehe
Swala ya Tarawehe ni miongoni mwa Sunnah zilizokokotezwa. Swala hii huswaliwa katika mwezi wa Ramadhan tu wakati wowote kati ya kipindi baada ya swala ya Isha na kuingia kwa swala ya Alfajiri. Umuhimu wa swala hii umedhihiri katika Hadithi ifuatayo:

 


Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah alikuwa akisisitiza swala ya usiku katika mwezi wa kufunga (Ramadhani), bila ya kuifaradhisha kwao. Alikuwa akisema: Atakaye swali katika usiku wa mwezi wa kufunga, akiwa na imani na akitarajia malipo (kutoka kwa Allah (s.w), dhambi zake zilizotangulia husamehewa. (Muslim)

 


Mtume (s.a.w) alikuwa akiswali Tarawehe katika sehemu ya pili ya usiku (katika wakati ule ule wa Tahajjud). Mtume (s.a.w) aliswali Tarawehe pamoja na masahaba katika jamaa siku tatu, kisha akaacha na akawa anaswalia nyumbani kwake kama tunavyofahamishwa katika Hadithi ifuatayo:

 


‘Aysha (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) alikwenda msikitini usiku na akaswalisha Tarawehe na watu wakaswali naye. Asubuhi watu wakasimuliana habari hiyo. Mtume (s.a.w) siku ya pili alikwenda kuswalisha watu wakajaa msikitini. Alifanya hivyo hivyo siku ya tatu. Asubuhi siku ya nne watu wakapeana habari na wakajazana zaidi msikitini kwa ajili ya sw ala ya Tarawehe lakini Mtume (s.a.w) hakw enda

 

kuswalisha. Baadhi ya watu walisema kwa sauti “swalah”, lakini Mtume (s.a.w) hakwenda msikitini mpaka Alfajir. Alipomaliza sw ala ya Alfajir aliwakabili watu na kuwaeleza: “Jambo lenu halikuwa limefichikana kwangu, lakini nilichelea kuwa kama ningaliendelea mfululizo na swala hiyo ya Tarawehe huenda ingalifanywa kuwa ni faradhi kwenu na huenda m ungalishindw a kuitekeleza ”. (Muslim)

 


Pamoja na Hadithi hii, pia Mtume (s.a.w) aliwasisitiza Waislamu kuswali swala za Sunnah majumbani mwao na kuwahakikishia kuwa kufanya hivyo kuna malipo makubwa zaidi. Swala ya Tarawehe iliendelea kuswaliwa na kila mtu nyumbani kwake katika kipindi chote cha Mtume (s.a.w) na kipindi cha Khalifa wake wa kwanza (Abu Bakar). Khalifa wa pili, Umar bin Khattab, alianzisha tena kuswali swala ya Tarawehe kwa jamaa msikitini kama inavyoendelea mpaka hivi leo.

 


Idadi ya Rakaa za Swala ya Tarawehe

 


Kumekuwepo na maelezo tofauti kuhusiana na idadi ya rakaa za Swala ya tarawehe kutoka kwa wanazuoni tofauti. Lakini kutokana na Hadithi iliyosimuliwa na Mama Aysha (r.a) na kupokelewa na Maimamu wa Hadithi, Mtume (s.a.w) hakupata kuswali zaidi ya rakaa 11 katika mwezi wowote ule. Hadithi ya Jabir (r.a) iliyopokelewa na Ibnu Khuzaimah na Ib n Hibban, Mtume ameripotiwa kuswali rakaa nane za tarawehe na rakaa tatu za witri pamoja na Masahaba wake na kisha siku iliyofuatia akawa hakutoka kwenda kusalisha.

 


Ama kuhusiana na kuswali rakaa ishirini, ni kweli kuwa Khalifa Umar, Uthman na Ali (r.a) waliswali kwa rakaa hizo. Imamu Ibnu Hibban amesema kuwa mwanzoni ilikuwa ni rakaa kumi na moja isipokuwa kisomo (kisimamo) kilikuwa kirefu kiasi cha watu kuchoka. Hivyo baadaye ikaamuliwa kuwa idadi ya rakaa iongezwe na kisomo kipunguzwe na kuwa cha wastani ingawaje jambo hili halikuingiza Swala ya Witri, kutoka hapo kwenye rakaa 20 ilifika kwa badhi ya wengine akiwemo Imamu Malik hadi rakaa 36 ikiwa kisomo kimezidi kufupishwa. Iliyo sunnah ni kuswali tarawehe kwa rakaa 11-8 za kisimamo cha usiku cha kawaida na rakaa 3 za witri. Kwa kuwa mwezi wa Ramadhani ni mwezi wa Qur-an inahimizwa sana kuwa Waislamu wahitimishe Qur-an yote alau kwa kusoma juzuu moja kila siku. Tarawehe ni swala sawa na swala nyingine hivyo kusihi kwake kunafungamana na kupatikana khushui, masharti na nguzo zote za swala. Ama hizi tarawehe zinazoswaliwa katika misikiti mingi mbazo Imamu hupata sifa kwa kuswali mbio mbio pasipo na mazingatio wala utulivu ni kinyume kabisa na utaratibu wa swala. Watu wengi ambao huharakisha kumaliza swala ya tarawehe kwa kiasi cha kutokamilisha nguzo za swala hawapati malipo yoyote kutokana na swala zao. Bali kwa kuwa watu hawa wanaifanyia swala mchezo hapana cha kutarajia zaidi ya adhabu kali waliyoahidiwa na Allah (s.w):

 

“Basi adhabu itawathibitikia wanao swali, ambao wanapuuza swala zao”. (107:4-5)

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Ni ipi hukumu ya muislamu anayekula mwezi wa Ramadhani bila ya sababu ya kisheria
Endapo muislamu hatafunga mwezi wa Ramadhani bila ya ruhusa je atatakiwa afanye nini. Je ataweza kuilipa funga hiyo? Soma Zaidi...

image Zijuwe nguzo 17 za swala.
Ili swala itimie utahitajika kutimiza nguzo zake na masharti yake. Hapa utajifunza nguzo 17 za swala. Soma Zaidi...

image Nguzo za udhu ni sita
Post hii itakufundisha kuhusu nguzo kuu sita za udhu. Soma Zaidi...

image Maandalizi kwa ajili ya kifo
Mwanadamu anatakiwa aishi huku akikumbuka kuwa ipo siki atakufa. Hivyo basi inatupata lujiandaa mapema kwa ajili ya kifo. Soma Zaidi...

image Historia ya adhana na Iqama na jinsi ya kuadhini.
Hadithi hii inakwenda kukufundisha historia fupi ya adhana pia utakwenda kujifunza jinsi ya kuadhini na kuqimu. Soma Zaidi...

image Swala ya witiri na faida zake, na jinsi ya kuiswali
Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya witiri na faida zake kwa mwenye kuiswali. Soma Zaidi...

image Zijuwe funga za kafara na jinsi ya kuzigunga
Post hii itakufundisha kuhusu funga za kafara, zinavyotokea na na jinsi ya kuzifunga. Soma Zaidi...

image Nini maana ya funga na ni lipi lengo lake
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la funga na maana yake katika uislamu. Soma Zaidi...

image Shart kuu nne za swala
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu masharti ya swala. Soma Zaidi...

image Je ni zipi nguzo za uislamu, na ni ngapi nguzo za uislamu?
Post hii itakujuza maana ya uislamu na nguzo zake. Soma Zaidi...