Surat Al qariah, ni moja katika sura zilizochuka miaka ya mwanzoni mwa utume.
Wanazuoni wa Tafsiri hawakupata nukuu juu ya sababu iliyopelekea kushuka kwa sura hii.
Sura hii imeteremka Makkah na ni katika sura za mwanzoni kushuka. Katika mpangilio wa Quran ipo katika juzuu ya 30 katikati mwa surat al adiyah na surat at Takaathur.
Surat al qariah ina aya 11, maneno 36 na herufi 158. Mtindo wa mwanzo wa sura hii inafanana na surat al haqqah. Na sura zote zimeanza kuzungumzia kiyama.
Aya ya kwanza hadi ya tani zinazungumzia kuhusu kiama, na kuwa watu watafufuliwa na kutawanyika kama nzige. Na majabali na milima haitokuwepo tena.
Aya ya 6 hadi ya 9 inazungumzia kuhusu matendo, na kuwa matendo yote yatapinwa kwenye mizani. Kipimo cha matendo mema kikiwa kizito zaidi basi mtu ataingia peponi. Na kikiwa cha na tendo mabovu ni kizito zaidi mtu ataingizwa motoni.
Aya ya 10 na 11 zinazungumzia kuhusu huo moto wa hawiyah. Hili ni moja ya tabaka za moto wa jahannam.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
SURAT AL-MUAWIDHATAYN (SURAT AL-FALAQ NA SURATUN-NAS) Inaelezwa kuwa sura mbili hizi zilishuka pamoja, na maulamaa wanaelezea kuwa Mtume (s.
Soma Zaidi...Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa
Soma Zaidi...Ni zipi hizo herufi saba, na ni vipi viraa saba katika usomaji wa Quran
Soma Zaidi...Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.
Soma Zaidi...