Mda wa kufanya tendo la ndoa baada ya kujifungua
Posti hii inahusu zaidi mda ambao mama anapaswa kukaa bila kufanya tendo la ndoa mara tu baada ya kujifungua.
Mda wa kufanya tendo la ndoa baada ya kujifungua.
1. Hili ni tatizo ambalo linawapata wanawake wengi ambapo hawajui ni mda gani na wakati gani waanze kufanya tendo la ndoa baada ya kujifungua, wengine wanakaa mda mrefu wengine mfupi ila kadri ya wataalamu wanashuri kuwa Mama anaweza kuanza kufanya tendo la ndoa baada ya wiki sita au siku arobaini na mbili tangia siku aliyojifungua, tendo la ndoa linakatazwa lisifanyike kwa Mama ndani ya siku arobaini na mbili baada ya kujifungua kwa sababu zifuatazo.
2.wakati wa kujifungua mwili wa Mama unakuwa uko tofauti kwa hiyo viungo vya Mama vinapaswa kujirudisha katika hali ya kawaida kwa sababu wakati wa kubeba mimba na kukua Kuna mabadiliko mengi kwenye mwili wa Mama kwa hiyo Mama anapojifungua anapaswa kurudi kwenye hali ya kawaida kadri ya wataalamu hali ya kawaida walau ni siku arobaini na mbili, kwa sababu ya utofauti wetu wakati wa kujifungua ni vizuri kuwasikiliza wataalamu wa afya Ili kama pametokea tatizo wakati wa kujifungua siku zinaweza kuongezewa .
3. Pia Mama anapojifungua Kuna bado uchafu unakuwa unatokea taratibu, kwa hiyo ikitokea mwanamke akafanya tendo la ndoa kabla ya siku zilizopangwa kwa sababu ya uchafu unaotoka anaweza kupata maambukizi, wote wawili ambao ni baba na Mama kwa hiyo kusubiri ni muhimu.
4. Na pengine kwa sababu ya kuwepo kwa ujauzito Kuna kipindi homoni zina badirisha mwili wa Mama ambapo Mama anakuwa mkavu kabisa kwenye via vya uzazi hali inayosababisha kuchubuka wakati wa kujamiiana, kwa hiyo ni vizuri kusubiri mpaka Mama apone kabisa.
5. Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kujua hilo kwa sababu wakikosea kuwakumbusha waume zao wanaweza kupata matatizo mbalimbali na wanaume wanapaswa kuwa Linda na kuwasaidia wake zao Ili siku za kujamiiana zifike.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 web hosting 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Kujaa gesi tumboni
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za kujaa tmgesi tumbon
Soma Zaidi...Zijue Athari za kuweka vitu ukeni.
Posti hii inahusu zaidi athari za kuweka vitu ukeni, tunajua kwa wakati huu kadri ya kukua kwa sayansi na teknolojia watu wanaendelea kugundua mbinu mbalimbali ili waweze kuwafurahisha wapenzi wao wakati wa kufanya tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Niharisha siku ya pili baada ya tendo. Jana hadi leo sijapata choo inawezakua nimeshika ujauzito?
Hivi unadhani kuharisha ni katika dalili za mimba, vipi kuhusu kutopata choo pia inaweza kuwa ni ujauzito?
Soma Zaidi...Madhara ya kutumia madawa ya shida ya upumuaji
Post hii inahusu zaidi madhara ya kutumia madawa ya shida ya upumuaji, ni madhara madogo madogo ambayo utokea kwa watumiaji wa matatizo ya kupumua.
Soma Zaidi...Dalili za mama mjamzito akikaribia kujifungua
Post hii inazungumzia mama wajawazito Mara tu mama anapohisi kuwa yeye ni mjamzito anashauriwa kuanza clinic.na clinic hizi zinasaidia kuwapatia wakina mama elimu,namna ya kumkinga Mtoto asipatwe na maradhi Kama UKIMWI. Pia mama anapoanza clinic
Soma Zaidi...