Makala hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa alam nasharah yaani Surat Ash sharh.
Surat Ash sharh, imeteremka Makkah na ina aya 8. Sura hii ni miongoni mwa sura za mwanzo kushuka. Sura hii ni ya 94 katika mpangilio wa Quran jinsi ilivyoandikwa kwenye mashaf. Sura hii ni sura iliyotangulia yaani surat dhuhaa zinafanana maudhui zao, na zinakadiriwa kushuka katika nyakati sawa. Wakati mwingine sura hizi huchanganywa kwenye kusoma.
Sura hii inasimulia kisa cha kupasuliwa kifua mtume. Tukio hili inasemekeana limetokea mara mbili. Moja alipokuwa mtoto na mara nyingine ni pale alipokuwa katika safari ya Israa na Miraj. Sura hii na iliyofuata zinataja baadhi ya neema ambazo Allah amempa Mtume s.a.w.
Sababu za kushuka sura hii:
Katika historia hakuna sababu maalumu za kushuka sura hii kama ambavyo tumeona sura zilizopita. Lakini ipo hivi. Sura hii na iliyotangulia zilishuka katika wakati ambao ndio Mtume s.a.w amepewa Utume. bado ni mgeni wa kazi ya utume. Wakati ambao vikwazo, fitina kutoka kwa makafiri vilikuwa vimeanza kupamba moto. Sura hizi zilishuka kwa lengo la kumfariji Mtume s.a.w. Na ndio maana sura hizi zinataja baadhi ya neema ambazo Allah amempa Mtume Muhammad, ambazo miongoni mwazo hakuna Mtume mwingine aliyepewa. Kwa mfano kupasuliwa kifu na kuondolewa uzito ambao ambao ungemfanya kazi ya utume iwe ngumu. Pia neema nyingine ni kutukuzwa utajo wake. Yaani huwezi shahadia kwa kusema laa ilaaha Illa Llha, mpaka umalizie Muhammad rasulullah.
Kisha sura ikaendelea kumfariji kuwa hakika kila utakapopata uzito basi kuna wepesi pia ndani yake. Yaani baada ya taabu utakayoipata basi ujuwe kuna neema zinafuata mbele. Aya ikaendelea kuwa utakapopa faragha fanya juhudi ya kutafuta radhi za Allah kwa ibada na adhkar na mambo mengine.
Ufupi wa maneno ni kuwa sura hii imeshuka kwa lengo la kumfariji Mtume s.a.w kutokana na yale aliyoyakuta katika kazi ya utume, na ktokana na yatakayokuja kutokea kama matokeo ya kazi ya Utume. Allah ndiye anajuwa zaidi
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu
Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF
Share On
Facebook
or
Whatsapp
Imesomwa mara 1841
Sponsored links
π1 Madrasa kiganjani
π2 Kitau cha Fiqh
π3 Kitabu cha Afya
π4 kitabu cha Simulizi
idadi sahihi kati ya sura zilizoshuka Makka na zile za madina
A. Soma Zaidi...
Jinsi Mtume Muhammad (s.a.w) alivyoipokea Qur-an:
(iii)Jinsi Mtume Muhammad (s. Soma Zaidi...
Sifa za waumini katika quran
Soma Zaidi...
HUKUMU YA NUN SAKINA NA TNWIN
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...
HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA (MIIM SAKINA)
HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA : Mym sakina ni miym ambayo haina iβrab ( Ω
Ω). Soma Zaidi...
HUKUMU ZA QALQALA
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...
Amri ya Kuchinja Ng'ombe
Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr. Soma Zaidi...
Suratul-takaathur (102) imeteremshwa makkah Ina aya nane
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Ni ipi aya ya mwisho kushuka katika Quran?
Maulamaa katika elimu ya Quran wametofautiana juu ya aya ya mwisho kushuka. Hata hivyo hapa nitakutajia ambayo imependekezwa zaidi Soma Zaidi...
quran na sayansi
QURANI KATIKA ZAMA ZA SAYANSI NA TEKNOLOJIAAsalaalaamu alykum warahmatullah wabarakaatuh. Soma Zaidi...
Aina za Madda twabiy kwenye usomaji wa Quran
Madda zimegawanyika katika maeneo makuu mawili ambayo ni madda twabiy na madda fariy Soma Zaidi...
HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA
SURA YA NNE HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA HUKUMU ZA MIYM SAKINA: Mym sakina ni miym ambayo haina iβrab ( Ω
Ω). Soma Zaidi...