picha

Fahamu mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa

Posti hii inahusu zaidi mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa, kwa kawaida tunajua kwamba mtoto wakati wa kuzaliwa ni lazima atangulize kichwa ila Kuna kipindi mtoto anatanguliza matako, kuna aina nne za mtoto kutanguliza matako.

Aina za mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa.

1. Tunaposema kwamba mtoto katanguliza matako kuna aina mbalimbali za kutanguliza matako , pengine ni matako yenyewe mtoto akiwa amejikunja aina hii kwa kitaalamu huitwa complete breech, kwa hiyo mikono ya mtoto huwa imejikunja Ila mtoto uzaliwa kawaida au hali kama sio nzuri mtoto anaweza kufanyiwa upasuaji na kutolewa kawaida tu.

 

2.Aina nyingine ni pale mtoto anapokuwa ametanguliza matako na mikono ikiwa imejikunja Ila ameamsha mguu mmoja juu na mguu wa pili unakuwa imejikunja chini ya mguu ulioamshwa juu,aina hii kwa kitaalamu huitwa in complete breech, kwa hiyo wauguzi na wataalamu wengine wa afya wanapaswa kufahamu Ili kuweza kuwasaidia wakina mama waweze kujifungua salama.

 

3. Kuna aina nyingine ni pale Mtoto anakuwa ametanguliza matako lakini miguu yake yote imeinuliwa juu na mikono alkiwa amejikumbatia kifuani aina hii kwa kitaalamu huitwa frank breech,kwa hiyo mtoto akijitokeza namna hii anapaswa kuangaliwa vizuri Ili kuepukana kuleta matatizo wakati wa kujifungua.

 

4. Kwa hiyo baada ya kuona na kujua aina za mtoto aliyetanguliza matako tunapaswa kuelewa kuwa na Hawa ni watoto wa kawaida, Kuna jamii ambazo uona kuwa ni watoto wa kipekee katika familia na kwa wakati mwingine upatiwa majina ya mapacha wakimanisha kuwa ni mapacha kuna jamii nyingine wanapona labda ni mkosi na kuanza kutambikia wakiwa na maana kwamba waondoe mkosi au tukio baya linaloashiliwa na mtoto kutanguliza matako.

 

5. Kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa kwenye jamii Ili kuweza kuondoa hizi Imani potofu na kufahamu kuwa huyu ni mtoto wa kawaida kama watoto wengine na pia kitenge cha mtoto kutanguliza matako ni kawaida utokea hasa kwa wanawake waliojofungua mara nyingi kwa hiyo uwanja huwa ni mkubwa na mtoto uweza kujigeuza jinsi anavyopenda akiwa tumboni, pia Mama akigunduliwa mapema kuwa mtoto katanguliza matako ni vizuri kujitahidi kujifungulia hospital Ili kupata huduma nzuri 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 8241

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Njia za kufanya ili kuepukana na tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo mtu anapaswa kutumia ili kuweza kupunguza tatizo hili kisiweze kutokea na pia kama jamii ikishirikiana kwa pamoja tunaweza kuepusha kwa kufanya yafuatayo.

Soma Zaidi...
Madhara ya mwili kushindwa kutengeneza projestron ya kutosha

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo mtu anaweza kupata ikiwa mwili utaeweza kutengeneza progesterone ya kutosha.

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo chini upande wa kulia

Soma Zaidi...
Kutoka kwa mimba, sababu za kutoka kwa mimba, dalili za kutoka mimba na kuzuia mimba kuoka

Mimba inapotoka ina dalili, na zipo sababu kadhaa za kutoka kwa mimba. Je utazuiaje mimba kutoka. Soma makala hii

Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka.

Post hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka mambo haya yanaweza yakawahusu akina Mama wenyewe, familia na jamii kwa ujumla.

Soma Zaidi...
Mabadiliko ya uzito kwa mjamzito

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya uzito kwa mjamzito, hii ni hali ya kubadilika kwa uzito kwa Mama akiwa na Mimba

Soma Zaidi...