Aasbab Nuzul surat Ash sharh: sababu za kushuka alam nashrah (surat Ash sharh)

Makala hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa alam nasharah yaani Surat Ash sharh.

Surat Ash sharh, imeteremka Makkah na ina aya 8. Sura hii ni miongoni mwa sura za mwanzo kushuka. Sura hii ni ya 94 katika mpangilio wa Quran jinsi ilivyoandikwa kwenye mashaf. Sura hii ni sura iliyotangulia yaani surat dhuhaa zinafanana maudhui zao, na zinakadiriwa kushuka katika nyakati sawa. Wakati mwingine sura hizi huchanganywa kwenye kusoma.

 

Sura hii inasimulia kisa cha kupasuliwa kifua mtume. Tukio hili inasemekeana limetokea mara mbili. Moja alipokuwa mtoto na mara nyingine ni pale alipokuwa katika safari ya Israa na Miraj. Sura hii na iliyofuata zinataja baadhi ya neema ambazo Allah amempa Mtume s.a.w.

 

Sababu za kushuka sura hii:

Katika historia hakuna sababu maalumu za kushuka sura hii kama ambavyo tumeona sura zilizopita. Lakini ipo hivi. Sura hii na iliyotangulia zilishuka katika wakati ambao ndio Mtume s.a.w amepewa Utume. bado ni mgeni wa kazi ya utume. Wakati ambao vikwazo, fitina kutoka kwa makafiri vilikuwa vimeanza kupamba moto. Sura hizi zilishuka kwa lengo la kumfariji Mtume s.a.w. Na ndio maana sura hizi zinataja baadhi ya neema ambazo Allah amempa Mtume Muhammad, ambazo miongoni mwazo hakuna Mtume mwingine aliyepewa. Kwa mfano kupasuliwa kifu na kuondolewa uzito ambao ambao ungemfanya kazi ya utume iwe ngumu. Pia neema nyingine ni kutukuzwa utajo wake. Yaani huwezi shahadia kwa kusema laa ilaaha Illa Llha, mpaka umalizie Muhammad rasulullah. 

 

Kisha sura ikaendelea kumfariji kuwa hakika kila utakapopata uzito basi kuna wepesi pia ndani yake. Yaani baada ya taabu utakayoipata basi ujuwe kuna neema zinafuata mbele. Aya ikaendelea kuwa utakapopa faragha fanya juhudi ya kutafuta radhi za Allah kwa ibada na adhkar na mambo mengine.

 

Ufupi wa maneno ni kuwa sura hii imeshuka kwa lengo la kumfariji Mtume s.a.w kutokana na yale aliyoyakuta katika kazi ya utume, na ktokana na yatakayokuja kutokea kama matokeo ya kazi ya Utume. Allah ndiye anajuwa zaidi

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 3215

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 web hosting    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Sababu za kushuka Surat al Kafirun

Sura hii imekuja kukata rai ya Makafiri wa Makka kuhusu ibada ya ushirika. Hivi leo tungesema kuhusu dini mseto.

Soma Zaidi...
Je, mtu anaweza kusoma quran akiwa amelala?

Kusoma Qur'an kuna faida kubwa kwa Muislamu, kwanza kunampatia thawabu, kunatoa nuru maisha yake, mwili wake na kumlinda na mashetani na watu wabaya. Quran ni dawa na pozo kwa magonjwa. Thawabu za Qur-an hulipwa kwa kila herufi. Quran pia huja kutet

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al-Falaq na surat an-Nas na fadhila za kusoma sura hizi

SURAT AL-MUAWIDHATAYN (SURAT AL-FALAQ NA SURATUN-NAS) Inaelezwa kuwa sura mbili hizi zilishuka pamoja, na maulamaa wanaelezea kuwa Mtume (s.

Soma Zaidi...
fadhila za sura kwenye quran

FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya.

Soma Zaidi...
Adabu za kusikiliza quran

ADABU ZA KUSIKILIZA QURANI 1.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al Fatiha

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu srat al fatiha, faida zake na maudhui zake

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka Surat al fatiha (Alhamdu)

Kwa kuwa hakuna sababu mwalumu ikiyonukuliwa kuwa ndio chanzo cha kushushwa suravhii. Basi post hii itakujuza mambo ambayo huwenda hukuyajuwa kuhusu fadhika za surabhii na mengineyo.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al Zilzalah

surat Zalzalah ni sura ya 99 katika mpangilio wa Quran, na ina aya 8. Sura hii imeteremshwa Madina ila pia kuna kauli zinathibitisha kuwa ni ya Makkah. Katika hadithi iliyopewa daraja la hassan na Imam Tirmidh Mtume S.A.W amesema kuwa kusoa surat Zilzalah

Soma Zaidi...