Fahamu mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa
Posti hii inahusu zaidi mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa, kwa kawaida tunajua kwamba mtoto wakati wa kuzaliwa ni lazima atangulize kichwa ila Kuna kipindi mtoto anatanguliza matako, kuna aina nne za mtoto kutanguliza matako.
Aina za mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa.
1. Tunaposema kwamba mtoto katanguliza matako kuna aina mbalimbali za kutanguliza matako , pengine ni matako yenyewe mtoto akiwa amejikunja aina hii kwa kitaalamu huitwa complete breech, kwa hiyo mikono ya mtoto huwa imejikunja Ila mtoto uzaliwa kawaida au hali kama sio nzuri mtoto anaweza kufanyiwa upasuaji na kutolewa kawaida tu.
2.Aina nyingine ni pale mtoto anapokuwa ametanguliza matako na mikono ikiwa imejikunja Ila ameamsha mguu mmoja juu na mguu wa pili unakuwa imejikunja chini ya mguu ulioamshwa juu,aina hii kwa kitaalamu huitwa in complete breech, kwa hiyo wauguzi na wataalamu wengine wa afya wanapaswa kufahamu Ili kuweza kuwasaidia wakina mama waweze kujifungua salama.
3. Kuna aina nyingine ni pale Mtoto anakuwa ametanguliza matako lakini miguu yake yote imeinuliwa juu na mikono alkiwa amejikumbatia kifuani aina hii kwa kitaalamu huitwa frank breech,kwa hiyo mtoto akijitokeza namna hii anapaswa kuangaliwa vizuri Ili kuepukana kuleta matatizo wakati wa kujifungua.
4. Kwa hiyo baada ya kuona na kujua aina za mtoto aliyetanguliza matako tunapaswa kuelewa kuwa na Hawa ni watoto wa kawaida, Kuna jamii ambazo uona kuwa ni watoto wa kipekee katika familia na kwa wakati mwingine upatiwa majina ya mapacha wakimanisha kuwa ni mapacha kuna jamii nyingine wanapona labda ni mkosi na kuanza kutambikia wakiwa na maana kwamba waondoe mkosi au tukio baya linaloashiliwa na mtoto kutanguliza matako.
5. Kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa kwenye jamii Ili kuweza kuondoa hizi Imani potofu na kufahamu kuwa huyu ni mtoto wa kawaida kama watoto wengine na pia kitenge cha mtoto kutanguliza matako ni kawaida utokea hasa kwa wanawake waliojofungua mara nyingi kwa hiyo uwanja huwa ni mkubwa na mtoto uweza kujigeuza jinsi anavyopenda akiwa tumboni, pia Mama akigunduliwa mapema kuwa mtoto katanguliza matako ni vizuri kujitahidi kujifungulia hospital Ili kupata huduma nzuri
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa.
Posti hii inahusu zaidi sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa, ni sababu ambazo utokea kwa akina Mama wengi kadri ya wataalamu wametafuta asilimia kuwa asilimia sabini ya wanawake mifuko yao ya kizazi kushindwa kisinyaa.
Soma Zaidi...Dalili za kujifunguwa, na dalili za uchungu wa kujifunguwa
Nitajuwaje kama mjamzito amekaribia kujifunguwa, ni dalili gani anaonyesha, dalili za uchungu wa kujifunguwa
Soma Zaidi...Damu, majimaji na uteute unaotoka kwenye uke wa Mjamzito, sababu zake na dalili zake
Unataka kujuwa sababu za mjamzito kutokwa na damu, utelezi ama majimaji kwenye uke wake. Na dalili gani zinaashiriwa na majimaji haya
Soma Zaidi...Dalili za kujifungua hatua kwa hatua
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za kujifungua hatua kwa hatua
Soma Zaidi...Ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito, ni ugonjwa unaowapata sana akina mama wajawazito na uisha tu pale Mama anapojifungua kwa hiyo tunapaswa kujua wazi sababu za ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito.
Soma Zaidi...Sababu za Kukoma hedhi (perimenopause)
Kukoma hedhi hufafanuliwa kuwa hutokea miezi 12 baada ya kipindi chako cha mwisho cha hedhi na huashiria mwisho wa mizunguko ya hedhi. Kukoma hedhi kunaweza kutokea katika miaka ya 40 au 50. Kukoma hedhi ni mchakato wa asili wa kibaolojia. Ingawa pia in
Soma Zaidi...