Asbsb nuzul surat al alaqa, sababu za kushuka surat alaqa. Sura hii imeshuka Makka na ina aya 19. Ni sura ya 96 katika mpangilio wa Quran.
{بسم الله الرحمان الرحيم}
اقْرَأْ بِاسْمِ رَبِّكَ الَّذِي خَلَقَ ﴿١﴾ خَلَقَ الْإِنسَانَ مِنْ عَلَقٍ ﴿٢﴾ اقْرَأْ وَرَبُّكَ الْأَكْرَمُ ﴿٣﴾ الَّذِي عَلَّمَ بِالْقَلَمِ ﴿٤﴾ عَلَّمَ الْإِنسَانَ مَا لَمْ يَعْلَمْ ﴿٥
Sura hii imeteremka Maka kwa makubaliano ya Mufasiruna wote. Pia Jamhuri ya mufasirun wanakubaliana kuwa sura hii ndio ya kwanza kushuka.
Hata hivyo zipo baadhi ya kauli kuwa sura ya kwanza kushuka ni Yaa ayuha al mudathir, hii kauli amesema Jabir Ibn Abdllah. Na imesemwa pia sura ya kwanza ni alhamdu amesema kauli hii Abu Maisarah na pia imesemwa sura ya kwanza ni aya ya 151 ya surat al anam . lakini kauli zote hizi sio sahihi. Iliyo sahihi ni kuwa sura ya jwanza ni surat al 'alaq
أَرَءَيْتَ ٱلَّذِى يَنْهَىٰ
[Surah Al-`Alaq: 9]
Aya hii na zinazofuata zinamzungumzia Abujahal mmoja katika maadui wa Mtume Muhammad wakati bado yupo Makkah.
Abujahal alikuwa akimuudhi Mtume hakuishia hapo pia alikuwa akimzuia kufanya ibada. Sio hivyo tu pia alikuwa akizuia watu wengine wasiende kwa Mtume wala kukutana nae.
Abujahal alikufa kwenye vita vya Badri na aliburutwa kifudifudi kuelekea kwenye shimo la kuzikia. Na wenzie wengine kama Abulahab alikufa siku chache baadaye.
Allah anasema:
9. Umemwona yule anaye mkataza
10 . Mja anapo sali?
11. Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?
12. Au anaamrisha uchamngu?
13. Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?
14. Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?
15. Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Kwa kuwa hakuna sababu mwalumu ikiyonukuliwa kuwa ndio chanzo cha kushushwa suravhii. Basi post hii itakujuza mambo ambayo huwenda hukuyajuwa kuhusu fadhika za surabhii na mengineyo.
Soma Zaidi...ASBAB NUZUL SABABU ZA KUSHUKA AYA NA SURA KWENYE QURAN Quran imeteremka kwa muda wa miaka 23 kidogokido.
Soma Zaidi...