image

Sababu za kushuka surat al alaqa

Asbsb nuzul surat al alaqa, sababu za kushuka surat alaqa. Sura hii imeshuka Makka na ina aya 19. Ni sura ya 96 katika mpangilio wa Quran.

{بسم الله الرحمان الرحيم}

اقْرَأْ بِاسْمِ رَبِّكَ الَّذِي خَلَقَ ﴿١﴾ خَلَقَ الْإِنسَانَ مِنْ عَلَقٍ ﴿٢﴾ اقْرَأْ وَرَبُّكَ الْأَكْرَمُ ﴿٣﴾ الَّذِي عَلَّمَ بِالْقَلَمِ ﴿٤﴾ عَلَّمَ الْإِنسَانَ مَا لَمْ يَعْلَمْ ﴿٥

Sura hii imeteremka Maka kwa makubaliano ya Mufasiruna wote. Pia Jamhuri ya mufasirun wanakubaliana kuwa sura hii ndio ya kwanza kushuka. 

 

Hata hivyo zipo baadhi ya kauli kuwa sura ya kwanza kushuka ni Yaa ayuha al mudathir, hii kauli amesema Jabir Ibn Abdllah. Na imesemwa pia sura ya kwanza ni alhamdu amesema kauli hii Abu Maisarah na pia imesemwa sura ya kwanza ni aya ya 151 ya surat al anam . lakini kauli zote hizi sio sahihi. Iliyo sahihi ni kuwa sura ya jwanza ni surat al 'alaq

 

أَرَءَيْتَ ٱلَّذِى يَنْهَىٰ
[Surah Al-`Alaq: 9]

Aya hii na zinazofuata zinamzungumzia Abujahal mmoja katika maadui wa Mtume Muhammad wakati bado yupo Makkah. 

 

Abujahal alikuwa akimuudhi Mtume hakuishia hapo pia alikuwa akimzuia kufanya ibada. Sio hivyo tu pia alikuwa akizuia watu wengine wasiende kwa Mtume wala kukutana nae. 

 

Abujahal alikufa kwenye vita vya Badri na aliburutwa kifudifudi kuelekea kwenye shimo la kuzikia. Na wenzie wengine kama Abulahab alikufa siku chache baadaye. 

 

Allah anasema: 

9. Umemwona yule anaye mkataza 
10 . Mja anapo sali? 
11. Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu? 
12. Au anaamrisha uchamngu? 
13. Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma? 
14. Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona? 
15. Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele! 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2301


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Je, mtu anaweza kusoma quran akiwa amelala?
Kusoma Qur'an kuna faida kubwa kwa Muislamu, kwanza kunampatia thawabu, kunatoa nuru maisha yake, mwili wake na kumlinda na mashetani na watu wabaya. Quran ni dawa na pozo kwa magonjwa. Thawabu za Qur-an hulipwa kwa kila herufi. Quran pia huja kutet Soma Zaidi...

namna quran inavyogawanya mirathi na wanaorithi pamoja na mafungu yao
Qur-an inavyogawa MirathiMgawanyo wa mirathi umebainishwa katika Qur-an kama ifuatavyo:Mwenyezi Mungu anakuusieni juu ya watoto wenu: Mwanamume apate sawa na sehemu ya wanawake wawili. Soma Zaidi...

idadi sahihi kati ya sura zilizoshuka Makka na zile za madina
A. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa surat al-Fiil
SURAT AL-FIILSura hii imeteremshwa Makkah na ina Aya Sita pamoja na Basmallah. Soma Zaidi...

Wanaadamu kushindwa Kuandika Kitabu Mithili ya Qur-an:
Soma Zaidi...

Hukumu ya Ikhfau katika tajwid
Ikh-fau ni moja ya hukumu za nun sakina na tanwin kwenye hukumu za Quran tajwid Soma Zaidi...

HUKUMU ZA QALQALA
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Ni ipi aya ya mwisho kushuka katika Quran?
Maulamaa katika elimu ya Quran wametofautiana juu ya aya ya mwisho kushuka. Hata hivyo hapa nitakutajia ambayo imependekezwa zaidi Soma Zaidi...

Aina za usomaji wa Quran
Je kuna aina ngapi zabusomaji wa Quran Soma Zaidi...

Nini maana ya Quran
Post hii inakwenda kukuambia maana ya Quran Soma Zaidi...

Quran haikuchukuliwa kutoka kwenye biblia
Soma Zaidi...

Kwa nini quran ilishuka kidogo kidogo?
Kuna sababu nyingi za kuonyesha umuhimu wa Quran kushuka kwa mfumo wa kidogo kidogo Soma Zaidi...