picha

Fahamu mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa

Posti hii inahusu zaidi mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa, kwa kawaida tunajua kwamba mtoto wakati wa kuzaliwa ni lazima atangulize kichwa ila Kuna kipindi mtoto anatanguliza matako, kuna aina nne za mtoto kutanguliza matako.

Aina za mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa.

1. Tunaposema kwamba mtoto katanguliza matako kuna aina mbalimbali za kutanguliza matako , pengine ni matako yenyewe mtoto akiwa amejikunja aina hii kwa kitaalamu huitwa complete breech, kwa hiyo mikono ya mtoto huwa imejikunja Ila mtoto uzaliwa kawaida au hali kama sio nzuri mtoto anaweza kufanyiwa upasuaji na kutolewa kawaida tu.

 

2.Aina nyingine ni pale mtoto anapokuwa ametanguliza matako na mikono ikiwa imejikunja Ila ameamsha mguu mmoja juu na mguu wa pili unakuwa imejikunja chini ya mguu ulioamshwa juu,aina hii kwa kitaalamu huitwa in complete breech, kwa hiyo wauguzi na wataalamu wengine wa afya wanapaswa kufahamu Ili kuweza kuwasaidia wakina mama waweze kujifungua salama.

 

3. Kuna aina nyingine ni pale Mtoto anakuwa ametanguliza matako lakini miguu yake yote imeinuliwa juu na mikono alkiwa amejikumbatia kifuani aina hii kwa kitaalamu huitwa frank breech,kwa hiyo mtoto akijitokeza namna hii anapaswa kuangaliwa vizuri Ili kuepukana kuleta matatizo wakati wa kujifungua.

 

4. Kwa hiyo baada ya kuona na kujua aina za mtoto aliyetanguliza matako tunapaswa kuelewa kuwa na Hawa ni watoto wa kawaida, Kuna jamii ambazo uona kuwa ni watoto wa kipekee katika familia na kwa wakati mwingine upatiwa majina ya mapacha wakimanisha kuwa ni mapacha kuna jamii nyingine wanapona labda ni mkosi na kuanza kutambikia wakiwa na maana kwamba waondoe mkosi au tukio baya linaloashiliwa na mtoto kutanguliza matako.

 

5. Kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa kwenye jamii Ili kuweza kuondoa hizi Imani potofu na kufahamu kuwa huyu ni mtoto wa kawaida kama watoto wengine na pia kitenge cha mtoto kutanguliza matako ni kawaida utokea hasa kwa wanawake waliojofungua mara nyingi kwa hiyo uwanja huwa ni mkubwa na mtoto uweza kujigeuza jinsi anavyopenda akiwa tumboni, pia Mama akigunduliwa mapema kuwa mtoto katanguliza matako ni vizuri kujitahidi kujifungulia hospital Ili kupata huduma nzuri 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 8651

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Njia za kiasili zilizotumika zamani kqtika kupima ujauzito

Somo hili linakwenda kukuletea njia za asili walizotumia zamani katika kupima ujauzito

Soma Zaidi...
Dalili za kupasuka kondo la nyuma (placenta)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Kupasuka kwa kondo la nyuma (plasenta) (abruptio placentae) ni tatizo lisilo la kawaida lakini kubwa la ujauzito.Kondo la nyuma (Placenta) ni muundo ambao hukua ndani ya uterasi wakati wa ujauzito ili kumlisha mtoto ana

Soma Zaidi...
Malengo kwa Akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba.

Posti hii inahusu zaidi malengo kwa akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba, ni malengo ambayo yametolewa ili kuweza kusaidia mtoto azaliwe vizuri na mambo mengine kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo kabla ya kupata hedhi

Je unasumbuliwa na maumivu ya tumbo. Unadhani ni dalili za mimba na ukapima hakuna mimba.

Soma Zaidi...
Madhara ya kutotoa huduma kwa Mama anayevuja damu baada ya kujifungua

Posti hii inahusu zaidi Madara ya kutomsaidia mama anayetokwa na damu nyingi baada ya kujifungua.

Soma Zaidi...
Je siku ya kwanza kabisa ya ovulation mimba inakuwa ni uhakika kupata mimba?

Watu wengi wanadhania kuwa kufanya tendo la ndoa katika siku hatari ni lazima kuwa utapata ujauzito. Hili sio sahihi kabisa. Post hii itakwenda kuangalia jambo hili zaidi.

Soma Zaidi...