Zijuwe Dalili za minyoo na dalili kuu 9 za minyoo

Utajifunza dalili za minyoo, sababu za minyoo na namna ya kujiepusha na minyoo. Dalili kuu 5 za minyoo mwilini

Zijuwe Dalili za minyoo na dalili kuu 9 za minyoo

Dalili za minyoo, sababu zake na kuiepuka minyoo.



Minyoo ni katika wadudu vimelea vinavyowapa shida watu wengi leo hii. Minyoo sio virusi wala bakteria kama ambavyo watu wengi wamekuwa wakidhania.minyoo ipo katika makundi meengi na huishi katika maeneo mbalimbali kwenye miili yetu ikiwemo tumbo, ini, utumbo, ubongo na kwenye damu na maeneo mengine. Dalili za minyoo hutofautiana sana kulingana na aina ya minyoo na wapi ipo. Lakini zipo dalili zenye kufanana kwa minyoo wote. Katika makala hii nitakwenda kukujuza baadhi ya dalili za minyoo katika mwili wako, pia tutaona sababu za kupata minyoo, wapi minyoo inapatikana na vipi tutaizuia:-


Utaweza kupata minyoo katika hali zifuatazo:-
1.kula kitu kisichooshwa kwema kwa maji yaliyo safi na salama
2.Kunywa maji ambayo si masafi na si salama
3.Kula nyama ambayo haikuiva vyema, ama nyama mbichi
4.Kutembea pekupeku kwenye ardhi yeye minyoo
5.Kula udongo,
6.Kinyesi cha wanyama na binadamu



DALILI ZA MINYOO
Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote. Na dalili za minyoo pia hutofautiana sana, kulingana na aina za minyoo. Lakini zifuatazo ni katika dalili kuu:-
1.Kichefuchefu
2.Kukosa hamu ya kula
3.Maumivu ya tumbo
4.Kupungua uzito
5.Uchovu wa viungo
6.Kuona utelezi mwingi kama kamasi kwenye kinyesi
7.Kuona minyoo kwenye kinyesi.
8.Kuona damu kwenye kinyesi
9.Tumbo kujaa


Dalili hizi kama nilivyotangulia kusema kuwa zinatofautiana kulingana na aina ya minyoo. Sasa hebu tuone kwa ufupi dalili hizi kulingana na aina ya minyoo:-


1.minyoo aina na tapeworm dalili zao ni:
A.Kuvimba kwa ngozi ama kujaa ama kujaa kwa tumbo
B.Kuwa na alegi
C.Kuwa na homa
D.Matatizo katika mfumo wa fahamu, kama kifafa


2.minyoo aina ya hookworm dalili zao ni kama:-
A.Kuwashwa
B.Kupata ugonjwa wa anaemia (upungufu wa seli hai nyekundu kwenye damu) hivyo kukosa oksijeni ya kutosha mwilini
C.Kuwa na uchovu wa hali ya juu.


3.minyoo aina ya trichinosis, minyoo hawa wana dalili kama:-
A.Kupata homa
B.Kuvimba kwa uso
C.Maumivu ya misuli na kuchoka
D.Maumivu ya kichwa
E.Kutokupenda kupigwa na mwanga
F.Matatizo katika macho (conjuctivist)



NJIA ZA KUKABILIANA NA MINYOO
Kwa kuwa tumekwisha kuona namna ambavyo minyoo huenezwa, hivyo basi ni rahisi sasa kutaja namna ya kubambana na minyoo. Njia hizo ni kama :-


1.usile chakula, nyama ana samaki ambaye hajapikwa vyema, ama kula nyama mbichi ama isiyoiva


2.Epuka kugusagusa nyama unapoandaa chakula chako, tenganisha nyama kivyake na vyakula vingine wakati unapoandaa kupika.


3.Safisha vyema vyembo ambavyo vimegusa nyama ambayo haikupikwa


4.Usile mimea ambayo inaishi ndani ya maji yabaridi


5.Usitembee miguu wazi kwenye maeneo machafu ambayo yana kinyesi


6.Safisha vyema kinyesi cha wanyama.


7.Hakikisha unapika vizuri nyama mpaka uhakikishe imewiva vyema,


8.Wanya kung’ata kucha ama kunyonya vidole


9.Hakikisha unaosha kila unachokila kwa maji yaliyo safi na salama.


10.Usafi wa mwili, mavazi na mazingira ni muhimu kwa ajili ya kupambana na minyoo.


11.Kuwacha kabisa kula udongo




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 18290

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Dalili za uvimbe kwenye kizazi

Posti hii inahusu zaidi Dalili za uvimbe kwenye kizazi,hizi ni Dalili ambazo ujitokeza kwa akina mama ambao wana uvimbe kwenye kizazi kwa hiyo endapo mama ameona Dalili kama hizi anapaswa kuwahi hospitali mara moja kwa uangalizi zaidi.

Soma Zaidi...
Dalili za mimba ya watoto mapacha

Makala hii itakwenda kukupa dalili ambazo zinaonyesha kuwa mimba ni ya mapacha. Dalili hizi zitahitajika kuthibitishwa na kipimo cha daktari ili kujuwa kuwa ni kweli.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa uzazi wa mpango kwa Mama

Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa akina Mama, tunajua wazi kubwa kuna faida kubwa za uzazi wa mpango kwa akina Mama pindi watumiapo njia hizi kwa uhakika zaidi.

Soma Zaidi...
Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa?

Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa mpaka siku ya kujifungua Kama mume wake pamoja na yeye akiwa Hana maambukizi ya zinaa na Kama akiona dalili zozote zile za hatari ndio hataruhusiwa kushiriki tendo la ndoa.

Soma Zaidi...
Mimba huonekana katka mkojo baada ya muda gan tangu itungwe

Kipimo cha mimba kwa mkojo kimekuwa kikitumika sana kuangalia ujauzito. Kipimo hiki kinapotumika vibaya kinaweza kukupa majibu ya uongo. Kuwa makini na ujue muda sahihi.

Soma Zaidi...
Fahamu mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa

Posti hii inahusu zaidi mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa, kwa kawaida tunajua kwamba mtoto wakati wa kuzaliwa ni lazima atangulize kichwa ila Kuna kipindi mtoto anatanguliza matako, kuna aina nne za mtoto kutanguliza matako.

Soma Zaidi...
Unakuta siku imefka ya hedhi kabla haijaanza kutoka hedhi yanatoka maji meupe clean kabisa hii Ina naamisha nini?

Kutoka na majimaji ka uchache kwa mwanamke sio jambo lakishangaa sana. Damu hii inawezapiabkikbatana damu na maumivu makali.

Soma Zaidi...
Dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi.

Posti hii inahusu zaidi dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama ambaye anakuwa amepasuka mfuko wa kizazi.

Soma Zaidi...
Sababu za kutoona hedhi kwa wakati

Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa hedhi wakati mda wa kuona hedhi umefika ni tatizo linalowasumbua baadhi ya wasichana wachache katika jamii na hii ni kwa sababu zifuatazo.

Soma Zaidi...
Hivi kipimo cha mimba cha mkojo baada ya kutumika Mara 1 ,hakiruhusiw tena kutumika au

Je ni kweli kupima kimoja cha mloka kinaweza kupima mimba zaidi ya mara moka?

Soma Zaidi...