Hadhi na Haki za Mwanamke Katika Jamii

Hadhi na Haki za Mwanamke Katika Jamii

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Hadhi na Haki za Mwanamke Katika Jamii

Hadhi na Haki za Mwanamke Katika Jamii

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za kijahili

i. Wanawake walikuwa na kazi na nafasi ya kuwastarehesha wanaume tu, yaani ukahaba na umalaya.


ii. Wanawake walikuwa watumishi kwa ajili ya kutunza na kuangalia sifa (afya)

za mabwana zao.



iii. Wanawake pia walikuwa na jukumu kubwa la kuzaa na kulea watoto kwa ajili ya mabwana zao.


iv. Wanawake walinyimwa na kunyanyaswa haki zao kiuchumi na kijamii na kufanywa amtegemee mume moja kwa moja.


v. Talaka haikuwa na nafasi yeyote, mwanamke alilazimika kuishi na mumewe mpaka afe hata kama hawaelewani.


vi. Ndoa za kuolewa mwanamke baada ya kuachwa hazikuwa na nafasi, zilichukuliwa kama uzinzi wa aina yake, (civilized adultery).


vii. Heshima na usawa katika ya mwanamume na mwanamke haikuwepo, heshima ilizingatia maumbile na hadhi ya mwanamke ndani ya jamii.


viii. Mwanamke alikuwa huru kuchanganyikana na wanaume jambo ambalo lilichochea umalaya, ukahaba na kuharibika maadili.




Hifadhi ya Mwanamke na Hekima yake Katika Uislamu

i. Wanawake wana uhuru wa kutoka majumbani mwao kwa kutekeleza haja maalum ili kuchunga heshima yao na kuepusha uchochezi wa zinaa, n.k.
Rejea Qur’an (33:59)

ii. Wanawake kulingana na umbile lao na jukumu lao la kuzaa na kulea, wana haki ya kulindwa heshima yao na kuhifadhiwa majumbani.
Rejea Qur’an (33:33)



iii. Wanaume kuwa viongozi wa wanawake, si kuwa wao ni bora kuliko wanawake, bali wanaume wana kuwa ni walinzi, wahifadhi na viongozi wao.


iv. Kutokana na fursa ya vipaji na vipawa alivyonavyo mwanaume juu ya mwanamke, analazimika kusimamia na kuongoza majukumu mengi zaidi.

v. Kulingana na asili ya maumbile, wanawake hawawezi kuwa sawa kikazi, kimajukumu, kimavazi, kimahusiano, n.k.
Rejea Qur’an (33:36), (24:31), (24:60)



Haki za Mwanamke Katika Uislamu

i. Haki ya mwanamke kupata elimu

- Kujielimisha ni amri kwa wanaume na wanawake, sio wanaume pekee.

Rejea Qur’an (96:1-5)



ii. Haki ya mwanamke katika sitara

- Ni haki kwa mwanamke kupata kulingana na asili ya maumbile yake.

Rejea Qur’an (33:59), (24:31)



iii. Haki ya mwanamke katika uchumi

- Kama ilivyo kwa mwanamume ana haki ya kuchuma na kumiliki uchumi, mwanamke pia ana haki hiyo.
Rejea Qur’an (4:32), (4:4)



iv. Haki ya mwanamke katika jamii (ndoa, mirathi na talaka)

- Mwanamke ana haki ya kuolewa na mwanamume anayemridhia kwa kuzingatia sheria za Kiislamu kwa hiari.

- Mwanamke ana haki ya kumuacha mume atakayeshindwa kuishi naye na kufikia lengo la ndoa. Mfano talaka ya I’laa, Khul’u, Mubaarat, n.k.


- Haki ya mwanamke mjane au aliyeachwa kuolewa tena na wanaume wanaowapenda kisheria.


- Mwanamke ana haki na fungu la kurithi kama alivyo mwanamume pindi mmoja wapo atakapokufa.
Rejea Qur’an (4:7)



v. Haki ya mwanamke katika sheria

- Mwanamume na mwanamke wana haki sawa mbele ya sheria katika kuhukumiwa, kuadhibiwa, kudai haki, n.k. bila ya ubaguzi wowote.
Rejea Qur’an (5:38), (24:2)



- Mwanamke kama mwanamume, ana haki ya kutoa ushahidi mahakamani pale inapobidi.
Rejea Qur’an (2:282)



vi. Haki ya mwanamke kushiriki katika uongozi na siasa

- Jukumu la kuendesha maisha ya jamii liko kwa mwanamume na mwanamke katika kuamrisha mema na kukataza mabaya.


- Suala la uongozi wa kifamilia na kijamii ni la wote, mwanamume na mwanamke isipokuwa mwanamke haruhusiwi kuwa kiongozi wa nchi.
Rejea Qur’an (9:71), (58:1-4)



                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 595

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Mwenendo wa Mtu aliyetoa Shahada
Mwenendo wa Mtu aliyetoa Shahada

Muislamu aliyetoa shahada ya kweli hanabudi kumfanya Mtume (s.

Soma Zaidi...
MAMBO YANAYOBATILISHA (HARIBU) SWALA YAKO
MAMBO YANAYOBATILISHA (HARIBU) SWALA YAKO

Lugha ya Swala Lugha ya swala,kuanzia kwenye Takbira ya kuhirimia Swala mpaka kumalizia swala kwa Salaam, ni Kiarabu.

Soma Zaidi...
Namna lengo la zakat linavyofikiwa
Namna lengo la zakat linavyofikiwa

Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Namna ya kurithisgha hatuwa kwa hatuwa.
Namna ya kurithisgha hatuwa kwa hatuwa.

Hspa utajifunza sasa jinsi ya kugawa mirathi kutokana na viwango maalumu.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kusherehekea siku ya idi katika uislamu
Jinsi ya kusherehekea siku ya idi katika uislamu

Uislamu umeweka taratibu maalumu za kuzifata katika kusherehekea siku ya idi.

Soma Zaidi...
Haki za maadui katika vita (mateka wa kivita)
Haki za maadui katika vita (mateka wa kivita)

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Utaratibu wa kuzika maiti ya kiislamu, hatua kwa hatua
Utaratibu wa kuzika maiti ya kiislamu, hatua kwa hatua

Kuzika Kuzika ni kitendo cha nne cha faradh tunacho lazimika kumfanyia ndugu yetu aliyetutangulia kufa.

Soma Zaidi...