image

Hadhi na Haki za Mwanamke Katika Jamii

Hadhi na Haki za Mwanamke Katika Jamii

Hadhi na Haki za Mwanamke Katika Jamii

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za kijahili

i. Wanawake walikuwa na kazi na nafasi ya kuwastarehesha wanaume tu, yaani ukahaba na umalaya.


ii. Wanawake walikuwa watumishi kwa ajili ya kutunza na kuangalia sifa (afya)

za mabwana zao.



iii. Wanawake pia walikuwa na jukumu kubwa la kuzaa na kulea watoto kwa ajili ya mabwana zao.


iv. Wanawake walinyimwa na kunyanyaswa haki zao kiuchumi na kijamii na kufanywa amtegemee mume moja kwa moja.


v. Talaka haikuwa na nafasi yeyote, mwanamke alilazimika kuishi na mumewe mpaka afe hata kama hawaelewani.


vi. Ndoa za kuolewa mwanamke baada ya kuachwa hazikuwa na nafasi, zilichukuliwa kama uzinzi wa aina yake, (civilized adultery).


vii. Heshima na usawa katika ya mwanamume na mwanamke haikuwepo, heshima ilizingatia maumbile na hadhi ya mwanamke ndani ya jamii.


viii. Mwanamke alikuwa huru kuchanganyikana na wanaume jambo ambalo lilichochea umalaya, ukahaba na kuharibika maadili.




Hifadhi ya Mwanamke na Hekima yake Katika Uislamu

i. Wanawake wana uhuru wa kutoka majumbani mwao kwa kutekeleza haja maalum ili kuchunga heshima yao na kuepusha uchochezi wa zinaa, n.k.
Rejea Qur’an (33:59)

ii. Wanawake kulingana na umbile lao na jukumu lao la kuzaa na kulea, wana haki ya kulindwa heshima yao na kuhifadhiwa majumbani.
Rejea Qur’an (33:33)



iii. Wanaume kuwa viongozi wa wanawake, si kuwa wao ni bora kuliko wanawake, bali wanaume wana kuwa ni walinzi, wahifadhi na viongozi wao.


iv. Kutokana na fursa ya vipaji na vipawa alivyonavyo mwanaume juu ya mwanamke, analazimika kusimamia na kuongoza majukumu mengi zaidi.

v. Kulingana na asili ya maumbile, wanawake hawawezi kuwa sawa kikazi, kimajukumu, kimavazi, kimahusiano, n.k.
Rejea Qur’an (33:36), (24:31), (24:60)



Haki za Mwanamke Katika Uislamu

i. Haki ya mwanamke kupata elimu

- Kujielimisha ni amri kwa wanaume na wanawake, sio wanaume pekee.

Rejea Qur’an (96:1-5)



ii. Haki ya mwanamke katika sitara

- Ni haki kwa mwanamke kupata kulingana na asili ya maumbile yake.

Rejea Qur’an (33:59), (24:31)



iii. Haki ya mwanamke katika uchumi

- Kama ilivyo kwa mwanamume ana haki ya kuchuma na kumiliki uchumi, mwanamke pia ana haki hiyo.
Rejea Qur’an (4:32), (4:4)



iv. Haki ya mwanamke katika jamii (ndoa, mirathi na talaka)

- Mwanamke ana haki ya kuolewa na mwanamume anayemridhia kwa kuzingatia sheria za Kiislamu kwa hiari.

- Mwanamke ana haki ya kumuacha mume atakayeshindwa kuishi naye na kufikia lengo la ndoa. Mfano talaka ya I’laa, Khul’u, Mubaarat, n.k.


- Haki ya mwanamke mjane au aliyeachwa kuolewa tena na wanaume wanaowapenda kisheria.


- Mwanamke ana haki na fungu la kurithi kama alivyo mwanamume pindi mmoja wapo atakapokufa.
Rejea Qur’an (4:7)



v. Haki ya mwanamke katika sheria

- Mwanamume na mwanamke wana haki sawa mbele ya sheria katika kuhukumiwa, kuadhibiwa, kudai haki, n.k. bila ya ubaguzi wowote.
Rejea Qur’an (5:38), (24:2)



- Mwanamke kama mwanamume, ana haki ya kutoa ushahidi mahakamani pale inapobidi.
Rejea Qur’an (2:282)



vi. Haki ya mwanamke kushiriki katika uongozi na siasa

- Jukumu la kuendesha maisha ya jamii liko kwa mwanamume na mwanamke katika kuamrisha mema na kukataza mabaya.


- Suala la uongozi wa kifamilia na kijamii ni la wote, mwanamume na mwanamke isipokuwa mwanamke haruhusiwi kuwa kiongozi wa nchi.
Rejea Qur’an (9:71), (58:1-4)



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 278


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga
Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga. Soma Zaidi...

Hijjah
Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Hadhi na Haki za Mwanamke Ulaya chini ya kanisa hapo zamani
Soma Zaidi...

Mifumo ya benk na uchumi wa kiislamu
7. Soma Zaidi...

chimbuko la sheria katika uislamu, hukumu za sheria na kuyatambua yaliyo halali na haramu
Soma Zaidi...

Shahada nguzo ya kwanza ya uislamu, sifa zake na umuhimu wake.
Soma Zaidi...

Jinsi ya kufanya suluhu kati ya mume na mke.
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kufanya suluhu katika ndoa. Soma Zaidi...

Faida za kuswali swala za sunnah
Posti hii inakwenda kukufundisha kuhush swala za sunnah. Soma Zaidi...

Umuhimu wa swala yaani kuswali kwa mwanadamu
Kwa nini ni muhimu kuswali? Post hii itakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kusimamisha swala. Soma Zaidi...

Jinsi ambavyo msafiri anatakiwa aswali akiwa safarini
Postvhiibinakwenda kukufundisha kuhusu swala ya msafiri na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

Zaka ni nini? Nini maana ya zaka katika uislamu
Zaka, kilugha ni kukua; kubariki na kuzidi kheri. Soma Zaidi...

Kutoa vilivyo halali
Nguzo za uislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...