Kusimamisha Swala na kuamrisha mema

Swala iliyosimamishwa vilivyo ndiyo nyenzo kuu ya kumtakasa Muislamu na kumpa sifa zinazomuwezesha kustahiki kufanya kazi takatifu ya kusimamisha Uislamu katika jamii.

Kusimamisha Swala na kuamrisha mema

(f)Kusimamisha Swala



Swala iliyosimamishwa vilivyo ndiyo nyenzo kuu ya kumtakasa Muislamu na kumpa sifa zinazomuwezesha kustahiki kufanya kazi takatifu ya kusimamisha Uislamu katika jamii. Swala ikisimamishwa vilivyo humuwezesha mja kumcha Allah (s.w) ipasavyo katika kukiendea kila kipengele cha maisha yake ya kibinafsi na pia ni msingi wa kumpelekea mja kusimamisha Uislamu katika jamii.



(g)Kuamrisha mema na kukataza mabaya na kusubiri juu yale yatakayokusibu
Kuamrisha mema na kukataza maovu ni masuala yanayohitaji mamlaka na nguvu (authority and power). Hata hivyo kuwa na mamlaka na nguvu sio lazima ianzie kileleni katika ngazi ya Dola, bali mamlaka na nguvu ya kuamrisha mema na kukataza mabaya huanzia kwa mtu binafsi, kisha kwa familia yake kisha kwa ndugu na jamaa zake wa karibu. Kuamrisha mema na kukataza maovu ni wajibu kwa waumini wote (Qur'an 3:104, 3:110, 8:25, n.k).



Kuamrisha mema na kukataza maovu ni suala la mapambano hata katika ngazi ya mtu binafsi na katika ngazi ya familia. Ni shughuli inayohitajia kuwa na subira ya hali ya juu. Subira ina maana pana ikiwa ni pamoja na:


1.Wewe mwenye kubakia na msimamo wa kufanya mema na kujiepusha na maovu
2.Kuwahimiza na kuendelea kuwashupalia kufanya mema
na kuacha maovu wale ambao unamamlaka juu yao.
3.Kuwa tayari kulaumiwa na yeyote atakayelaumu.
4.Kuwa tayari kukabiliana na magumu yoyote
yata kayo kufika.
5.Kutotarajia kupata matunda ya haraka haraka kutokana na kazi ya kuamrisha mema na kukataza mabaya.




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 618

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Tofauti kati ya hijjah na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nguzo za udhu ni sita

Post hii itakufundisha kuhusu nguzo kuu sita za udhu.

Soma Zaidi...
Lengo la kusimamisha swala

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kufanya suluhu kati ya mume na mke.

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kufanya suluhu katika ndoa.

Soma Zaidi...
udhaifu wa hoja za kuunga mkono kuzibiti uzazi na uzazi wa mpango

Udhaifu wa Hoja za Kudhibiti Uzazi:Hoja nyingi zinazotolewa kuunga mkono udhibiti wa uzazi zimejengwa juu ya hali na mazingira ya maisha yaliyoletwa na utamaduni na maendeleo ya nchi za Ulaya na Marekani.

Soma Zaidi...
benki za kiislamu na njia zake za kuingiza kipato

Benki za KiislamuBenki za Kiislamu ambazo hutoa huduma kama benki nyingine zinaendeshwa katika msingi wa biashara na sio ule wa riba.

Soma Zaidi...