(ii)Qur-an Yenyewe Inajieleza kuwa ni Ufunuo Kutoka kwa Allah (s.
(ii)Qur-an Yenyewe Inajieleza kuwa ni Ufunuo Kutoka kwa Allah (s.w) :
Ukiisoma Qur-an kwa makini utakuta kuna aya nyingi zinazojieleza kuwa Qur-an imeshushwa kutoka kwa Allah, kama inavyodhihirika katika aya chache zifuatazo:
Lakini Allah anayashuhudia kuwa aliyokuteremshia (kuwa ni haki) ameyateremsha kwa ilimu yake, na Malaika (pia) wana shuhudia. Na Allah anatosha kuwa shahidi. (4:166).
"Uteremsho wa Kitabu hiki hauna shaka kuwa umetoka kwa Muumba wa ulimwengu. Je, wanasema: "Amekitunga mwenyewe ". (Sivyo hivyo). Bali hicho ni haki itokayo kwa Mola wako ili uwaonye watu wasiojiwa na muonyaji kabla yako. Huenda wakaongoka." (32:2-3)
Na Kitabu tulichokuletea kwa wahyi ndicho cha haki, kinasadikisha (vitabu) vilivyokuwa kabla yake. Bila shaka Allah kwa waja wake ni Mwenye kuwajua vyema na kuwaona vizuri." (35:31)
Ni mwenye kuleta baraka (kweli kweli) yule aliyeteremsha Qur-an kwa mja wake, ili awe muonyaji kwa walimwengu wote. (25:1)
Uteremsho wa Kitabu hiki umetoka kwa Allah, mwenye nguvu, na mwenye hikima. (45:2)
Aya zote hizi na nyingi nyinginezo kama hizi zilizomo ndani ya Qur-an hujieleza wazi wazi kuwa Qur-an ni Kitabu cha Allah (s.w) alichowashushia wanaadamu kupitia kwa Mtume Muhammad (s.a.w). Pangelikuwa na haja gani Mtume kuandika kitabu kisha adai kuwa kinatoka kwa Allah (s.w) tukikumbuka kuwa yeye amekuwa mwaminifu na mkweli katika historia yote ya maisha yake.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
3; Mchujo wa maji dhaliliKatika aya nyingine tunakuja kupata funzo kuwa maji aliyoumbiwa mwanadamu licha yakuwa na sifa zilizotajwa katika kurasa zilizopita ila pia maji haya yanasifa kuwa ni madhalilina pia na yamechujwa kama tunavyoelezwa katika quran??
Soma Zaidi...Ikh-fau ni moja ya hukumu za nun sakina na tanwin kwenye hukumu za Quran tajwid
Soma Zaidi...Al fiyl ni neno la Kiarabu lenye maana ya tembo. Sura hii inazungumziakisa cha jeshi lenye tembo. Jeshi hili lilikuwa na nia ya kuvunja al qaaba
Soma Zaidi...SURATUN-NASR Sura hii imeteremka wakati Mtume (s.
Soma Zaidi...Wanazuoni wengi zaidi wanakubaliana ya kuwa sura hii surat At-Takaathur ilishuka Makka, na hizi ndio sababu za kushuka kwa sura hii
Soma Zaidi...Asbab nuzul surat al qadi. Hii ni sura ya 97 katika mpangilio wa mashaf. Surat al qadir imeteremshwa Madina na ina aya 5.
Soma Zaidi...Makala hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa alam nasharah yaani Surat Ash sharh.
Soma Zaidi...Sura za Makka na Madina Kutokana na historia ya kushuka kwake sura za Qur-an zimegawanywa katika makundi mawili - sura za Makka na sura za Madina.
Soma Zaidi...Tafsiri ya quran kw akiswahili, imeandikw ana Shekh Ali Muhsin al-Barwani
Soma Zaidi...