Siku za kupata mimba

Siku za kupata mimba

Nitakujulisha siku ya kupata mimba na sifa zake, na namna ya kuweza kuitafuta

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Siku za kupata mimba

SIKU ZA KUPATA MIMBA
Kwa wale wanaohangaika kutafuta ujauzito makala hii ni kwa ajili yako. Hapa nitakwenda kukujuza siku yako mujarabu ambayo utatapa ujauzito. Pia nitakujuza sifa za siku za kupata mimba. Unajuwa wanawake wanatofautiana sana katika mifumo yao ya uzazi, simaanishi maumbile, namaanisha hali zao. Watu wengi wanaelewa kuwa mwanamke anaweza kupata mimba siku zote. Hapa hii sio sahihi kabisa. Ukweli ni kuwa kuna siku maalumu na ni chache. Kitaalamu siku hizi hufahamika kama faertile window.



Siku ya kupata ujauzito utaweza kuijuwa kwanza kuangalia mambo kadhaa nitakayoyatajahapo chini. Kabla ya kuyajuwa mabo hayo haklikisha kuwa unakula lishe bora na inayoshawishi kutafuta mtoto kweli kama unatafuta mtoto. Kwa wanaume wale vyakula vya kuongeza mbegu za kiume kama karangga, korosho, kunywa maji mengi na vyakula vingine, wasiliana nasi hapo chini nikueleze. Pia hakikisha wewe na mwenza mnakula vyakula vya kuongeza hamu ya tendo lando kwaingi. Hakikisha mwili ni msafi na kila mmoja amejiandaa vyema kumpokea mwenza. Sasa nakwenda kukufundisha siku za kupata mimba.



1.Kutambuwa siku za kupata mimba kwa mahesabu.
Kwanza hakikisha unaujuwa tarehe yako ukiwa ni mwanmke, na kama ni mwanaume itambuwe vyema tarehe ya mwenzio. Tambua byema mzunguruko wake wa hedhi unakwenda siku ngapi. Ukitambua vitu hivyo sasa twende pamoja. Wataalamu wanaeleza kuwa mwaname anaweza kubeba mimba siku 12 mpaka 14 kabla ya kuingia hedhi yake. Pia wataalamu wanatueleza kuwa yai la mbegu ya mwanaume inaweza kuwa hai ndani ya siku tatu mbaka 5 na yai la mwanamke linaweza kukaa masaa 12 mpaka 24 . ila sanasana ni siku 3, yaani mbegu iliyoingia leo inaweza kurutubisha yai siku tatu zijazo. Hivyo tyujaalie mwaname ana mrunguruko wa hedhi wa siku 28. tutafanya hivi:-



Mfano wa kwanza mwenye siku 28
A.28 - 12 = 16 (ongeza moja iwe 17, kufidia yai la mama)
B.16 - 02 = 14
C.14 - 3 = 11 (tunapunguza 3 nyuma kufidia mbegu ya maba)
Hivyo mwanamke huyu siku zake za kupata mimba ni kati ya siku ya 11 mpaka 17 toka siku ya kwanza aingie hedhi.



Mfano wa pili mwenye siku 35
A.35 - 12 = 23 (ongeza 1 iwe 24)
B.23 - 02 = 21
C.21 - 03 = 18
Hivyo mwenye mzunguruko wa siki 35 siku zake hatari kupata mimba ni kati ya siku ya 18 mpaka 24 toka siku ya kwanza kuona hedhi.



Mfano wa tatu mwenye siku 21
A.21 - 12 = 9 (ongeza 1 iwe 10)
B.9 - 2 = 7
C.7 - 3 = 4
Mwanamke huyu anaweza kubeba ujauzito punde tu baada ya kumaliza hedhi mpaka siku ya 10



Unaweza kutumia mifano hii kitafuta skuku yako ya kupata mimba. Wanawake wanatofautiana sana siku zao. Kuna ambao ni 21, kuna ambao ni 35. ila kwa hali ya kawaida siku za hedhi ni kati ya 21 mpaka 35. ikizidi hapo ama kuwa chini ya hapo kutakuwa na shida kwenye mfumo wa homoni. Kama upo katika kutafuta ujauzito hakikisha unashiriki ngono katika siku zote hizo ama unaweza kuruka ruka ila hakikisha unaanza na siku ya kwanza, kisha unaweza kuacha moja na kushiriki inayofata.



2.Sifa za siku za kupata mimba.
Baada ya kujuwa kuitafuta siku ya kupata mimba sasa napenda ujuwe ssifa za siku hiyo. Sasa hata kama unaijuwa kwa mahesabu ukweli ni kuwa unaweza pia kuikosa kwani sio maalumu. Sasa hapa nitakurahisishia kazi kwa kukutajia sifa za siku hizo za kupata mimba.



1.Siku ya kupata mimba ina sifa hii, kwanza joto la mwili linakuwa kubwa tofauti na siku zilizotangulia na siku zijazo. Tambuwa kuwa hapa mwili utakuwa na joto ila haliusiani na ugionjwa wowote ama mambo mengine. Kwa mfano kuchelewa kulala, misongo ya mawazo maradhi na homa kwa pamoja hupelekea joto la mwili kupata. Joto tunalolizungumzia hapa halisababishwi na sababu yeyeote katika hizi.



2.Uteute wa ukeni utakuwa mwingi kulinganisha na siku zilizopita. Uteute huu husaidia kati akuzisafirisha mbegu za kiume kwenda kutungisha mimba. Uteute kuu ni mlaini na unateleza sana. Mwanamke anaweza kuuiona baada ya kuingiza kidole ndani sana kwenye shingo ya uzazi.



3.Siku hii mwanamke atakuwa na hamu sana ya kushiriki tendo la ndoa kuliko siku zilizopita. Hii ni kutokana na miamsho iliyosababishwa na homoni ambazo zinaandaa mwili kwa ajili ya ujauzito.



Sifa hizi huweza kupotea baada ya kupata ujauzito ama muda wa kubeba mimba ukiisha. Mabadiliko hayo pia huweza kuathiriwa na mabo mengine kama matumizi ya uzazi wa mpango hasa wa kutumia sindano. Je utakuwa na maoni, maswali ama mapendekezo?. wasiliana nasi kwa hapo chini





                   



Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 2423

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Imani potofu kuhusu uzazi wa mpango
Imani potofu kuhusu uzazi wa mpango

Post hii inahusu zaidi imani potofu kuhusu uzazi wa mpango, ni imani walizonazo Watu kuhusu matumizi ya uzazi wa mpango.

Soma Zaidi...
Kwa mjamzito kuumia wakati wa tendo la ndoa tatizo linaweza kuwa ni nini?
Kwa mjamzito kuumia wakati wa tendo la ndoa tatizo linaweza kuwa ni nini?

Je unaweza kunielezaKwa mjamzito kuumia wakati wa tendo la ndoa tatizo linaweza kuwa ni nini?

Soma Zaidi...
 Mambo ya kuzingatia kwa mama ili apate huduma endelevu.
Mambo ya kuzingatia kwa mama ili apate huduma endelevu.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na huduma kwa mama wajawazito na waliojifungua.

Soma Zaidi...
Nikila tumbo linauma, mdomo mchungu, matiti yanauma na hedhi sijapata, je ni dalili za mimba?
Nikila tumbo linauma, mdomo mchungu, matiti yanauma na hedhi sijapata, je ni dalili za mimba?

Mdomo kuwa mchungu ni halia mabayo haiashirii ishara mbaya za kiafya. Mdomo unaweza kuwa mchungu kutokana na vyakula. Pia hutokea ikawa ni ishara ya baadhi ya maradhi, ama ni matokeo ya baadhi ya shda za kiafya. Je vipi kuhusu maumivu ya matiti na tumb?

Soma Zaidi...
SABABU ZA KUKOSA NGUVU ZA KIUME AMA KUWA NA UWEZO MDOGO WA KUHIMILI TENDO LA NDOA
SABABU ZA KUKOSA NGUVU ZA KIUME AMA KUWA NA UWEZO MDOGO WA KUHIMILI TENDO LA NDOA

Hii ni hali inayowapata wanaume kushindwa kuhimili tendo la ndoa.

Soma Zaidi...
Kiwango cha juu cha Androgen
Kiwango cha juu cha Androgen

Posti hii inahusu zaidi homoni ya androgen, ni homoni ambayo imo kwa wanaume na ikizidi kwa kiwango chake inaweza kuleta shida kwenye mwili wa binadamu kwa hiyo homoni hii inaweza kuleta shida iwapo ikiongezeka kwa kiasi kikubwa.

Soma Zaidi...
Dalili za kujifungua hatua kwa hatua
Dalili za kujifungua hatua kwa hatua

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za kujifungua hatua kwa hatua

Soma Zaidi...
Sababu za kutokea kwa saratani ya matiti
Sababu za kutokea kwa saratani ya matiti

Saratani ya matiti ji moja kati ya saratani zinazosumbuwa wqnawake wengi. Katika somo hili utajifunza chanzo cha kutokea saratani ya matiti

Soma Zaidi...