Swala iliyosimamishwa vilivyo ndiyo nyenzo kuu ya kumtakasa Muislamu na kumpa sifa zinazomuwezesha kustahiki kufanya kazi takatifu ya kusimamisha Uislamu katika jamii.
Swala iliyosimamishwa vilivyo ndiyo nyenzo kuu ya kumtakasa Muislamu na kumpa sifa zinazomuwezesha kustahiki kufanya kazi takatifu ya kusimamisha Uislamu katika jamii. Swala ikisimamishwa vilivyo humuwezesha mja kumcha Allah (s.w) ipasavyo katika kukiendea kila kipengele cha maisha yake ya kibinafsi na pia ni msingi wa kumpelekea mja kusimamisha Uislamu katika jamii.
(g)Kuamrisha mema na kukataza mabaya na kusubiri juu yale yatakayokusibu
Kuamrisha mema na kukataza maovu ni masuala yanayohitaji mamlaka na nguvu (authority and power). Hata hivyo kuwa na mamlaka na nguvu sio lazima ianzie kileleni katika ngazi ya Dola, bali mamlaka na nguvu ya kuamrisha mema na kukataza mabaya huanzia kwa mtu binafsi, kisha kwa familia yake kisha kwa ndugu na jamaa zake wa karibu. Kuamrisha mema na kukataza maovu ni wajibu kwa waumini wote (Qur'an 3:104, 3:110, 8:25, n.k).
Kuamrisha mema na kukataza maovu ni suala la mapambano hata katika ngazi ya mtu binafsi na katika ngazi ya familia. Ni shughuli inayohitajia kuwa na subira ya hali ya juu. Subira ina maana pana ikiwa ni pamoja na:
1.Wewe mwenye kubakia na msimamo wa kufanya mema na kujiepusha na maovu
2.Kuwahimiza na kuendelea kuwashupalia kufanya mema
na kuacha maovu wale ambao unamamlaka juu yao.
3.Kuwa tayari kulaumiwa na yeyote atakayelaumu.
4.Kuwa tayari kukabiliana na magumu yoyote
yata kayo kufika.
5.Kutotarajia kupata matunda ya haraka haraka kutokana na kazi ya kuamrisha mema na kukataza mabaya.
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa
Mwandhishi Tarehe 2018-08-01 Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 125
Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani
👉2 Kitau cha Fiqh
👉3 Kitabu cha Afya
👉4 kitabu cha Simulizi
Kujiepusha na kukaribia zinaa
Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa. Soma Zaidi...
MAFUNZO YA SWALA: NGUZO ZA SWALA, SHARTI ZA SWASL, FADHILA ZA SWALA, HUKUMU YA MWENYE KUACHA SWALA
Soma Zaidi...
UTARATIBU WA KULEA MIMBA
Soma Zaidi...
NYAKATI AMBAZO DUA HUJIBIWA
NYAKATI AMBAZO DUA HUJUBIWA. Soma Zaidi...
Hadithi Ya 33: Jukumu La Ushahidi Liko Kwa Yule Anayedai Na Kula Kiapo Kunamuwajibikia Yule Anayekana
Soma Zaidi...
quran na sayansi
YALIYOMONENO LA AWALI1. Soma Zaidi...
Masharti ya swala
Sharti za SwalaSharti za Swala Sharti za swala ni yale mambo ya lazima anayotakiwa Muislamu ayachunge na kuyatekeleza kabla hajaanza kuswali. Soma Zaidi...
Imam Abu Daud na Sunan Abi Daud
Soma Zaidi...
Kujiepusha na kukaribia zinaa
Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa. Soma Zaidi...
hizi ndio nguzo za swala, swala za faradhi na suna
Soma Zaidi...
Hadithi Ya 41: Hatoamini Mmoja Wenu Mpaka Mapenzi Yake Yatakapomili (yatakapoendana) Na Yale Niliyokuja Nayo
Soma Zaidi...