image

Nafsi ya mwanadamu inavyothinitisha uwepo wa Allah

Mwanadamu ukifikiria vyema. Kuhusu nafsi yako, hakika utapatabfikra yabuwepp wa Mwenyezi Mungu

Nafsi ya mwanaadamu

“Na katika ardhi zipo (alama namna kwa namna za kuonyesha kuwepo Allah (s.w) kwa wenye akili. Na katika nafsi zenu (pia zimo ishara hizo)Je, hamuoni?” (51:20-21)

Ukimtafakari mwanaadamu utapata dalili nyingi zinazothibitisha kuwepo kwa Allah (s.w). Maeneo ya kutafakari ni pamoja na:

 

(i) Chanzo na mwisho wa uhai wa mwanaadamu“Vipi mnamkanusha Allah (s.w) na hali mlikuwa wafu, akakuhuisheni, kisha atakufisheni, kisha atakurudisheni (tena) kisha kwake mtarejeshwa” (2:28)“Basi mbona (roho) ifikapo kooni, na nyinyi wakati ule mnamtazama. (56:83-84)Nasi tunakaribiana naye zaidi (huyo anayetoka roho) kuliko nyinyi, wala nyinyi hamuoni. (56:85)Kama nyinyi hamumo katika mamlaka (yangu), kwanini hamuirudishi (hiyo roho) ikiwa mnasema kweli?” (56:86-8 7).

 

(ii)Asili ya mwanaadamu “Na katika ishara zake (za kuonyesha kuwepo kwake) ni huku kukuumbeni kwa udongo kisha mnakuwa watu mnaoenea (kila mahali).” (30:20)

 

(iii)Kuumbwa Wanaume na Wanawake “Je! Anafikiri binaadamu kuwa ataachwa bure (asipewa amri za Mwenyezi Mungu wala makatazo yake)? Je, hakuwa tone la manii lililotonwa? (75:36-37).Kisha akawa kidonge cha damu, kisha akamuumba na akamsawazisha, kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.(75:38-39).Je! Hakuwa huyo ni muweza wa kuhuisha wafu?” (75:40). “Na katika ishara zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu katika jinsi yenu ili mpate utulivu kwao, naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. Bila shaka katika haya ziko alama (za kuwepo Allah) kwa watu wanaofikiri” (30:21)

 

(iv) Tofauti ya Lugha, Rangi, Makabila, Mataifa “Na katika ishara zake (za kuonyesha kuwepo kwake na uwezo wake) ni kuumba mbingu na ardhi na kuhitalifiana lugha zenu na rangi zenu. Kwa yakini katika haya zimo ishara kwa wenye ujuzi” (30:22).

 

“Enyi w atu! Kwa hakika tumekuumbeni (nyote) kw a (yule) mw anamume (mmoja Adam) na (yule) mwanamke (mmoja Hawwa). Na tumekufanyeni mataifa na makabila (mbali mbali) ili mjuane (tu basi). Hakika aheshimiwaye sana miongoni mw enu mbele ya Allah ni yule amchaye Allah zaidi katika nyinyi. Kwa yakini Allah ni Mjuzi Mwenye habari (za mambo yote).” (49:13)

 

(v) Umbo na Sura “Ewe mwanaadamu! Nini kikudanganyacho na Mola wako Mtukufu (hata ukamkanusha). Aliyekuumba na akakutengeneza, kisha akakulinganisha sawasawa. Katika sura yoyote aliyoipenda amekutengeneza ”. “Na katika umbo lenu na katika viumbe alivyovitawanya zimo alama kwa watu wenye yakini.” (45:4)

 

(vi)Chakula cha Mwanaadamu “Hebu mwanaadam na atazame chakula chake. Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu (kutoka maw inguni).Tena tukaipasuapasua ardhi.Kisha Tukaotesha humo (vyakula vilivyo) chembe chembe. Na mizabibu na mboga. Na mizeituni na mitende.Na mabustani, (mashamba) yenye miti iliyosongamana barabara.Na matunda na malisho.Kwa ajili ya kukustarehesheni nyinyi na wanyama wenu. (80:24-32)

 

(vii)Ufanyaji kazi wa viungo vya ndani na nje ya mwili wa Mwanaadamu

 

 

“Basi uelekeze uso wako katika dini iliyo sawasawa - ndilo umbile Mwenyezi Mungu alilowaumbia watu; (yaani dini hii ya Kiislamu inawafikiana barabara na umbo la binaadamu).Hakuna mabadiliko katika maumbile ya viumbe vya Mw enyezi Mungu. Hiyo ndiyo dini iliyo haki, lakini w atu w engi haw ajui.”

 

(30:30) “Na katika ishara zake ni kulala kwenu usiku na kuamka mchana na kutafuta fadhila Yake. Hakika katika hayo zimo ishara kwa wenye kusikia.(30:23)

 

Mwanadamu japo analala kila siku, hajui chanzo cha usingizi. Mtu anapokuwa usingizini hajui chochote kinachoendelea, Je! ni nani anayeleta usingizi na kuuondoa?

 

(ix) Mwanadamu kumkumbuka Allah (s.w) wakati wa matatizo“Sema: Ni nani anayekuokoeni katika viza (taabu) vya bara na baharini? Mnamuomba kwa unyenyekevu na kwa sauti ndogo (mnasema): Kama akituokoa katika (baa) hii bila shaka tutakuwa miongoni mwa wanaoshukuru (6:63)

 

Hata Fir’auni, aliyetakabari sana kiasi cha kudai kuwa yeye ni mkubwa kuliko Allah, alimkumbuka Mola wake pale alipokabiliwa barabara na matatizo.“Na tukawapitisha wana wa Israel katika bahari, na Firauni na majeshi yake wakawafuata kwa dhulma na jeuri. Hata kulipomfikia Fir’aun kuzama alisema, “Naamini kwamba hakuna aabudiw aye kwa haki ila yule wanayemuamini wana wa Israel na mimi ni miongoni mwa wanaotii”. (10:90)

 

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1148


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Kwa nini uislamu umeipa elimu nafasi ya kwanza
Elimu imepewa nafasi kubwa sana katika uislamu. Soma Zaidi...

Sababu za kutokubalika kwa vitabu vilivyotumwa kuwa muongozo sahihi wa maisha ya mwanadamu zama hizi
Soma Zaidi...

Elimu Yenye Manufaa
Kwenye kipengele hiki tutajifunza elimu yenye manufaa kwenye jamii na pia tutajifunza sifa za elimu yenye manufaa. Soma Zaidi...

Ni yupi mtume wa mwisho? na je ni kwa nini Muhammad ndiye mtume wa mwisho?
Soma Zaidi...

maana ya dini
Soma Zaidi...

Maadili na malezi ya jamii
Soma Zaidi...

Mtazamo wa uislamu juu ya dini
Kwenye kipengele hichi tutajifunza mitazamo ya kikafiri juu ya dini. Soma Zaidi...

Muumini ni yule ambaye anazungumza ukweli
Ukweli ni katika sifa za waumini. Siku zote hakuna hasara katika kusema ukweli. Kinyume chake uongo ni katika madhambi makubwa sana. Soma Zaidi...

Kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila dini?
Mwanadamu hawezi kuishi bila dini, kwani dini imekusanya mfumo mzima wa maisha yake. Soma Zaidi...

Dalili Kubwa za kukaribia Siku ya kiama
Soma Zaidi...

Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu
Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo: (i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu. Soma Zaidi...

Kuangamizwa Waovu na Kuokolewa Waumini
Baada ya kuonywa wasionyeke, Allah(s. Soma Zaidi...