Sunnah za siku ya idi na utaratibu wa kusherehekea


image


Hapa utajifunza utaratibu wa kusherekea ifil fitir. Pia utajifunza sunnah zinazoambatsns na idil fitir


Iddil -Fitri

 


Iddil-Fitri ni siku kuu ya Kiislamu ya kusherehekea kumalizika kwa Mfungo wa Ramadhani. Mwezi wa Ramadhani ambao ndani yake imefaradhishwa funga ambayo imeambatanishwa na matendo mbali mbali ya sunnah, umekusudiwa uwe mwezi wa mafunzo na mazoezi ya kumfanya mja awe mchaji Mungu katika kiwango kinachostahiki kwa kipindi chote cha mwaka mzima.

 

Iddil-Fitri ndicho kilele cha mafunzo haya ambapo Waislamu wanafurahia na kumshukuru Allah (s.w) kwa kumaliza salama mafunzo haya muhimu na wakati huo huo humuomba Allah (s.w) ayafanye mafunzo hayo yawe yenye kuwafikisha kwenye lengo lililokusudiwa. Hivyo, moja kwa moja inadhihiri kuwa Iddil-Fitri haisherehekewi kwa mavazi mazuri na kwa vyakula na vinywaji vizuri tu, bali kilele cha sherehe hii kinafikiwa kwa kuswali swala ya Iddil-Fitri na kumtukuza na kumuhimidi Allah (s.w) sana kwa Takbira.

 


Swala ya Iddil-Fitri

 


Swala ya Idd mbili - Iddil-Fitri na Iddil-Hajj (kilele cha ibada ya Hija) ni sunnah zilizokokotezwa. Swala ya Idd inaswaliwa kwa rakaa mbili na kufuatiwa na Khutuba mbili kama zile zinazosomwa kabla ya swala ya Ijumaa. Swala ya idd ina Takbira 12,takbira 7 hutolewa katika rakaa ya kwanza kabla ya kusoma suratul-Faatiha na takbira 5 huletwa katika rakaa ya pili. vile vile kabla ya kusoma suratul-Faatiha.Mahali pa kuswalia Idd ni bora pawe uwanjani ili Waislamu wakusanyike pamoja kutoka sehemu mbali mbali za mji. Mtume (s.a.w) alikuwa akifanya hivyo. Ni sunnah kula chochote kabla ya kuswali Iddil-Fitri kama tunavyofahamishwa katika Hadith zifu atazo:

 


Anas (r.a) ameeleza kuw a Mtume w a Allah hakw enda kusw ali Iddil- Fitri mpaka alipokula Tende katika idadi ya witri. (Bukhari).


Buraydah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah alikuwa hatoki kwa swala ya Iddil-Fitri mpaka awe amekula (Kitu) na hakuwa anakula katika s iku ya kuchinja (Iddil-Haj) mpaka asw ali (Dirim i).

 


Ni sunnah kuleta takbira mara kwa mara kuanzia pale mwezi wa Shawwal unapoandama mpaka baada ya swala ya Iddil-fitri. Takbira

 

Tafsiri ya Takbira:
Allah Mkubwa, Allah Mkubwa, Allah Mkubwa hapana mola ila Allah Allah Mkubwa, Allah Mkubwa na shukurani zote ni za Allah. Allah Mkubwa aliyetukuka, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa wingi, na namtakasa asubuhi na jioni. Hapana Mola ila Allah. Wala hatumuabudu yeyote ila Yeye peke yake, tunamtakasa yeye na dini yake hata kama w atachukia makafiri.Hapana mola ila Allah peke yake. Ameisadikisha (ameitimiza) ahadi yake na akamnusuru mja (Mtume s.a.w) wake, na akalitukuza jeshi lake, akalipa ushindi kundi lake. Hapana mola ila Allah. Allah Mkubwa. Ewe Allah, teremsha rehma zako juu ya Muhammad, na Maswahaba wake Muhammad, na waliomnusuru Muhammad, na Wakeze Muhammad, na kizazi chake Muhammad, na uwape salama na amani kwa wingi.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    2 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani offline    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Yajuwe masharti ya udhu yaani yanayofanya udhu kukubalika
Posti hii itakufundisha masharti yanayohitajika kwa mwenye kutaka kutia udhu. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake
Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

image Jinsi ambavyo mtu anazuiliwa kurithi mali ya marehemu
Endapo mtu yupp katika orodha ya wanaotakiwa kutithi, anaweza kuzuiliwa kurithi kwa kuzingatia haya. Soma Zaidi...

image Nini maana ya kusimamisha swala?
Je kusimamisha swala kuna maana gani kwenye uislamu? Soma Zaidi...

image Yaliyo haramu kwa mtu asiyekuwa na udhu
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ambauo ni haramu kwa mtu asiye na udhu. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kushona sanda ya maiti na kumvisha yaani kumkafini
Hapa utajifunza taratibu za kumkafini maiti wa kiislamu. Yaani kushona sanda yake na kumvisha. Soma Zaidi...

image Njia za kujitwaharisha, na vitu vinavyotumika kujitwaharisha
Post hii inakwenda kukufundisha njia zinazotumika kujitwaharisha. Soma Zaidi...

image Je ni kwa nini lengo la finga halifikiwi kwa wafungaji
Lengo la funga ni kuwa mchamungu sasa ni kwa nini wafungaji hawalifikii lengo hili na kuwa wachamungu. Soma Zaidi...

image Swala ya tahiyatul masjidi yaani maamkizi ya msikitini, pamoja na swala za qabliya na baadiya
Post hii inakwenda kukujuza kuhusu swala za qabliya, baadiya na tahiyatul masjid. Soma Zaidi...

image Zijuwe aina kuu 6 za talaka katika uislamu
Talaka zimegawanyika katika makundi mengi. Katika somo hili utakwenda kukifunza aina kuu za talaka katika uislamu. Soma Zaidi...