Sababu za kushuka surat al alaqa
Asbsb nuzul surat al alaqa, sababu za kushuka surat alaqa. Sura hii imeshuka Makka na ina aya 19. Ni sura ya 96 katika mpangilio wa Quran.
{بسم الله الرحمان الرحيم}
اقْرَأْ بِاسْمِ رَبِّكَ الَّذِي خَلَقَ ﴿١﴾ خَلَقَ الْإِنسَانَ مِنْ عَلَقٍ ﴿٢﴾ اقْرَأْ وَرَبُّكَ الْأَكْرَمُ ﴿٣﴾ الَّذِي عَلَّمَ بِالْقَلَمِ ﴿٤﴾ عَلَّمَ الْإِنسَانَ مَا لَمْ يَعْلَمْ ﴿٥
Sura hii imeteremka Maka kwa makubaliano ya Mufasiruna wote. Pia Jamhuri ya mufasirun wanakubaliana kuwa sura hii ndio ya kwanza kushuka.
Hata hivyo zipo baadhi ya kauli kuwa sura ya kwanza kushuka ni Yaa ayuha al mudathir, hii kauli amesema Jabir Ibn Abdllah. Na imesemwa pia sura ya kwanza ni alhamdu amesema kauli hii Abu Maisarah na pia imesemwa sura ya kwanza ni aya ya 151 ya surat al anam . lakini kauli zote hizi sio sahihi. Iliyo sahihi ni kuwa sura ya jwanza ni surat al 'alaq
أَرَءَيْتَ ٱلَّذِى يَنْهَىٰ
[Surah Al-`Alaq: 9]
Aya hii na zinazofuata zinamzungumzia Abujahal mmoja katika maadui wa Mtume Muhammad wakati bado yupo Makkah.
Abujahal alikuwa akimuudhi Mtume hakuishia hapo pia alikuwa akimzuia kufanya ibada. Sio hivyo tu pia alikuwa akizuia watu wengine wasiende kwa Mtume wala kukutana nae.
Abujahal alikufa kwenye vita vya Badri na aliburutwa kifudifudi kuelekea kwenye shimo la kuzikia. Na wenzie wengine kama Abulahab alikufa siku chache baadaye.
Allah anasema:
9. Umemwona yule anaye mkataza
10 . Mja anapo sali?
11. Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?
12. Au anaamrisha uchamngu?
13. Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?
14. Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?
15. Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 web hosting 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 ai web app 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Aina saba za Viraa vya usomaji wa Quran
Post hii inakwenda kukuorodheshea aina saba za viraka vya usomaji wa Quran.
Soma Zaidi...Maisha ya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 19. Hapa utajifunza maisha ya Mtume kabla ya utume.
Soma Zaidi...Quran na sayansi
3; Mchujo wa maji dhaliliKatika aya nyingine tunakuja kupata funzo kuwa maji aliyoumbiwa mwanadamu licha yakuwa na sifa zilizotajwa katika kurasa zilizopita ila pia maji haya yanasifa kuwa ni madhalilina pia na yamechujwa kama tunavyoelezwa katika quran??
Soma Zaidi...