image

Qur-an Kushuka Kidogo Kidogo kwa Kipindi cha Miaka 23:

Qur-an Kushuka Kidogo Kidogo kwa Kipindi cha Miaka 23:

(iv)Qur-an Kushuka Kidogo Kidogo kwa Kipindi cha Miaka 23:



Historia inatuthibitishia kuwa Mtume Muhammad (s.a.w) hakuanza kuufundisha Uislamu na kuutangaza ulimwengu mzima kwa kurejea Qur-an kama Kitabu tulicho nacho hivi sasa bali aya za Qur-an zilikuwa zikimshukia kidogo kidogo kulingana na haja na wakati kwa kipindi chote cha Utume wake cha miaka 23. Kwa maana nyingine Qur-an imeshuka kidogo kidogo katika kipindi chote cha utume kuanzia mwanzo wa Utume 610 A.D. mpaka siku chache kabla ya kutawafu Mtume(saw), 632 A.D. Kuhusu Qur-an kushuka kidogo kidogo tunafahamishwa katika aya zifuatazo:


Na Qur-an tumeigawanya sehemu mbali mbali ili uwasomee watu kwa kituo, na tumeiteremsha kidogo kidogo. (17:106)



Na wakasema wale waliokufuru; Mbona hakuteremshiwa Qur-an yote kwa mara moja? Kama hivi (mnavyoona, tumeiteremsha kidogo kidogo) ili tuuthibitishe, (tuutie nguvu), moyo wako (kwa hizo aya mpya mpya zinazoteremshwa wakati baada ya wakati) na tumeipanga kwa uzuri. (25:32)


Hakika sisi tumekuteremshia Qur-an sehemu sehemu (kidogo kidogo). (76:23).
Kama inavyoonekana katika aya hizi. Qur-an imeshushwa kidogo kidogo ili iwe wepesi kwa Mtume Muhammad (s.a.w) kuufikisha ujumbe uliotangulia kwa ukamilifu kinadharia na kimatendo kabla ya ujumbe mwingine uliofuata.



Kwa upande mwingine Qur-an imeshuka kidogo kidogo ili kuwawezesha waumini wa mwanzo kuihifadhi Qur-an kwa wepesi, kuyaelewa fika mafundisho yake kinadharia na kuwawezesha kuitekeleza Qur-an katika kila kipengele cha maisha yao ili wawe jamii bora ya kuigwa na jamii zitakazofuatia.



Kushuka Qur-an kidogo kidogo kwa muda wa miaka 23 ni hoja nyingine kuwa Qur-an ni Kitabu cha Allah (s.w). Kwa yeyote yule anayeisoma Qur-an kwa makini na akajua mpangilio wake wa aya na sura kama vile sura moja kuwa na mchanganyiko wa aya za mwanzo na zilizoshushwa mwishoni lakini bado kunapatikana mtiririko mzuri wa maudhui na mpangilio wa sura usiofuata mtiririko wa kushuka, utaona kuwa haiyumkiniki kuwa Qur-an ni Kitabu kilichoandikwa na Mtume Muhammad (s.a.w) kama wanavyodai makafiri.


Pia Qur-an ingelikuwa imeandikwa na Mtume Muhammad (s.a.w) isingelichukua muda wote huo, bali ingelibidi aiandike yote kwa muda mfupi ili aweze kuitumia katika kazi yake ya kuwaongoza watu. Ni kawaida kuwa ili kufanikiwa katika utekelezaji wa jambo lolote ni lazima kwanza pawe na nadharia nzuri inayoelekeza namna ya utekelezaji. Halikadhalika, Mtume Muhammad (s.a.w) aliyekuwa kiongozi wa Dola ambaye mfano wake haujapatikana, asingeliweza kufanya kazi nzito na kubwa kiasi hicho bila ya kuwa na nadharia ya kumwongoza. Hivyo, kwa kutokuwa na Qur-an yote mkononi mwake ili kuitumia katika kila hatua ya kazi yake, inadhihirisha kuwa alikuwa akiletewa mwongozo kutoka kwa Allah(sw) katika kila hatua ya kazi yake mpaka alipoikamilisha.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 770


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

HUKUMU ZA QALQALA
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

MAANA YA Quran
Maana na majina ya Quran Maana ya Wahyi. Soma Zaidi...

HUKUMU ZA MADD
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

quran na sayansi
Soma Zaidi...

Tafsiri na mafunzo ya sura zilizochaguliwa - Saratul-fiyl
Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mtume Muhammad hakujuwa kusoma wala kuandika ni hoja na kuna hekima zake
(i)Mtume Muhammad (s. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al-Falaq na surat an-Nas na fadhila za kusoma sura hizi
SURAT AL-MUAWIDHATAYN (SURAT AL-FALAQ NA SURATUN-NAS) Inaelezwa kuwa sura mbili hizi zilishuka pamoja, na maulamaa wanaelezea kuwa Mtume (s. Soma Zaidi...

Hukumu za Idh-har na id-gham katika laam al-maarifa
Laam al- maarifa inaweza kusomwa kwa idgham au idh-har pindibitakapokutana na herufi za shamsiya au qamariya. Soma Zaidi...

Kitabu Cha Darsa za Quran
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

Fadhila za kusoma surat al Baqarah
Surat al Baqarah ni katika sura ambazo tunapaswa tuwe tunasoma mara kwa mara. Post hii itakufundisha kuhusu fadhila za sura hii. Soma Zaidi...

quran na sayansi
YALIYOMONENO LA AWALI1. Soma Zaidi...

Quran si maneno ya mwenye kifafa
Soma Zaidi...