Sifa za wuamini zilizotajwa katika surat Al-ma'aarij

Kwa hakika binaadamu ameumbwa, hali ya kuwa mwenye pap atiko.

Sifa za wuamini zilizotajwa katika surat Al-ma'aarij

Sifa za wuamini zilizotajwa katika surat Al-ma'aarij


Kwa hakika binaadamu ameumbwa, hali ya kuwa mwenye pap atiko. Inapomgusa shari huwa mwenye fadhaa. Na inapomgusa kheri huwa anaizuilia. Ila wanaosali; (hao hawana sifa mbaya). Ambao wanadumisha Sala zao. Na ambao katika mali zao iko sehemu maalumu. (70:19-24)


Kwa ajili ya aombaye na anayejizuilia kuomba (japo muhitaji). Na ambao wanasadiki siku ya Malipo. Na ambao wanaiogopa adhabu (itokayo) kwa Mola wao. Hakika adhabu ya Mola wao si ya kusalimika nayo mtu (mbaya). Na ambao wanahifadhi tupu zao. (70:25-2 9)


Isipokuwa kwa wake zao au wale iliyowamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi. Lakini wanaotaka kinyume cha haya, basi hao ndio wanaoruka mipaka. Na ambao wanaangalia amana zao na ahadi zao . Na ambao ni imara katika ushahidi wao. Na ambao wanazihifadhi Swala zao Hao ndio watakaokuwa katika Mabustani wakihishimiwa. (70:30-35)



Mafunzo
Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa:
Kwanza, binaadamu ameumbwa na udhaifu mwingi. Miongoni mwa udhaifu alionao ni kuwa anapofikwa na jambo lolote la shari hushikwa na huzuni kubwa na kukata tamaa; lakini akipata kheri kidogo, hujivuna na kuwa bahili.
Pili, mwanaadamu ataepukana na udhaifu mwingi alionao ambao humdunisha na kumshusha chini kuliko vilivyo chini, pale tu atakapokuwa Muumini wa kweli anayefanya vitendo vizuri ikiwa ni pamoja na:



(i)Kusimamisha swala kwa kuzihifadhi(kuteleleza vilivyo sharti na ngozo zake), kuziswali kwa unyenyekevu na kudumu nazo katika maisha yote.

(ii)Kutoa mali na kuwasaidia wanaadamu wenziwe wanaohitajia baada ya kupatwa na shida mbali mbali.

(iii)Kusadikisha au kuwa na yakini kuwa atarejea kwa Mola wake.

(iv)Kuogopa adhabu ya Allah(sw) kwa kujiepusha na yale yote yanayomghadhibisha Allah(sw) na kuomba mara kwa mara kuepushwa na moto (25:65 - 66)

(v)Kuhifadhi tupu kwa kujiepusha mbali na zinaa na vishawishi vyake vyote.

(vi)Kuchunga amana zote na amana kuu ikiwa ni ile ya Ukhalifa aliyotunukiwa na Allah (s.w) kama tu navyoku m bushwa kati ka aya ifuatayo:



"Kwa yakini tulitoa amana (ya Ukhalifa) kwa mbingu na ardhi na milima vikakataa kuichukua na vikaogopa, lakini mwanaadamu akaichukua.Bila shaka yeye ni dhalimu mkubwa (kwa kuhini amana aliyopewa na Mola wake) mjinga sana." (33:72)



(vii) Kuchunga ahadi zote anazotoa kwa watu na kwa Allah (s.w). Ahadi kuu aliyoitoa muumini kwa Allah (s.w) ni ile ya "shahada mbili" pale anapoahidi kuwa hatamshirikisha Allah (s.w) na mungu yeyote na kuwa ataishi kwa kufuata sunnah ya Mtume Muhammad (s.a.w).



(viii)Kuwa imara katika ushahidi au katika kusimamia haki. Muumini wa kweli ni yule asiyehofu chochote katika kusimamia haki.




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 667

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰3 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Mtazamo wa uislamu juu ya dini

Kwenye kipengele hichi tutajifunza mitazamo ya kikafiri juu ya dini.

Soma Zaidi...
Mtazamo wa Uislamu juu ya maana ya dini

Uislamu unaitazama dini katika nyanja zote za maisha ya mwanadamu. Hii ni tofauti na mtazamo wa kikafiri juu ya dini.

Soma Zaidi...
Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na sababu zifuatazo

Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na nini? (EDK form 1: mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na sababu zifuatazo)

Soma Zaidi...
Athari za vita vya Uhud

Vita vya uhudi viliweza kuleta athari nyingi. Post hii itakuletea athari baadhi za vita hivyo.

Soma Zaidi...
Nini chanzo cha elimu zote na ujuzi wote

Ninichanzo cha Elimu? (EDK form 1 Dhanaya Elimu)

Soma Zaidi...
Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu

Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo: (i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu.

Soma Zaidi...
Kwa nini Uislamu ndio dini pekee inayostahiki kufuatwa

Kwa nini uislamu ndio dini pekee ya haki ambayo watu wanatakiwa waifuate.

Soma Zaidi...
Ni lipi lengo la Elimu katika yislamu?

Ni lipi lengo kuu la Elimu katika uislamu (Edk form 1 Dhanaya Elimu)

Soma Zaidi...