picha

Kujiepusha na Kibri na Majivuno

Kujiepusha na Kibri na Majivuno

(h) Kujiepusha na Kibri na Majivuno



"Wala usiwatizame watu kwa upande mmoja wa uso (usiwafanyie watu jeuri) Wala usiende katika nchi kwa maringo; Hakika Mwenyezi Mungu hampendi kila ajivunaye, ajifaharishaye" (31:18)



"Wala usitembee (usiende) katika ardhi kwa maringo. Hakika wewe huwezi kuipasua ardhi wala huwezi kufikia urefu wa mlima. Haya yote ubaya wake ni wenye kuchukiza mbele ya Mola wako" (17:37-38)



Kibri ni tabia ya kukataa ukweli na kuwadharau watu kama tu navyoj ifu nza katika Hadithi ifuatayo:
"Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa, Mtume wa Allah am esem a, "Yule ambaye moyoni mwake mnachembe ya kibri hataingia peponi" Swahaba mmoja akauliza: "Je kama mtu anapenda nguo nzuri na viatu?" Mtume (s. a.w) akasema, "Allah (s.w) ni mzuri na anapenda vizuri. Kibri ni kukataa ukweli na kupuuza watu ". (Muslimu)



Vile vile kibri na majivuno ni tabia ya kishirikina kama tunavyojifunza katika Hadithi nyingine ifuatayo:


"Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema; Allah akasema; Utukufu ni nguo yangu na kibri ni kilemba changu. Yeyote atakaye shindania kimoja wapo katika hivi ataangamia." (Muslimu)



Mtu mwenye kibri na majivuno daima atakuwa ni mpinzani wa harakati za kusimamisha Uislamu katika ardhi, kwani atapendelea utawala ule ambao utamfanya kuwa mungu katika jamii.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Views 2394

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 web hosting     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Nini chanzo cha elimu zote na ujuzi wote

Ninichanzo cha Elimu? (EDK form 1 Dhanaya Elimu)

Soma Zaidi...
Mtazamo wa Uislamu juu ya maana ya dini

Uislamu unaitazama dini katika nyanja zote za maisha ya mwanadamu. Hii ni tofauti na mtazamo wa kikafiri juu ya dini.

Soma Zaidi...
Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu

Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo: (i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu.

Soma Zaidi...
Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)

"Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu

Soma Zaidi...
Elimu Yenye Manufaa

Kwenye kipengele hiki tutajifunza elimu yenye manufaa kwenye jamii na pia tutajifunza sifa za elimu yenye manufaa.

Soma Zaidi...