image

Wanaadamu kushindwa Kuandika Kitabu Mithili ya Qur-an:

Wanaadamu kushindwa Kuandika Kitabu Mithili ya Qur-an:

(ix)Wanaadamu kushindwa Kuandika Kitabu Mithili ya Qur-an:



Ushahidi mkubwa na wa uwazi zaidi ni hii changa moto iliyonadiwa kwa wanaadamu wote katika Qur-an yenyewe. Ni kwamba, watu waliokufuru wa nyakati zote za historia ya Qur-an wanadai kuwa Qur-an si kitabu cha Allah(s.w) bali ni kitabu kinachotokana na kazi ya mwanaadamu, hususan Mtume Muhammad (s.a.w). Baadhi ya madai yao tumeshayaona katika kurasa za nyuma.


Baada ya kutoa madai yao haya yasiyo na ushahidi wowote au fununu yoyote ya ukweli, Allah (s.w), aliye Mjuzi na Mwingi wa hekima, Alitoa changamoto si kwa hawa wapinzani tu bali kwa wanaadamu wote ili baada ya hapo kila mwenye akili timamu ashuhudie kuwa Qur-an ni Kitabu cha Allah (s.w). Allah (s.w) alitoa wito kwa wapinzani wote wa Qur-an kuwa wakusanyike pamoja na washirikiane na wataalamu wote wa ulimwengu walio na uzoefu na uhodari katika sanaa ya uandishi kisha katika ushirikiano wao huo watoe kitabu mfano wa Qur-an. Historia nzima inatuonesha kuwa hakuna aliyefua dafu. Hebu turejee changa moto hii katika aya ifuatayo:


Sema: "Hata wakijikusanya watu (wote) na majini ili kuleta mfano wa hii Qur-an basi hawangaliweza kuleta mfano wake, hata kama watasaidiana (vipi) wao kwa wao." (17:88)



Baada ya kushindwa kutoa kitabu mfano wa Qur-an, Allah (s.w) aliwapa makafiri tahfifu ili wazidi kutanabahi na kuhuzunika kwa kuwanadia kuwa waandike mfano wa sura kumi tu za Qur-an badala ya sura 114, kama tunavyofahamishwa katika aya ifuatayo:



Ndiyo kweli wanasema kuwa: "Ameitunga mwenyewe (Muhammad hii Qur-an)?" Sema: "Basi leteni sura kumi za uwongo zilizotungwa mfano wa hii, na waiteni muwawezao (kuwaita) badala ya Allah (waje wakusaidieni kutunga hivyo) ikiwa mnasema kweli." (11:13)'



Hakuna aliyethubutu kutoa sura hizo kumi mfano wa Sura za Qur-an kwa wakati wote wa historia ya Qur-an. Allah (s.w) Mwingi wa Rehema na Mwingi wa Ujuzi na Hekima, alitoa tena tahfifu nyingine kwa kuwataka wale wote wanaodai kuwa Qur-an ni kitabu cha Mtume Muhammad (s.a.w) nao waandike angalau sura moja tu mfano wa sura za Qur-an kwa ufasaha wa lugha, mantiki, mtiririko wa maudhui na ukamilifu wa ujumbe. Hebu turejee aya zifuatazo:


"Na ikiwa mna shaka kwa hayo tuliyomteremshia mtumwa wetu, (kuwa hakuteremshiwa na Allah), basi leteni sura moja iliyofanywa na (mtu) aliye mfano wake, na muwaite miungu yenu bighairi ya Allah (wakusaidieni) ikiwa mnasema kweli." (2:23)


Je, ndiyo wanasema ameitunga? Sema: "Hebu (tungeni na nyie) mlete sura moja mfano wake na waiteni muwezao (kuwapata waje) isipokuwa Allah (wa kuwasaidieni) kama nyinyi mnasema kweli (kuwa haya ameyazua Muhammad)" (10:38)


Kama Muhammad (s.a.w) ndiye mwandishi wa Qur-an angelithubutu kweli kutoa changa moto hii kwa walimwengu wote wa nyakati zote? Mtume (s.a.w) angaliwezaje kutamka kwa uhakika kiasi hicho kuwa walimwengu wote hata wakishirkiana pamoja hawawezi kuandika kitabu mithili ya Qur-an uhakika ambao umebakia mpaka hivi leo? Kwa hiyo kushindwa kwa wanaadamu wa enzi zote za historia ya Qur-an kuleta mfano wa Qur-an angalau sura moja ni hoja tosha kuwa Qur-an ni Kitabu cha Allah (s.w).



Aidha Qur-an pia imewajibu wale watu wanaosema kuwa Muhammad (s.a.w) ndiye aliyeandika Qur-an kwa kuwataka watu hao wazingatie mawili: Kwanza Muhammad aliishi nao kwa muda wa miaka 40 na hakuonesha dalili zozote za kuwa mwandishi wala mshairi. Imekuwaje ghafla mtu huyo akaweza kuandika aya ambazo hakuna awezaye kuleta mfano wake? Pili, Muhammad angewezaje kuandika Qur-an na ilhali hakujua kusoma wala kuandika? Hoja hizo zinapatikana katika aya zifuatazo za Qur-an:


"Sema: Kama Allah angelitaka nisingalikusomeeni hii (Qur-an), wala asingalikujulisheni (hiyo Qur-an). Nalikaa baina yenu umri (mwingi) kabla ya haya; (hamkunisikia kusema kitu). Basi hamfahamu (kuwa haya si yangu mwenyewe kwa nafsi yangu)? (10:16)


"Na hukuwa mwenye kusoma chochote kabla ya hiki, wala hukukiandika kwa mkono wako wa kuume, (ingekuwa hivyo) wangefanya shaka wale wanaotaka kubadilisha (haki). (29:48)




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 458


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Wanaoongozwa na wasioongozwa na quran
Soma Zaidi...

QURAN: TAJWID, FADHIKA ZA KUSOMA QURAN, FADHILA ZA KUSIKILIZA QURAN, FAIDA ZA SURAT FATIHA, YASIN, BAQARA, TABARAK
Soma Zaidi...

quran na sayansi
YALIYOMONENO LA AWALI1. Soma Zaidi...

Ni zipi hukumu za nuni yenye sakina au tanwin?
Hapa utajifunza usomaji wa Quran pindi utakapokuta nuni yenyebsakina au tanwin Soma Zaidi...

Maana ya Idgham na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid
Aina za idgham ni idgham al mutamathilain, na idgham al mutajanisain Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat Ikhlas
Surat Ikhlas ni katika sura za kitawhid ambazo zilishuka miaka siku za mwanzoni mwa utume. Sura hii imekuja kujibu maswali mengi kuhusu Allah ikiwemo, Allah ni nani? Soma Zaidi...

HUKUMU ZA QALQALA
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Hukumu ya Ikhfau katika tajwid
Ikh-fau ni moja ya hukumu za nun sakina na tanwin kwenye hukumu za Quran tajwid Soma Zaidi...

Sura za makkah na madinah
Quran (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al Mauun
Sura hii ni katika sura ambazo zinahitaji kusomwa kwa mazingatio sana. Wanaoswali bila ya kuzingatia swala zao, wameonywa vikali sana. Wanaowatesa na kuwanyanyasa mayatima wameonywa vikali. Wanaowanyima wenye haja na masikini huku wakiwakaripia nakuwasem Soma Zaidi...

Faida za kujuwa Quran tajwid
Hapa nitakufindisha faida za kusoma quran kwa Tajwid. Soma Zaidi...