Posti hii inahusu zaidi mda ambao mama anapaswa kukaa bila kufanya tendo la ndoa mara tu baada ya kujifungua.
1. Hili ni tatizo ambalo linawapata wanawake wengi ambapo hawajui ni mda gani na wakati gani waanze kufanya tendo la ndoa baada ya kujifungua, wengine wanakaa mda mrefu wengine mfupi ila kadri ya wataalamu wanashuri kuwa Mama anaweza kuanza kufanya tendo la ndoa baada ya wiki sita au siku arobaini na mbili tangia siku aliyojifungua, tendo la ndoa linakatazwa lisifanyike kwa Mama ndani ya siku arobaini na mbili baada ya kujifungua kwa sababu zifuatazo.
2.wakati wa kujifungua mwili wa Mama unakuwa uko tofauti kwa hiyo viungo vya Mama vinapaswa kujirudisha katika hali ya kawaida kwa sababu wakati wa kubeba mimba na kukua Kuna mabadiliko mengi kwenye mwili wa Mama kwa hiyo Mama anapojifungua anapaswa kurudi kwenye hali ya kawaida kadri ya wataalamu hali ya kawaida walau ni siku arobaini na mbili, kwa sababu ya utofauti wetu wakati wa kujifungua ni vizuri kuwasikiliza wataalamu wa afya Ili kama pametokea tatizo wakati wa kujifungua siku zinaweza kuongezewa .
3. Pia Mama anapojifungua Kuna bado uchafu unakuwa unatokea taratibu, kwa hiyo ikitokea mwanamke akafanya tendo la ndoa kabla ya siku zilizopangwa kwa sababu ya uchafu unaotoka anaweza kupata maambukizi, wote wawili ambao ni baba na Mama kwa hiyo kusubiri ni muhimu.
4. Na pengine kwa sababu ya kuwepo kwa ujauzito Kuna kipindi homoni zina badirisha mwili wa Mama ambapo Mama anakuwa mkavu kabisa kwenye via vya uzazi hali inayosababisha kuchubuka wakati wa kujamiiana, kwa hiyo ni vizuri kusubiri mpaka Mama apone kabisa.
5. Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kujua hilo kwa sababu wakikosea kuwakumbusha waume zao wanaweza kupata matatizo mbalimbali na wanaume wanapaswa kuwa Linda na kuwasaidia wake zao Ili siku za kujamiiana zifike.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Tezidume ni moja ya magonjwa hayari yanayotokea katika mwili wa mwanaume.Hapa nimekuandalia sababu za kutokea kwa tezi dume.
Soma Zaidi...Mimba hatari iliyotungia nje ya mji wa mimba, ni zipi dalili zake na ni kivipo mimba inatungia nje?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wajawazito wanaweza kuzipata wakiwa na Dalli au tayari wana kifafa cha mimba.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Dalili za saratani kwa watoto, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa watoto na ikiwa mlezi au mzazi akiziona tu anaweza kutambua mara moja kwamba hii ni saratani au la na kama bado ana wasiwasi anaweza kupata msaada zaidi kutoka kwa wataa
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo anaweza kuzipata mwenye Ugonjwa wa tezi dume, sio Dalili zote mtu anaweza kuzipata kwa sababu dalili kama hizi zinaweza kujitokeza hata kwa magonjwa mengine.
Soma Zaidi...Majimaji yanayitoka kwenye uke yanafungamana na taarifa nyingi kuhusu afya vya mwanamke. Ujauzito, maradhi, mabadiliko ya homoni na zaidi.
Soma Zaidi...