KUVIMBA VYA MIGUU KWA WAJAWAZITO Kuvimba kwa miguu ni hali inayowapara wengi katika wajawazito.
KUVIMBA VYA MIGUU KWA WAJAWAZITO
Kuvimba kwa miguu ni hali inayowapara wengi katika wajawazito. Kitaalamu hali hii hutambulika kama odema. Wakati mwingine si miguu tu ndio huvimba bali mikono, nyayo na uso huweza kuvimba. Ijapouwa huku kukuvimba kwa ghafla kwa uso na mikono ni dalili ya maradhi mengine kama preeclampsia.
Hali hii ya kuvimba kwa miguu huweza kuwapata wanawake katika kipindi chote cha ujauzito, iwe wajauzito ulio mchanga, ama kipindi cha katikati cha ujauzito ama kipindi cha mwisho cha ujauzito. Katika hali ya kawaida kuvimba kwa miguu kwa wajawazito sio jambo la kusumbua kiafya yaani kusema kuwa ni tatizo kubwa. Hapana hii ni kawaida kwa wajawazito.
Kuvimba huku kunaweza kuwa ni tatiko kama kutaweza kuambatana na baadhi ya matatizo mengine ya kiafya kama maumivu makali ya kicha, kizunguzungu, kutokwa na damu, kushinwa kuona kwa usahihi ama kushinwa kupumua ama kupumua kwa taabu, hali hizi kuweza kuashiria hatari. Ni vyema mjamzito awahi kituo cha afya kama ana hali hizi.
Sababu za kutokea kwa vimbe hizi ni mabadiliko ya mwilini yanayopatikana wakati wa ujauzito. Kuongezeka kwa damu mwilini na kuongezeka kwa mapigo ya moyo huweza kuchangia zaidi hali hii. Halikadhalika ongezeko la homoni maalumu zinazotolewa wakati wa ujauzito. Haya yote kwa pamoja huchangia kutokea hali hizi za kuvimba.
Tofauti na sababu hizi pia zipo nyingine kama mabadiliko ya hali ya hewa. Hapa tunazungumzia joto, ambalo pia ni sababu ya kuvimba. Sababu nyingine ni kutokunywa maji ya kutosha, matatizo ya homoni yaani homone imbalance. Kukaachini kwa muda mrefu ukaaji wa kukalia miguu. Ama kusimama kwa muda mefu.
Kupunguza ama kuepuka hali hii ni vyema kufanya mazoezi ya mara kwa mara, kukaa kivulini, kulalia upande kwa kushoto unapolala. Hakikisha unakula mlo kamili, hakikisha kuwa unakunywa maji ya kutoka kwa siku. Na hata ukizidisha ni faida kwako. Epuka kusimama kwa muda mrefu ama kukaa kwa kukalia mguu. Epuka kukaa kwa muda mrefu kwa staili moja. Kuna matatizo mengu ya kiafya yanayoambatana na ujauzito, ni vyema mjamzito akiwa makini.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Miongoni mwa matunda yenye virutubisho vingi ni pamoja na papai, nanasi, tikiti, palachichi, pera, karoti, hindi na boga. Lakini katika matunda haya yapo ambayo kwa mimba changa anatakiwa awe makini, kama papai na nanasi. Sasa vipi kuhusu mimba ya
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi upungufu wa homoni ya estrogen na dalili zake, aina hii ya homoni ikipungua mwilini uleta madhara na matatizo mbalimbali kwenye mwili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa, kwa kawaida tunajua kwamba mtoto wakati wa kuzaliwa ni lazima atangulize kichwa ila Kuna kipindi mtoto anatanguliza matako, kuna aina nne za mtoto kutanguliza matako.
Soma Zaidi...Majimaji msule sehemu za siriyanaweza kuashiria mambo mengi ka mwanamke. Ikiwemo ujauzitina maradhi. Pia yanaweza kuashiria kuwa mwanamke unaweza kuoatavujauzito amalaa.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito, ni ugonjwa unaowapata sana akina mama wajawazito na uisha tu pale Mama anapojifungua kwa hiyo tunapaswa kujua wazi sababu za ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa mama, zoezi hili ufanyika kila mwezi pale mama anapokuja kwenye mahudhurio kwa kufanya hivyo tunaweza kuja maendeleo ya mtoto kwa kila mwezi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa akina Mama, tunajua wazi kubwa kuna faida kubwa za uzazi wa mpango kwa akina Mama pindi watumiapo njia hizi kwa uhakika zaidi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya kuharibika kwa mimba kuanzia miezi zero mpaka miezi mitatu, kwa sababu hii ni miezi ya kwanza kabisa Kuna sababu au vyanzo vya kuharibika kwa mimba katika kipindi hiki.
Soma Zaidi...Makala hii itakwenda kukufundisha dalili za kujifunguwa, hatuwa za kujifunguwa na kuzalisha, pia utajifunza mabo muhimu kabla na wakatii wa kujifungua.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa watu waliopata maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi, ni faida wanazozipata waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi.
Soma Zaidi...