Quran si maneno ya shetani

Quran si maneno ya shetani

(v) Dai kuwa Qur-an ni aya za Shetani



Katika mwaka 1988 Salman Rushdie, Muingereza mwenye asili ya kihindi, aliandika kitabu chake alichokiita "Satanic Verses" (yaani aya za Shetani) ambamo amemtukana Mtume (s.a.w), Uislamu na Qur-an kwa kuiita "aya za Shetani."



Katika kitabu chake hicho, Rushdie amedai kuwa hapakuwa na wahy wowote uliomshukia Muhammad (s.a.w) bali alikuwa akidai tu kuwa anashushiwa Wahy. Aidha Rushdie anadai kuwa Muhammad (s.a.w) alikuwa ni mtu aliyekuwa akifuata matashi yake mwenyewe akiongozwa na shetani na kwa hiyo yote yaliyomo ndani ya Qur-an ni maneno ya shetani.



Pia Rushdie katika kitabu chake hicho amedai kuwa Mtume (s.a.w) hakuwa na uwezo wa kutofautisha wahy kutoka kwa Malaika au wahy kutoka kwa shetani.

Vile vile Salman Rushdie amedai kuwa Mtume (s.a.w) hakuwa na kumbukumbu ya kile alichowasomea waandishi wake na wala hakuweza kutambua hata kile ambacho waandishi hao wamekiongeza kichini-chini. Amepiga mfano wa mwandishi mmoja wa Kifursi kuwa alisomewa na Mtume aandike "Mwenye kusikia, mwenye kujua kila kitu" lakini yeye akaandika "Mwenye kujua na Mwenye hikma" na Mtume hakung'amua mabadiliko hayo!



Udhaifu wa madai ya Salman Rushdie
Kwanza,
ujumbe wa Qur-an umeteremshwa ili kumtoa binaadamu kutokana na hadaa zote za shetani. Shetani katika Qur-an ameelezwa wazi pamoja na vitimbi vyake na watu anaowatumia ili wanaadamu wasiweze kupotezwa naye. Hebu turejee aya chache zifuatazo:


"Na namna hii tumemfanyia kila Nabii maadui, (nao ni) mashetani katika watu na (mashetani) katika majini. Baadhi yao wanawafunulia wenzao maneno ya kupamba pamba ili kuwadanganya. Na Mola wako angelipenda wasingelifanya hayo. Basi waache na uongo wao." (6:112)


"Enyi wanaadamu! Shetani (Iblisi) asikutieni katika matata, kama alivyowatoa wazee wenu katika Pepo akawavua nguo zao ili kuwaonesha tupu zao. Hakika yeye pamoja na kabila yake wanakuoneni na hali ya kuwa hamuwaoni." Bila shaka sisi tumewajaalia mashetani kuwa marafiki wa wale wasioamini." (7:2 7)



"Kwa yakini Shetani ni adui yenu, basi mfanyeni adui (yenu; kwa hivyo msimtii) kwani anaita (analiita) kundi lake liwe katika watu wa Motoni." (35:6)
Kama Qur-an ni maneno ya Shetani, inakuwaje tena shetani mwenyewe ajidhihirishe kiasi hicho ili watu wamkimbie?



Pili, Allah (s.w) anasema kuwa laiti ingelikuwa hii Qur-an inatoka kwa mwingine asiye kuwa Yeye au kama ingekuwa ina waandishi wawili tofauti ambao wana malengo yanayopingana mmoja anavutia kwenye mema na mwingine kwenye uovu pangelikuwa na khitilafu nyingi (Qur-an 4:82). Je, uko mgongano wowote katika maneno ya Qur-an? Haupo, bali maneno yote ya Qur-an ni yenye kusadikishana. Hivyo haiwezekani Qur-an kuwa na mchanganyiko wa maneno ya shetani na ya Allah (s.w) kwa pamoja.



Tatu, Qur-an yenyewe imekataa kuwa Qur-an si maneno ya shetani."Wala hii si kauli ya shetani aliyefukuzwa (katika rehma za Mwenyezi Mungu.) (81:25)



Nne, Sote tunamfahamu shetani kuwa ni kiumbe dhaifu pamoja na kuwa hatumuoni. Sasa ikiwa shetani ameleta maneno na ujumbe mzito uliomo ndani ya Qur-an, kwanini na mashetani wengine nao hawakai pamoja kujibu zile changamoto zilizotolewa? "Mahound" kama alivyomwita Rushdie ni shetani mmoja tu, je pamekuwa na uzito gani kwa wanaadamu pamoja na majini wakichanganyika kuleta mfano wa angalau sura moja ya Qur-an? Qur-an imetoa changamoto hiyo tangu kuanza kushuka kwake:


"Sema "Hata wakijikusanya watu (wote) na majini kuleta mfano wa hii Qur-an basi hawangaliweza kuleta mfano wake, hata kama watasaidiana (vipi) wao kwa wao." (17:88)




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1579

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Hukumu ya tafkhim na tarqiq katika usomaji wa Quran tajwid

Tarqiq ni kuisoma herufi kwa kuipa wepesi na tqfkhim ni kuisoma herufi kwa kuipa uzito.

Soma Zaidi...
Quran si Mashairi kama wanavyodai makafiri

(i)Dai kuwa Qur-an ni Mashairi aliyotunga Muhammad (s.

Soma Zaidi...
Kwa nini quran ilishuka kidogo kidogo?

Kuna sababu nyingi za kuonyesha umuhimu wa Quran kushuka kwa mfumo wa kidogo kidogo

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat an-Nas na surat al Falaq

Sura mbili hizi pia hujulikana kwa jina la al muawidhatain ambazo ni surat an Nas na surat al falaq.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa Surat Al-Asr

Surat Al-Asri imeteremshwa Makka, na hapa utazujuwa sababu za kushuka kwa sura hii

Soma Zaidi...
namna quran inavyogawanya mirathi na wanaorithi pamoja na mafungu yao

Qur-an inavyogawa MirathiMgawanyo wa mirathi umebainishwa katika Qur-an kama ifuatavyo:Mwenyezi Mungu anakuusieni juu ya watoto wenu: Mwanamume apate sawa na sehemu ya wanawake wawili.

Soma Zaidi...
MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Aina saba za Viraa vya usomaji wa Quran

Post hii inakwenda kukuorodheshea aina saba za viraka vya usomaji wa Quran.

Soma Zaidi...
quran na sayansi

YALIYOMONENO LA AWALI1.

Soma Zaidi...