Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)

"Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu

Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)

(d)Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)


"Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu ni kwangu, hapo nitakuambieni mliyokuwa mkiyatenda." (31:15).



Aya inabainisha wazi kuwa hatupaswi kuwatii wazazi wetu pale watakapotuamrisha kumuasi Allah (s.w). Tukiwatii tutakuwa tumemshirikisha Allah (s.w) kwa kuwafanya wazazi wetu miungu badala yake kama inavyo bainika katika Qur'an.



'Mayahudi na Wakristo) wamewafanya wanavyuoni wao na watawa wao kuwa ni miungu badala ya Allah (s.w) '." (9:31)



Iliposhushwa aya hii Adi bin Hatimu (r.a) ambaye alisilimu kutoka kwenye Ukristo, alimtaka Mtume (s.a.w) atoe ufafanuzi kwa sababu alidai kuwa kinadharia hawakuwa wanawafanya watawa wao miungu. Katika kufafanua, Mtume (s.a.w) alimuuliza Adi, "Je hawakuwa watawa wenu wanawahalalishia alivyo viharamisha Allah (s.w) na nyinyi mkawatii?" Alijibu Adi, "Ndiyo" Mtume (s.a.w) akamuuliza tena, "Je watawa wenu hawakuwa wanakuharamishieni alivyo halalisha Allah (s.w) na nyinyi mkawatii? Adi akajibu tena "Ndiyo." Basi Mtume (s.a.w) akasema, "Huko ndio kuwafanya miungu".



Hivyo, kumtii mzazi au kiongozi au yeyote yule katika kumuasi Allah (s.w) ni kumfanya mungu badala ya Allah (s.w). Pia ukitii matashi ya nafsi yako kinyume na amri au makatazo ya Allah (s.w) utakuwa umeifanya nafsi yako mungu badala ya Allah (s.w).


"Je, umemuona yule aliyefanya matamanio yake, (kile anachikipenda), kuwa Mungu wake? Basi je, utaweza kuwa mlinzi wake (ukamhifadhi na hayo, na hali ya kuwa hataki?). "(25:43).



Lakini, tunaamrishwa katika aya hii (31:15) kuwa pamoja na kutowatii wazazi wetu katika kumshirikisha Allah (s.w), tusiwe jeuri na fedhuli kwao, bali tuzungumze nao kwa upole kwa kauli njema na tuendelee kuwatii na kuwafanyia wema katika mambo yote ya halali.


Wakati mwingine wazazi wanaweza kutishia kuacha laana tutakapowakatalia kwa kauli nzuri kutowatii katika yale yatakayotupelekea kumuasi na kumshirikisha Allah (s.w). Tusiyumbishwe na tishio hili kwa sababu marejeo yetu sote ni kwa Allah (s.w) na ni mjuzi kamili juu ya dhamira (nia) zetu na vitendo vyetu - "'kisha marejeo yenu ni kwangu, Hapo nitakuambieni mliyokuwa mkiyatenda" (31:15).




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 151


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

KUAMINI MITUME WA ALLAH (S.W)
Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya Mitume wa Allah (s. Soma Zaidi...

Je inafaha kuingizwa eda na kutolewa?
Kuingizwa au Kutolewa EdaKatika sheria ya Kiislamu hapana suala Ia kuingizwa au kutolewa eda na Sheikh. Soma Zaidi...

Vita vya wenyewe kwa wenyewe baada ya kif cha khalifa Uthman
Soma Zaidi...

quran na sayansi
2; mbegu ya uhai uliyo changanyikaUmbile la mwanadamu limepitia hatua nyingi sana kama tutakavyoendelea mbele kuonalakini ukiachilia mbali na hatua zote alizopitia mwanadamu wakati wa kuumbwa lakiniumbile la mwanadamu bado limebakia kuwa dhalili kama ALLA Soma Zaidi...

Ni yapi mambo yanayoharibu Swaumu na Mambo yanayobatilisha funga
Soma Zaidi...

Historia ya Luqman mtu aliyesifika kuwa na Hikma
Luqman ni katika watu wema kabisa waliopita zama za nyuma. Soma Zaidi...

Nini maana ya Uchoyo, na madhara yake kwenye jamii
31. Soma Zaidi...

zijue Nguzo za uislamu, imani, ihsani pamoja na dalili za qiyama
' ' ' ' ' ' ': " ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ?... Soma Zaidi...

MASHARTI YA KUKUBALIWA KWA DUA
MASHART YA KUKUBALIWA KWA DUA. Soma Zaidi...

Maryam Apewa Habari ya Kumzaa Isa(a.s)
Baada ya maandalizi hayo ya kimalezi pamoja na hifadhi ya Allah(s. Soma Zaidi...

USULUHISHWAJI KWA WALODHULUMIWA
Download kitabu Hiki Bofya hapa USULUHISHAJI WA WALODHULUMIWA. Soma Zaidi...

DUA 120
Soma Zaidi...