Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Zifuatazo ni athari za muumini wa kweli juu ya imani ya malaika katika kila kipengele cha maisha ya kila siku;
Kwanza, imani ya kweli juu ya Malaika humuepusha na kumshirikisha Mwenyezi Mungu (s.w) na viumbe wake hasa wale wasioonekana kama Malaika, majini, n.k.
Rejea Qur’an (37:149-154), (43:16-19) na (21:26-27).
Pili, imani juu ya malaika huchochea mja kufanya ibada kwa bidii na kujiepusha na maovu na machafu ili kupata cheo kama malaika au zaidi.
Tatu, imani juu ya malaika pia humfanya mtu kuepuka kufanya maovu popote alipo na muda wowote kwa kujua kuwa yupo pamoja na malaika.
Nne, Mja anapoamini kuwa malaika huandika na kuhudhurisha vitendo vyake kwa Mwenyezi Mungu (s.w), hufanya bidii katika kufanya mema zaidi na kuepuka maovu kadri ya uwezo wake.
Tano, Muumini anapoamini kuwa malaika humuombea maghufira kwa Mwenyezi Mungu (s.w), hufanya bidii katika kuzidisha mema na kuepuka maovu kadri awezavyo ili kupata msamaha wa Mwenyezi Mungu (s.w) zaidi.
Rejea Qur’an (17:13-14) na (18:49).
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Kwa nini uislamu ndio dini pekee ya haki ambayo watu wanatakiwa waifuate.
Soma Zaidi...Kwa hakika binaadamu ameumbwa, hali ya kuwa mwenye pap atiko.
Soma Zaidi...عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "مَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاَللَّهِ وَالْيَوْمِ...
Soma Zaidi...Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kamili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi..."Hakika wanaoamini kweli ni wale ambao anapotajwa Allah nyoyo zao hujaa khofu; na wanaposomewa aya zake huwazidishia imani na wanamtegemea Mola wao tu basi.
Soma Zaidi...