Kutopupia dunia

"Ewe mwanangu!

Kutopupia dunia

(e) Kutopupia dunia



"Ewe mwanangu! Kwa hakika jambo lolote lijapokuwa na uzito wa chembe ya hardali, likawa ndani ya jabali au mbinguni au katika ardhi, Mwenyezi Mungu Atalileta (amlipe aliyefanya); bila shaka Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mambo yaliyofichikana, (na) Mjuzi wa mambo yaliyo dhahiri"(31:16).



Aya hii inatuhakikishia kuwa kila mtu amekadiriwa jambo lake na hapana yeyote na hila yoyote itakayomzuia mtu asipate kile alichokadiriwa kukipata au kumuwezesha mtu kupata kile ambacho hakukadiriwa. Pia aya ifuatayo inatuweka wazi zaidi:


β€œNa hakuna mnyama yoyote (kiumbe chochote) katika ardhi ila riziki yake iko juu ya Mwenyezi Mungu….. " (11:6)



Kutokana na aya hii tunajifunza kuwa lengo la maisha yetu si kutafuta rizki na maslahi ya dunia bali vitu hivi ni vitendea kazi tu vyakutuwezesha kulifikia lengo kuu. Lengo letu kuu ni kuusimamisha Uislamu katika jamii ili tuweze kumuabudu Allah (s.w) ipasavyo katika kila kipengele cha maisha yetu ya kibinafsi na ya kijamii ambalo ndilo lengo la kuumbwa kwetu.



Hivyo katika mchakato wa kuliendea lengo hili la kusimamisha Uislamu katika jamii, tusimchelee yeyote wala


tusichelee kupoteza chochote kwani hamna mwenye uwezo wa kutupokonya au kutuzidishia chochote kile kinyume na alivyotukadiria Allah (s.w). Katika hili ni vyema tukazingatia pia aya ifuatayo:


Hautokei msiba katika ardhi wala katika nafsi zenu ila umekwishaandikwa katika Kitabu (cha Mwenyezi Mungu) kabla Hatujaumba. Kwa yakini hili ni sahali kwa Mwenyezi Mungu." (57:22).




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 872

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰2 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰5 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Ni lipi lengo la Elimu katika yislamu?

Ni lipi lengo kuu la Elimu katika uislamu (Edk form 1 Dhanaya Elimu)

Soma Zaidi...
KUAMINI MALAIKA

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Umbile la mbingu na ardhi linavyothibitisha uwepo wa Allah

Allah anatutaka kuchunguza umbile na mbingu na ardhi ili kupata mazingatio.

Soma Zaidi...
Kwa namna gani Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia ndoto.

Ndoto za kweli ni moja kati ya njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu.

Soma Zaidi...
Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu

Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu Ni upi? (EDK form 1: mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu)

Soma Zaidi...
Kujiepusha na Shirk

Shirki ni kitendo chochote cha kukipa kiumbe nafasi ya Allah (s.

Soma Zaidi...