Menu



Quran si maneno ya shetani

Quran si maneno ya shetani

(v) Dai kuwa Qur-an ni aya za Shetani



Katika mwaka 1988 Salman Rushdie, Muingereza mwenye asili ya kihindi, aliandika kitabu chake alichokiita "Satanic Verses" (yaani aya za Shetani) ambamo amemtukana Mtume (s.a.w), Uislamu na Qur-an kwa kuiita "aya za Shetani."



Katika kitabu chake hicho, Rushdie amedai kuwa hapakuwa na wahy wowote uliomshukia Muhammad (s.a.w) bali alikuwa akidai tu kuwa anashushiwa Wahy. Aidha Rushdie anadai kuwa Muhammad (s.a.w) alikuwa ni mtu aliyekuwa akifuata matashi yake mwenyewe akiongozwa na shetani na kwa hiyo yote yaliyomo ndani ya Qur-an ni maneno ya shetani.



Pia Rushdie katika kitabu chake hicho amedai kuwa Mtume (s.a.w) hakuwa na uwezo wa kutofautisha wahy kutoka kwa Malaika au wahy kutoka kwa shetani.

Vile vile Salman Rushdie amedai kuwa Mtume (s.a.w) hakuwa na kumbukumbu ya kile alichowasomea waandishi wake na wala hakuweza kutambua hata kile ambacho waandishi hao wamekiongeza kichini-chini. Amepiga mfano wa mwandishi mmoja wa Kifursi kuwa alisomewa na Mtume aandike "Mwenye kusikia, mwenye kujua kila kitu" lakini yeye akaandika "Mwenye kujua na Mwenye hikma" na Mtume hakung'amua mabadiliko hayo!



Udhaifu wa madai ya Salman Rushdie
Kwanza,
ujumbe wa Qur-an umeteremshwa ili kumtoa binaadamu kutokana na hadaa zote za shetani. Shetani katika Qur-an ameelezwa wazi pamoja na vitimbi vyake na watu anaowatumia ili wanaadamu wasiweze kupotezwa naye. Hebu turejee aya chache zifuatazo:


"Na namna hii tumemfanyia kila Nabii maadui, (nao ni) mashetani katika watu na (mashetani) katika majini. Baadhi yao wanawafunulia wenzao maneno ya kupamba pamba ili kuwadanganya. Na Mola wako angelipenda wasingelifanya hayo. Basi waache na uongo wao." (6:112)


"Enyi wanaadamu! Shetani (Iblisi) asikutieni katika matata, kama alivyowatoa wazee wenu katika Pepo akawavua nguo zao ili kuwaonesha tupu zao. Hakika yeye pamoja na kabila yake wanakuoneni na hali ya kuwa hamuwaoni." Bila shaka sisi tumewajaalia mashetani kuwa marafiki wa wale wasioamini." (7:2 7)



"Kwa yakini Shetani ni adui yenu, basi mfanyeni adui (yenu; kwa hivyo msimtii) kwani anaita (analiita) kundi lake liwe katika watu wa Motoni." (35:6)
Kama Qur-an ni maneno ya Shetani, inakuwaje tena shetani mwenyewe ajidhihirishe kiasi hicho ili watu wamkimbie?



Pili, Allah (s.w) anasema kuwa laiti ingelikuwa hii Qur-an inatoka kwa mwingine asiye kuwa Yeye au kama ingekuwa ina waandishi wawili tofauti ambao wana malengo yanayopingana mmoja anavutia kwenye mema na mwingine kwenye uovu pangelikuwa na khitilafu nyingi (Qur-an 4:82). Je, uko mgongano wowote katika maneno ya Qur-an? Haupo, bali maneno yote ya Qur-an ni yenye kusadikishana. Hivyo haiwezekani Qur-an kuwa na mchanganyiko wa maneno ya shetani na ya Allah (s.w) kwa pamoja.



Tatu, Qur-an yenyewe imekataa kuwa Qur-an si maneno ya shetani."Wala hii si kauli ya shetani aliyefukuzwa (katika rehma za Mwenyezi Mungu.) (81:25)



Nne, Sote tunamfahamu shetani kuwa ni kiumbe dhaifu pamoja na kuwa hatumuoni. Sasa ikiwa shetani ameleta maneno na ujumbe mzito uliomo ndani ya Qur-an, kwanini na mashetani wengine nao hawakai pamoja kujibu zile changamoto zilizotolewa? "Mahound" kama alivyomwita Rushdie ni shetani mmoja tu, je pamekuwa na uzito gani kwa wanaadamu pamoja na majini wakichanganyika kuleta mfano wa angalau sura moja ya Qur-an? Qur-an imetoa changamoto hiyo tangu kuanza kushuka kwake:


"Sema "Hata wakijikusanya watu (wote) na majini kuleta mfano wa hii Qur-an basi hawangaliweza kuleta mfano wake, hata kama watasaidiana (vipi) wao kwa wao." (17:88)




                   


Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Quran Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1127


Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰5 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zifazofanana:-

Sababu za kushuka surat an-Nas na surat al Falaq
Sura mbili hizi pia hujulikana kwa jina la al muawidhatain ambazo ni surat an Nas na surat al falaq. Soma Zaidi...

Kwa nini quran ilishuka kidogo kidogo?
Kuna sababu nyingi za kuonyesha umuhimu wa Quran kushuka kwa mfumo wa kidogo kidogo Soma Zaidi...

Kushuka na kuhifadhiwa kwa quran, hatua kwa hatua: mafunzo ya baadhi ya sura za quran
QUR’AN 5. Soma Zaidi...

Sababu za kshuka surat al Asr
Sura hii ni katika sura za kitawhidi sana. Maulamaa wanasema inatosha sura hii kuwa ni mawaidha. Imamu sharifu anasema kuwa sura hii inatosha kuwa muongozo… Soma Zaidi...

Sababu za kushukasurat an Nasr
Sura hii ni katika sura za mwisho kushuka, huwendakuwa ndio ya mwisho kabisa. Masahaba waliamini kuwa sura hii imetabiri kifo cha Mtume S.A.W Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa surat Dhuha
Sura hii imetermka Makkah na ina aya 11. Sura hii ni moja ya sura ambazo zimeshuka mwanzoni wakati ambapo Mtume ameanza kazi ya utume. Soma Zaidi...

Kutokea Kweli Matukio yaliyotabiriwa katika Qur-an
Soma Zaidi...

QURAN: TAJWID, FADHIKA ZA KUSOMA QURAN, FADHILA ZA KUSIKILIZA QURAN, FAIDA ZA SURAT FATIHA, YASIN, BAQARA, TABARAK
Soma Zaidi...

surat al mauun
SURATUL-MAM’UUN Imeteremshwa Maka, anasimulia Ibn Jurayj kuwa Abuu Sufyan ibn Harb alikuwa na kawaida ya kuchinja ngamia wawili kila wiki, hivyo siku moja yatima mmoja alikuja kwake na kumlilia shida, na hakumsaidia kwa chochote na hatimaye akampiga yat.. Soma Zaidi...

Saratul-asr 103
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...