Posti hii inahusu zaidi mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa, kwa kawaida tunajua kwamba mtoto wakati wa kuzaliwa ni lazima atangulize kichwa ila Kuna kipindi mtoto anatanguliza matako, kuna aina nne za mtoto kutanguliza matako.
1. Tunaposema kwamba mtoto katanguliza matako kuna aina mbalimbali za kutanguliza matako , pengine ni matako yenyewe mtoto akiwa amejikunja aina hii kwa kitaalamu huitwa complete breech, kwa hiyo mikono ya mtoto huwa imejikunja Ila mtoto uzaliwa kawaida au hali kama sio nzuri mtoto anaweza kufanyiwa upasuaji na kutolewa kawaida tu.
2.Aina nyingine ni pale mtoto anapokuwa ametanguliza matako na mikono ikiwa imejikunja Ila ameamsha mguu mmoja juu na mguu wa pili unakuwa imejikunja chini ya mguu ulioamshwa juu,aina hii kwa kitaalamu huitwa in complete breech, kwa hiyo wauguzi na wataalamu wengine wa afya wanapaswa kufahamu Ili kuweza kuwasaidia wakina mama waweze kujifungua salama.
3. Kuna aina nyingine ni pale Mtoto anakuwa ametanguliza matako lakini miguu yake yote imeinuliwa juu na mikono alkiwa amejikumbatia kifuani aina hii kwa kitaalamu huitwa frank breech,kwa hiyo mtoto akijitokeza namna hii anapaswa kuangaliwa vizuri Ili kuepukana kuleta matatizo wakati wa kujifungua.
4. Kwa hiyo baada ya kuona na kujua aina za mtoto aliyetanguliza matako tunapaswa kuelewa kuwa na Hawa ni watoto wa kawaida, Kuna jamii ambazo uona kuwa ni watoto wa kipekee katika familia na kwa wakati mwingine upatiwa majina ya mapacha wakimanisha kuwa ni mapacha kuna jamii nyingine wanapona labda ni mkosi na kuanza kutambikia wakiwa na maana kwamba waondoe mkosi au tukio baya linaloashiliwa na mtoto kutanguliza matako.
5. Kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa kwenye jamii Ili kuweza kuondoa hizi Imani potofu na kufahamu kuwa huyu ni mtoto wa kawaida kama watoto wengine na pia kitenge cha mtoto kutanguliza matako ni kawaida utokea hasa kwa wanawake waliojofungua mara nyingi kwa hiyo uwanja huwa ni mkubwa na mtoto uweza kujigeuza jinsi anavyopenda akiwa tumboni, pia Mama akigunduliwa mapema kuwa mtoto katanguliza matako ni vizuri kujitahidi kujifungulia hospital Ili kupata huduma nzuri
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Kama unadhani una tatizo la kuwahi kufika kileleni basi post hii ni kwa ajili yako.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye mfumo wa chakula kwa wajawazito, ni mabadiliko ambayo utokea kwa wajawazito hasa kwenye mfumo wa chakula.
Soma Zaidi...Je ni kweli kupima kimoja cha mloka kinaweza kupima mimba zaidi ya mara moka?
Soma Zaidi...Majimaji yanayitoka kwenye uke yanafungamana na taarifa nyingi kuhusu afya vya mwanamke. Ujauzito, maradhi, mabadiliko ya homoni na zaidi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi uchafu unaotoka ukeni na rangi zake, kwa kawaida ukeni utolewa uchafu, uchafu huo unaweza kuwa kawaida na unaweza kuwa na rangi mbalimbali kutokana na kuwepo kwa Maambukizi.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi kazi za homoni katika Mzunguko wa hedhi, katika kipindi hiki kuna homoni mbalimbali ambazo ufanya kazi kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Swali langi ni hiliMama mjamzito anapo hisi uchungu je mtoto huendelea kucheza tumboni?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi wajibu wa Mama mjamzito katika kileo mimba sio yeye tu Bali na wote waliomzunguka wanapaswa kuhakikisha kuwa mama mjamzito anapaswa kufanyiwa huduma zote Ili kuweza kujifungua salama na bila shida yoyote.
Soma Zaidi...Utawezaje kukabiliana na changamoto za ujauzito, je ni zipi changamoto hizo. Hapa nitakujuza.
Soma Zaidi...