Post hii itakujuza jinsi ya kiswali swala ya tahajudi. Pia utajifunza jinsi ya kuswali swala za usikubyaanibqiyamublayl
4. Swala ya Tahajjud
Swala ya Tahajjud ni miongoni mwa swala zilizokokotezwa sana katika Qur-an na Hadithi. Neno “Tahajud” lina maana ya kuamka kutoka usingizini. Swala hii huswaliwa usiku wa manane, hasa katika theluthi ya mwisho wa usiku karibu na al-Fajiri.
Swala hii vile vile hujulikana kwa jina la “Qiyaamul-layl”. Yaani kisimamo cha usiku kwa sababu inakuwa na visimamo virefu ambapo Qur-an husomwa kwa urefu. Mkokotezo wa swala ya Tahajjud unadhihirika katika aya za Qur-an zifuatazo:
Na katika usiku jiondoshee usingizi (kid ogo) kwa (kusoma) hiyo (Qur-an ndani ya Swala).Hiyo ni (Ibada) zaidi kwako. Huwenda Mola wako akakuinua cheo kinachosifika. (17:79).
Miongoni mwa sifa za waja wema wa Allah (s.w) ni pamoja:
“Na wale wanaopitisha baadhi ya saa za usiku kwa ajili ya Mola wao kwa kusujudu na kusimama ”. (25:64).
J e , afanyaye ibada nyakati za usiku kwa kusujudu na kusimama na kuogopa Akhera na kutarajia rehema ya Mola wake (ni sawa na asiyefanya hayo)? Sema: “Je, wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?” Wanaotanabahi ni wale wenye akili tu. (39:9)
Pia Mtume (s.a.w) amekokoteza Swala za Usiku kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo.
Abu Umamah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Jizoesheni kusimama Usiku (kwa swala) kwa sababu ilikuwa ndio tabia ya Wacha-Mungu w aliokutangulieni na ni njia ya kukukurubisheni karibu na Mola wenu na ni njia ya kufutiwa dhambi na ni kizuizi cha kutenda maovu (dhambi)”. (Tirmidh).
Idadi ya rakaa alizoswali Mtume (s.a.w) katika hii swala ya Tahajjudi ni nane (8) na kisha akamalizia na rakaa tatu za Witri. Katika hizi rakaa nane alitoa salam kila baada ya rakaa mbili. Mtume (s.a.w) alikuwa akisoma Qur-an kwa kitambo kirefu kwa kila rakaa kiasi kwamba miguu yake ilikuwa inavimba kama tunavyojifunza katika Hadithi ifuatayo:-
“Mughirah (r.a) ameeleza kuwa Mtume (s.a.w) alikuwa akisimama katika (sw ala ya usiku) kwa kitambo kirefu kiasi kw amba miguu yake ilivimba, akaulizwa: Kwanini unafanya hivi ambapo umesamehewa dhambi zako zilizotangulia na zitakazokuja? Akauliza: “Nisiwe mja mwenye Shukrani?” (Bukhari na Muslim).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Ili swala itimie utahitajika kutimiza nguzo zake na masharti yake. Hapa utajifunza nguzo 17 za swala.
Soma Zaidi...KuzuilianaTumeona kuwa wanaume wenye kurithi ni 15 na wanawake wanaorithi ni 10.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha njia zinazotumika kujitwaharisha.
Soma Zaidi...Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Post hii itakufundisha kuhusu swala ya maiti, nguzo za swala ya maiti, sharti za swwla ya maiti na jinsi ya kuiswali.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha sunnah 9 za swala. Sunnah hizi ni zile ambazo ukiziwacha swala yako haibatiliki.
Soma Zaidi...Je unaijuwa mipaka yako katika kumiliki mali. Ama unajuwa haki zako katika mali inayomiliki. Endelea na somo
Soma Zaidi...Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...