Kwa nini benki za kiislamu ni bora kuliko benki nyingine?
Uzuri wa benki za Kiislamu
Pamoja na benki za Kiislamu kutoa huduma zinazotolewa na kila benki kama tulivyoziorodhesha huko nyuma, kuna faida za ziada zinazopatikana kutokana na benki hizi kama ifuatavyo:
Kwanza benki za Kiislamu huiokoa jamii na uchumi wake na madhara yote yanayosababishwa na riba.
Pili, Benki za Kiislamu huwaingiza katika uchumi na kuwainua hata wale ambao hawana hata rasilimali yoyote kwa mtindo wa Mudharabah. Hivyo ni kwamba, benki zinazoendeshwa kwa mikopo ya riba, haziwezi kukopesha fedha zake kwa mtu yeyote asiye na rasilimali yenye thamani sawa au zaidi ya mkopo ili atakaposhindwa kulipa ifilisiwe rasilimali hiyo. Kwa mtindo huu wa mikopo ya riba, ni matajiri tu wanaopata mikopo ya benki na masikini wasio na rasilimali yoyote huachwa hivyo hivyo na umasikini wao bila ya msaada kutoka benki wa kuwainua kiuchumi.
Tatu, benki za Kiislamu huinua uchumi wa jamii, kutokana na umakini na tahadhari kubwa zinazochukua katika kuchagua na kuendesha miradi mbali mbali ya uchumi. Kwa kuwa benki zenyewe zinajiingiza katika uchumi, zinahakikisha kuwa miradi zitakazoichagua ni ile yenye uwezo mkubwa wa kuzalisha faida kubwa na yenye uwezekano mdogo wa kusababisha hasara.
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika uislamu imekatazwa kutamani kufa hata kama utakuwa ni mtu muovu sana ama mchamungu sana.
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu, kusimamisha swala za Sunnah (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya witiri na faida zake kwa mwenye kuiswali.
Soma Zaidi...KuzuilianaTumeona kuwa wanaume wenye kurithi ni 15 na wanawake wanaorithi ni 10.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha maana ya kusimamisha swala kama inavyotumika kisheria.
Soma Zaidi...Serikali ina nafasi kubwa katika kuzuia dhulma na kufanya uchumibuwe huru kuyokana na dhulma.
Soma Zaidi...