Umuhimu wa swala

Umuhimu wa KusimamishaSwala Kwa mujibu wa Hadith ya Ibn Umar (r.

Umuhimu wa swala

Umuhimu wa Kusimamisha
Swala Kwa mujibu wa Hadith ya Ibn Umar (r.a) tuliyoirejea mwanzoni, kusimamisha swala ni nguzo ya pili ya nguzo za Uislamu. Katika kuonyesha umuhimu wa kusimamisha nguzo hii Mtume (s.a.w) amesema: Swala ndio nguzo kubwa ya Dini (Uislamu) mwenye kusimamisha swala amesimamisha dini (Uislamu) na mwenye kuiacha swala amevunja Dini .(Uislamu)

Katika Hadithi nyingine, amesimulia Jabir (r.a) kuwa Mtume wa Allah amesema: Tofauti yetu sisi (Waislamu) na ukafiri ni kuacha swalah. (Muslim) Pia Mtume (s.a.w) amesema: Tofauti iliyopo kati yetu (Waislamu) na wengine (wasiokuwa Waislamu) ni swala (Ahmad, Abu Daud, An-Nasai, Tirmidh)

Kutokana na hadithi hizi, tunajifunza kuwa mtu ambaye hasimamishi swala, hatakama anajiita Muislamu si Muislamu bali ni kafiri kama makafiri wengine. Anakuwa kafiri kwa sababu amekanusha amri ya Allah iliyowazi kama inavyobainika katika aya zifuatazo: Waambie waja wangu walioamini, wasimamishe swala.(14:31)  Basi simamisheni swala, kwa hakika swala kwa waumini ni faradhi iliyowekewa nyakati makhsusi. (4:103) Na waamrishe watu wako kuswali (kusimamisha swala) na uendelee mwenyewe kwa hayo... (20:132).

Tukumbuke kuwa hawi Muumini yule anayekuwa na hiari katika kutekeleza amri ya Allah na Mtume wake kama tunavyokumbushwa katika aya ifuatayo: Haiwi kwa mwanamume aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapokata shauri, wawe na hiari katika shauri lao. Na mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amepotea upotofu ulio wazi. (33:36).


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Jiunge nasi WhatsApp
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2302

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Umuhimu na nafasi za hijjah katika uislamu

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Taasisi za Kifedha Katika Mfumo wa Uchumi wa Kiislamu

- Ni taasisi za kifedha zinazohusika na kuhifadhi akiba na mali za watu zenye thamani kubwa kama dhahabu, n.

Soma Zaidi...
Nguzo za udhu ni sita

Post hii itakufundisha kuhusu nguzo kuu sita za udhu.

Soma Zaidi...
Kutoa zakat

Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maana ya hadathi na aina zake

Post hii inakwenda kukugundisha maana ya hadathi pamoja na kutaja aina za hadathi

Soma Zaidi...