Kujiepusha na Kibri na Majivuno
(h) Kujiepusha na Kibri na Majivuno
"Wala usiwatizame watu kwa upande mmoja wa uso (usiwafanyie watu jeuri) Wala usiende katika nchi kwa maringo; Hakika Mwenyezi Mungu hampendi kila ajivunaye, ajifaharishaye" (31:18)
"Wala usitembee (usiende) katika ardhi kwa maringo. Hakika wewe huwezi kuipasua ardhi wala huwezi kufikia urefu wa mlima. Haya yote ubaya wake ni wenye kuchukiza mbele ya Mola wako" (17:37-38)
Kibri ni tabia ya kukataa ukweli na kuwadharau watu kama tu navyoj ifu nza katika Hadithi ifuatayo:
"Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa, Mtume wa Allah am esem a, "Yule ambaye moyoni mwake mnachembe ya kibri hataingia peponi" Swahaba mmoja akauliza: "Je kama mtu anapenda nguo nzuri na viatu?" Mtume (s. a.w) akasema, "Allah (s.w) ni mzuri na anapenda vizuri. Kibri ni kukataa ukweli na kupuuza watu ". (Muslimu)
Vile vile kibri na majivuno ni tabia ya kishirikina kama tunavyojifunza katika Hadithi nyingine ifuatayo:
"Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema; Allah akasema; Utukufu ni nguo yangu na kibri ni kilemba changu. Yeyote atakaye shindania kimoja wapo katika hivi ataangamia." (Muslimu)
Mtu mwenye kibri na majivuno daima atakuwa ni mpinzani wa harakati za kusimamisha Uislamu katika ardhi, kwani atapendelea utawala ule ambao utamfanya kuwa mungu katika jamii.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
KAZI ZA MALAIKA
Malaika wamepewa kazi ya kumtumikia Allah(SW) kwa kumtukuza na kumtakasa, kama wanavyosema wenyewe:Hakuna yoyote miongoni mwetu ila anapo mahali pake mahususi.
Soma Zaidi...Maana ya Elimu katika uislamu na nani aliye elimika?
Hili ni swali kutoka katika maarifa ya elimu ya dini ya kiislamu kidato cha kwanza (EDK FORM 1)
Soma Zaidi...Lengo la kushushwa vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Sifa za waumini zilizotajwa katika surat As-Sajida
Nao husema (kwa maskhara): "Je, tutakapopotea katika ardhi, (tukageuka mchanga) ndio tutarudishwa katika umbo jipya?
Soma Zaidi...