Kujiepusha na Kibri na Majivuno

Kujiepusha na Kibri na Majivuno

Kujiepusha na Kibri na Majivuno

(h) Kujiepusha na Kibri na Majivuno



"Wala usiwatizame watu kwa upande mmoja wa uso (usiwafanyie watu jeuri) Wala usiende katika nchi kwa maringo; Hakika Mwenyezi Mungu hampendi kila ajivunaye, ajifaharishaye" (31:18)



"Wala usitembee (usiende) katika ardhi kwa maringo. Hakika wewe huwezi kuipasua ardhi wala huwezi kufikia urefu wa mlima. Haya yote ubaya wake ni wenye kuchukiza mbele ya Mola wako" (17:37-38)



Kibri ni tabia ya kukataa ukweli na kuwadharau watu kama tu navyoj ifu nza katika Hadithi ifuatayo:
"Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa, Mtume wa Allah am esem a, "Yule ambaye moyoni mwake mnachembe ya kibri hataingia peponi" Swahaba mmoja akauliza: "Je kama mtu anapenda nguo nzuri na viatu?" Mtume (s. a.w) akasema, "Allah (s.w) ni mzuri na anapenda vizuri. Kibri ni kukataa ukweli na kupuuza watu ". (Muslimu)



Vile vile kibri na majivuno ni tabia ya kishirikina kama tunavyojifunza katika Hadithi nyingine ifuatayo:


"Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema; Allah akasema; Utukufu ni nguo yangu na kibri ni kilemba changu. Yeyote atakaye shindania kimoja wapo katika hivi ataangamia." (Muslimu)



Mtu mwenye kibri na majivuno daima atakuwa ni mpinzani wa harakati za kusimamisha Uislamu katika ardhi, kwani atapendelea utawala ule ambao utamfanya kuwa mungu katika jamii.




                   


Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Views: 3011

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Elimu ya mwingozo na elimu ya mazingira katika uislamu

Mahusiano kati ya elimu ya mwongizo na elimu ya mazingira katika uislamu.

Soma Zaidi...
Lengo la kushushwa vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sifa za waumini zilizotajwa katika surat ash-Shuura

“Basi vyote hivi mlivyopewa ni starehe ya maisha ya dunia tu, lakini kilicho kwa Mwenyezi Mungu ni bora na cha kudumu (milele).

Soma Zaidi...