Jinsi ya kiswali swala ya tahajud na swala za usiku yaani qiyamu layl

Post hii itakujuza jinsi ya kiswali swala ya tahajudi. Pia utajifunza jinsi ya kuswali swala za usikubyaanibqiyamublayl

4. Swala ya Tahajjud

Swala ya Tahajjud ni miongoni mwa swala zilizokokotezwa sana katika Qur-an na Hadithi. Neno “Tahajud” lina maana ya kuamka kutoka usingizini. Swala hii huswaliwa usiku wa manane, hasa katika theluthi ya mwisho wa usiku karibu na al-Fajiri.

 


Swala hii vile vile hujulikana kwa jina la “Qiyaamul-layl”. Yaani kisimamo cha usiku kwa sababu inakuwa na visimamo virefu ambapo Qur-an husomwa kwa urefu. Mkokotezo wa swala ya Tahajjud unadhihirika katika aya za Qur-an zifuatazo:

 

Na katika usiku jiondoshee usingizi (kid ogo) kwa (kusoma) hiyo (Qur-an ndani ya Swala).Hiyo ni (Ibada) zaidi kwako. Huwenda Mola wako akakuinua cheo kinachosifika. (17:79).

 


Miongoni mwa sifa za waja wema wa Allah (s.w) ni pamoja:

 

“Na wale wanaopitisha baadhi ya saa za usiku kwa ajili ya Mola wao kwa kusujudu na kusimama ”. (25:64).
J e , afanyaye ibada nyakati za usiku kwa kusujudu na kusimama na kuogopa Akhera na kutarajia rehema ya Mola wake (ni sawa na asiyefanya hayo)? Sema: “Je, wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?” Wanaotanabahi ni wale wenye akili tu. (39:9)

 

Pia Mtume (s.a.w) amekokoteza Swala za Usiku kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo.

 


Abu Umamah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Jizoesheni kusimama Usiku (kwa swala) kwa sababu ilikuwa ndio tabia ya Wacha-Mungu w aliokutangulieni na ni njia ya kukukurubisheni karibu na Mola wenu na ni njia ya kufutiwa dhambi na ni kizuizi cha kutenda maovu (dhambi)”. (Tirmidh).

 


Idadi ya rakaa alizoswali Mtume (s.a.w) katika hii swala ya Tahajjudi ni nane (8) na kisha akamalizia na rakaa tatu za Witri. Katika hizi rakaa nane alitoa salam kila baada ya rakaa mbili. Mtume (s.a.w) alikuwa akisoma Qur-an kwa kitambo kirefu kwa kila rakaa kiasi kwamba miguu yake ilikuwa inavimba kama tunavyojifunza katika Hadithi ifuatayo:-

 


“Mughirah (r.a) ameeleza kuwa Mtume (s.a.w) alikuwa akisimama katika (sw ala ya usiku) kwa kitambo kirefu kiasi kw amba miguu yake ilivimba, akaulizwa: Kwanini unafanya hivi ambapo umesamehewa dhambi zako zilizotangulia na zitakazokuja? Akauliza: “Nisiwe mja mwenye Shukrani?” (Bukhari na Muslim).

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 5915

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 web hosting   

Post zinazofanana:

Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga

Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.

Soma Zaidi...
sunnah za swala

Sunnah za SwalaSunnah za Swala Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutwaharisha aina mbalimbali za najisi

Kila najisi ina namna yake ya kutwaharisha, hata hivyo namna hizo hufanana. Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutwaharisha najisi mbalimbali.

Soma Zaidi...
Maswali juu ya haki na uadilifu katika uislamu

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3:Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda

Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi

Soma Zaidi...
Aina mbili za talaka zisizo na rejea katika uislamu

Huwezi kuruhusiwa kumrejea mke endapo utamuacha kwa talaka hizi mbili.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuswali kuswali swala ya maiti

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya maiti, nguzo za swala ya maiti, sharti za swwla ya maiti na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...
Wafundisheni kuswali watoto wenu

Mtume amemfundisha kuwa watoto wafundishwe kuswali wakiwa na miaka saba na waadhibiwe wakiacha wakiwa na miaka 10

Soma Zaidi...