Jinsi Mtume Muhammad (s.a.w) alivyoipokea Qur-an:

(iii)Jinsi Mtume Muhammad (s.

Jinsi Mtume Muhammad (s.a.w) alivyoipokea Qur-an:

(iii)Jinsi Mtume Muhammad (s.a.w) alivyoipokea Qur-an:



Tumejifunza kuwa Allah (s.w) huwasiliana na wanaadamu kwa njia ya Wahyi (ufunuo) kwa kutumia njia za mawasiliano zifuatazo:
- Il-hamu.
- Kutumwa Malaika.
- Kuongeleshwa nyuma ya pazia.
- Maandishi (yaliyoandikwa tayari)
- Ndoto za kweli.



Qur-an ilishushwa kwa Mtume (s.a.w) kwa njia hii ya wahyi kupitia kwa Malaika Jibril.
Kuonesha kuwa Qur-an ni neno la Allah (s.w) na wala si tungo za Mtume Muhammad (s.a.w) ni ile hali aliyokuwa nayo wakati wa kupokea wahyi. Wakati wa mwanzo mwanzo wa kuanza kushushiwa wahyi Mtume (s.a.w) alikuwa akiyarudia haraka haraka yale aliyokuwa anasomewa na Malaika Jibril kwa wasi wasi kuwa atasahau. Ndipo Allah (s.w) akamtoa wasi wasi huo kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:


Usiutikise ulimi wako kwa (kuufanyia haraka) wahyi (unapoteremka. Wewe sikiliza tu. Usiseme kitu). Kwa hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha (kukukusanyia na kukusomesha). Wakati tunapokusomea, basi fuata kusomwa kwake. Kisha ni juu yetu kuubainisha (kukubainishia). (75:16-19)


Tutakusomesha (tutakusomea) wala hutasahau. Ila Akipenda Mwenyezi Mungu; Yeye anajua yaliyodhahiri na yaliyofichikana. (87:6-7)
Kwa hiyo kutokana na aya hizi Qur-an si maneno ya Mtume Muhammad (s.a.w) aliyoyatoa kichwani mwake. Kwani yangelitoka kichwani mwake asingelikuwa na wasi wasi wowote kuwa atakuja yasahau. Alikuwa na wasi wasi kwa sababu yeye akiwa ni Mtume wa Allah(s.w) alijua fika kuwa jukumu lake kubwa ni kuufikisha ujumbe wa Allah kwa watu kama ulivyo bila ya kupunguza au kuzidisha hata chembe.




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1905

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Maana ya Idgham na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid

Aina za idgham ni idgham al mutamathilain, na idgham al mutajanisain

Soma Zaidi...
Asbab nuzul surat at Tin, Sababu za kushuka surat at Tin (watin wazaitun)

Post hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa surat at Tin (watin wazaitun).

Soma Zaidi...
Saratul-humaza

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maswali yanayohusu quran

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Ni ipi aya ya mwisho kushuka katika Quran?

Maulamaa katika elimu ya Quran wametofautiana juu ya aya ya mwisho kushuka. Hata hivyo hapa nitakutajia ambayo imependekezwa zaidi

Soma Zaidi...
quran na sayansi

QURANI KATIKA ZAMA ZA SAYANSI NA TEKNOLOJIAAsalaalaamu alykum warahmatullah wabarakaatuh.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa Surat Al-Asr

Surat Al-Asri imeteremshwa Makka, na hapa utazujuwa sababu za kushuka kwa sura hii

Soma Zaidi...