image

Kiungulia kwa wajawazito, dawa yake na njia za kukabilianannacho

Wajawazito wamekuwa wakisumbuliwa sana na kiungulia, makala hii itakujulisha njia za kukabiliana na kiungulia, dalili zake na dawa zake

Kiungulia kwa wajawazito, dawa yake na njia za kukabilianannacho

Dawa ya kiungulia kwa wajawazito.
Kiungulia ni moka katika matatizo yanayotokea katika mfumo wa chakula. Kiungulia si katika mambo ya hatari, ila huwa ni hali sumbufu sana hasahasa kwa wajawazito. Kama na wewe unasumbuliwa sana na kiungulia makala hii ni kwa ajili yako. Hapa tutaoa sababu za kiungulia, matibabu yake na njia za kuepuka kiungulia.



Nini husababisha kiungulia cha mara kwa mara kwa wajawazito?
1.Ni kuwa wakati wa ujauzito kuna mabadiliko mengi ya homoni yanatokea kwa mwanamke. Mabadiliko haya yanapelekea misuli ya kooni inayounganisha tumbo na koo, kujiachia mara kwa mara na hivyo kusababisha tindikali iliyopo tumboni kupanda juu, na kusababisha kiungulia. Hali hii huweza ktokea sana pale unapolala baada ya kula chakula kingi.



2.Kadiri mtoto anavyoendelea kukuwa na mimba inavyosonga mbele ndivyo mtoto anaongeza mkandamizo kwenye tumbo. Hali hii inapelekea tindikali iliyopo tundoni kusukumwa kupanda juu na hatimaye kusababisha kiungulia.



Je ujauzito unasababisha kiungulia?
Hapana, ujauzito hausababishi kiungulia ila unaongeza uwezekano wa kupata kiungulia. Kivipi?, ni hivi mwanzoni mwa ujauzito koo lako linachukuwa chakula kidogokidogo, na kwa kuwa kuna mabadiliko mengi yanatokea husababisha mmeng’enyo wa chakula kufanya kazi kidogokidogo hivyo kuchelewa kukimeng’enya chakula kwa haraka. Hali hii husaidia mwali kupata muda wa kutosha kufyonza chakula na kukipeleka kwa mtoto, ila kwa upande mwingine hali hii husababisha kiungulia.



Hata hivyo si kila mjamzito atakuwa anasumbuliwa na kiungulia, ni kwa sababu kuna mambo mengi yanafngamanna na kiungulia. Hali namna ambavyo mjamzito anaishi inaweza kuchangia kupata kiungulia. Namna mtu alivyo, vyakula anavyokula, namna anavyolala na hata mavazi pia yanaweza kuchangia kupata kiungulia.



Mjamzito afanye nini kuepuka kiungulia?
1.Kla kidogo kidogo mara kwa mara na hakikisha hunywi maji wakati wa kula
2.Kula kidogo na hakikisha unatafuna kila tonge kwa ufanisi zaidi
3.Wacha kula unapokaribia kulala
4.Punguza kula vyakula kama chokoleti, vyenye mafuta mengi, vyenye pilipili na vyenye uchachu
5.Usilale baada ya kula angalau unaweza kusimama ama kutembea.
6.Wacha kuvaa nguo za kubana sana
7.Unapolala hakikisha kichwa chako kinakuwa juu, unaweza kutumia mto ama mfano wake
8.Unapolala lalia ubavu wa kushoto
9.Tafuna bigji zisizo na sukari baada ya kula
10.Kunywa maziwa kama unayo unapohisi kiungulia
11.Kunywa asali kama unayo unapohisi kiungulia.



Dawa za kutibu kiungulia
Unaweza kutibu kiungulia kwa kutumia antacid kama vile Tums, Rolaids na Maalox.dawa ambazo zimetengenezwa kwa madini ya calcium carbonate au magnesium ni nzuri pia. Magnesium si nzuri kama ujauzito upo mwishoni.



Madaktari wengi wanakataza matumizi ya antacid ambazo zimechanganywa na sodium, ama zila lebo ya aluminium carbonate kwani zinawza kupelekea kukosa choo. Pia dawa hizi za kiungulia zinakatazwa kwa wajawazito Alka-Seltzer.





                   







           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 3015


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Dalili za ongezeko la homoni ya estrogen
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo mtu anaweza kupata ikiwa homoni ya estrogen imeongezeka, hizi dalili zikitokea mama anapaswa kuwahi hospital ili kuweza kupata matibabu au ushauri zaidi. Soma Zaidi...

Je dalili ya kuuma tumbo huanza baada ya wiki ngapi Toka mwanamke apate ujauzito?
Maumivu ya tumbo ni moja katika dalili za ujauzito. Maumivu wanawake wengi hushindwa kujuwa kuwa ni ujauzito ama laa. Na hii ni kwa sababu kwa wanawake wengi maumivu ya tumbo ama changu ni jalivya kawaida kwao. Soma Zaidi...

Dalili ambazo mwanamke hapaswi kufumbia macho
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo mwanamke hapaswi kufumbia macho. Soma Zaidi...

SABABU ZA KUKOSA HAMU YA TENDO LANDOA
Hii ni hali inayompata mtu kukosa hamu kabisa ya kushiriki kitendo chochote kinachohusiana na kufanya tendo landoa au bunyeto. Soma Zaidi...

UTI na ujauzito
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa UTI kwa wajawazito Soma Zaidi...

Ni vipi nitagundua kuwa nina ujauzito?
Hali ya ujauzito huanza kutabirika Mara tu ya kujamiana, pia chemikali (hormon) za mwili huanza mchakato wa kuongeza na kupunguza utendaji kazi wa kemikali hizo mfano.follical stimulating hormon (FSH) na lutenazing hormon kuivisha yai tayari kwa kutengen Soma Zaidi...

Mwezi juzi niliingia tarhe 21 ila mwez uloisha nmeingia tarh 25 maana mzunguko wangu umekuwa mrefu nikahs naujauzito kumbe mzunguko umebadilika hapo tatz n nn
Posti hii utakwenda kutoa sababu kuu za kuvurugika kwa mzunguko wa hedhi. Kama na wewe numiongini mwaka endelea kusoma Soma Zaidi...

Faida na hasara za Kufunga kizazi kwa wanawake.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Kufunga kizazi kwa wanawake. Soma Zaidi...

Je matiti kujaa na chuchu kuuma inakua ni dalili za hedhi?
Kuunda na kujaa kwa matiti ni miongoni mwa dalili za ujauzito lakini pia ni dalili za kukaribia hedhi kwa baadhi ya wanawake. Posti hii itakwenda kufafanuabutofauti wa dalili hizi na kipi ni sahihibkatibya hedhi ama ujauzito. Soma Zaidi...

Sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa.
Post hii inahusu zaidi sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, kuna wakati mtoto anapozaliwa anaweza kuvunjika kwenye sehemu mbalimbali kwa sababu zifuatazo. Soma Zaidi...

Namna ya kumpima mtoto uzito
Posti hii inahusu namna ya kumpima mtoto uzito, ni njia ambayo utumika kujua uzito wake na maendeleo ya mtoto. Soma Zaidi...

Dawa ya chango na dawa maumivu ya tumbo la hedhi
Nitakujiza dawa ya chango na maumivu ya tumbo lahedhi, dalili zake na njia za kukabiliana na maumivu ya tumbo la chango. Soma Zaidi...